Kesi ya Lema: Maswali matano magumu kujibika, mepesi kuulizwa

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,504
La kwanza, iwapo kila mshtakiwa yuko huru hadi atakapokutwa na hatia na Mahakama na iwapo dhamana ni haki kwa kila mshtakiwa (ikiwa tu shtaka lake linadhaminika), kwanini kuna mkwamo mkubwa kwenye dhamana ya Mbunge Godbless Lema wa Arusha Mjini ikiwa mashtaka yake yanadhaminika?

La pili, iwapo Mshtaki/Jamhuri (Mkurugenzi wa Mashtaka nchini-DPP) ana kesi zenye ushahidi na uzito wa hoja dhidi ya mshtakiwa Godbless Lema na iwapo kuna nafasi ya kuharakisha upelelezi na kuanza kusikilizwa kwa kesi za msingi, kwanini Jamhuri inatumia nguvu kubwa kwenye suala la dhamana?

La tatu, Mawakili wa Lema kwasasa wanapaswa kufanya nini hasa wakati huu ambapo Jamhuri imeshafika Mahakama ya Rufaa kupinga ruhusa ya Lema kukata rufaa, dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi kukataa kutoa dhamana, nje ya muda?

La nne, Jamhuri ina sababu gani kubwa na ya kisheria ya kuzuia kupewa dhamana kwa mshtakiwa Godbless Lema kwa mashtaka mawili yanayomkabili?

La tano, siku Mbunge na mshtakiwa Lema akikataliwa kabisa dhamana au akikubaliwa dhamana na kuachiwa kuendelea na kesi zake akitokea uraiani, hali itakuwaje na kwa faida ya nani?
 
Suala la Lema kwa lilipofikia hivi sasa linaidhalilisha kabisa Mhimili wa Mahakama.

Uhuru ambao ulikuwepo kwenye Mhimili huu haupo tena.

Kesi hii inaendeshwa kwa namna dola wanavyotaka iwe.

Lakini kitu kimoja ninachokiamini katika kesi zitakazo kuja KUMJENGA sana Mh Lema ni hii hapa.

Muda utaongea.
 
Suala la Lema kwa lilipofikia hivi sasa linaidhalilisha kabisa Mhimili wa Mahakama.

Uhuru ambao ulikuwepo kwenye Mhimili huu haupo tena.

Kesi hii inaendeshwa kwa namna dola wanavyotaka iwe.

Lakini kitu kimoja ninachokiamini katika kesi zitakazo kuja KUMJENGA sana Mh Lema ni hii hapa.

Muda utaongea.
lema siasa imemshinda amegeuka kuwa nabii mwenye ndoto, si afungue kanisa
 
6. kwa nini mawakili zaidi ya 6 wasimaie kesi moja kwa kivuli cha cdm na wakati huo kuna kesi za kifisaidi nyingi ambazo chadema wanadai wanahushaidi kwa nini hizo wasizisimamie??
Mahakama ya mafisadi ipo na haina kesi hata moja, mwenye jukumu la kukamata ni polisi, jukumu la kushtaki ni la DPP.

Lakini vyombo vyote hivyo havioni ufisadi ila kipaumbele chao ni Lema.

Nchi ya kusadikika.
 
Lema na chadema wamepewa kazi ya kufanya, kwa kulitambua hilo uongozi wa juu chadema wamekataa kuicheza ngoma ya serikali hadharani kwa kukaa kimya though underground wanaicheza... ndio ukweli.

Nini kusudio la serikali? Ni kufifisha sauti za upinzani kwa kila wanalolifanya.

Watafanikiwa? Kwa sasa wanaelekea kufanikiw ila 2020 watajutia hili maana litawagharimu.
 
Ni vizuri umeuliza maswali haya, majibu yake lazima yaonyeshe udhaifu mkubwa kwa upande fulani lakini kikubwa zaidi ni matokeo ya kinachoendelea kuongeza 'upendo' au chuki kwa upande mmoja.
Niko hapa nafuatilia uzi wa tamko la kufuta tamko lingine la karo elekezi ambazo hazikuwahi kuwepo kimsingi!
 
La kwanza, iwapo kila mshtakiwa yuko huru hadi atakapokutwa na hatia na Mahakama na iwapo dhamana ni haki kwa kila mshtakiwa (ikiwa tu shtaka lake linadhaminika), kwanini kuna mkwamo mkubwa kwenye dhamana ya Mbunge Godbless Lema wa Arusha Mjini ikiwa mashtaka yake yanadhaminika?

La pili, iwapo Mshtaki/Jamhuri (Mkurugenzi wa Mashtaka nchini-DPP) ana kesi zenye ushahidi na uzito wa hoja dhidi ya mshtakiwa Godbless Lema na iwapo kuna nafasi ya kuharakisha upelelezi na kuanza kusikilizwa kwa kesi za msingi, kwanini Jamhuri inatumia nguvu kubwa kwenye suala la dhamana?

La tatu, Mawakili wa Lema kwasasa wanapaswa kufanya nini hasa wakati huu ambapo Jamhuri imeshafika Mahakama ya Rufaa kupinga ruhusa ya Lema kukata rufaa, dhidi ya uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi kukataa kutoa dhamana, nje ya muda?

La nne, Jamhuri ina sababu gani kubwa na ya kisheria ya kuzuia kupewa dhamana kwa mshtakiwa Godbless Lema kwa mashtaka mawili yanayomkabili?

La tano, siku Mbunge na mshtakiwa Lema akikataliwa kabisa dhamana au akikubaliwa dhamana na kuachiwa kuendelea na kesi zake akitokea uraiani, hali itakuwaje na kwa faida ya nani?
DUNIA NZIMA UKIACHIWA KWA DHAMANA HALAFU UKIWA NJE KWA DHAMANA UKATENDA KOSA HILO HILO ULILOSHITAKIWA NALO, NI SAWA NA UMEUA DHAMANA YAKO MWENYEWE.

LOGIC NI KWAMBA UNETENDA KOSA UMESHITAKIWA UKUSHINDWA LABDA UTANYONGA AU UTAFUNGWA. KUPEWA DHAMANA NI KUSUBIRI KESI IFIKIE UAMUZI UFUNGWE AU UACHIWE. UKITENDA KOSA HILO HILO UTANYONGWA MARA NGAPI.

KUMTUKANA MAGUFULI AU KUMTUKANA LOWASSA AU SLAA UAMUZI NI HUO HUO: LEMA ALISHITAKIWA LAZIMA ASUBIRI MAHAKAMA IAMUE.

HILO NDIYO JIBU LA MASWALI YAKO YOTE.

MAWAKILI WA LEMA EMA HAWAFAI AU WANA SABABU NYINGINE BINAFSI KUENDELEA KUMDANGANYA LEMA KUWA ATAACHIWA, SIJUI NI NANI ANAWALIPIA GHARAMA.

KULE KUMWINGIZA MRS LEMA HAIINGII AKILINI MPAKA LEO LABDA AULIZWE MR LEMA MWENYEWE. NI UJINGA.

MWISJO KABISA, KAMA LEMA ASINGEKATA HIZI RUFAA RUFAA ZA KITOTO KESI INGEKUWA INESHAISHA ZAMANI.

WA KULAUMIWA NI NANI? NI MAWAKILI WAKE, HAWAJAIVA. ASHAURIWE ATAFUTE WENGINE.
 
Jibu ni moja tu kwa maswali ya Petro. Nalo ni hili " Mhimili wangu una mizizi mirefu kuliko mihimili mingine kwa sababu mimi na mhimili wangu ndio natoa fedha na maelekezo mengine kwa mihimili mingine".
 
Kuhamasisha fujo na maandamano sio jambo jema. Lakini watu wa Arusha kama wanaona wanakomolewa kupitia Mbunge wao basi ni haki yao kuonyesha kutokubaliana na jambo hilo.
Wataonyeshaje kuwa hawakubaliani? Duniani kote wananchi wasiokubaliana na jambo lakini serikali yao haiwasikilizi wana riot mpaka waeleweke. Arusha mumekuwaje siku hizi? Mkikinukisha na dunia nzima itajua kuna nini na hapo watashangaa kwa nini Lema anafanyiwa hivyo mwakilishi wa wananchi?
Arusha msilale!
 
Kuhamasisha fujo na maandamano sio jambo jema. Lakini watu wa Arusha kama wanaona wanakomolewa kupitia Mbunge wao basi ni haki yao kuonyesha kutokubaliana na jambo hilo.
Wataonyeshaje kuwa hawakubaliani? Duniani kote wananchi wasiokubaliana na jambo lakini serikali yao haiwasikilizi wana riot mpaka waeleweke. Arusha mumekuwaje siku hizi? Mkikinukisha na dunia nzima itajua kuna nini na hapo watashangaa kwa nini Lema anafanyiwa hivyo mwakilishi wa wananchi?
Arusha msilale!
Mbowe yuko zake Dubai anakula bata , anza wewe na familia yako kuandamana
 
Wana muimalisha saana Lema...kwani ameshaingia kwenye vitabu vya historian ya africa
 
Suala la Lema kwa lilipofikia hivi sasa linaidhalilisha kabisa Mhimili wa Mahakama.

Uhuru ambao ulikuwepo kwenye Mhimili huu haupo tena.

Kesi hii inaendeshwa kwa namna dola wanavyotaka iwe.

Lakini kitu kimoja ninachokiamini katika kesi zitakazo kuja KUMJENGA sana Mh Lema ni hii hapa.

Muda utaongea.


endapo dola inaendesha itakavyo yenyewe basi kitakachotokea...namaanisha hukumu ..ambayo itakuwa ni kwa kosa la jinai itamfanya Lema asiwe na haki ya kikatiba kugombea nafasi za kisiasa...Na ataondolewa ubunge

Na hicho ndicho ninachokiona
 
Kuhamasisha fujo na maandamano sio jambo jema. Lakini watu wa Arusha kama wanaona wanakomolewa kupitia Mbunge wao basi ni haki yao kuonyesha kutokubaliana na jambo hilo.
Wataonyeshaje kuwa hawakubaliani? Duniani kote wananchi wasiokubaliana na jambo lakini serikali yao haiwasikilizi wana riot mpaka waeleweke. Arusha mumekuwaje siku hizi? Mkikinukisha na dunia nzima itajua kuna nini na hapo watashangaa kwa nini Lema anafanyiwa hivyo mwakilishi wa wananchi?
Arusha msilale!

Hivi mkuu hujiulizi kwa nini chama chetu kimesinyaa sana siku hizi?

Tatizo ni mbowe mkuu...amekuwa diluted na Lowasaism

Can you imagine mbunge wa chama yuko jela siku zote hizo na mwenyekiti wa chama hajawahi kuthubutu hata kwenda kumuona
 
Back
Top Bottom