Kesi ya kina Mdee dhidi ya CHADEMA kuhusu kuvuliwa uanachama haina tija ni ubadhilifu mwingine

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,418
7,206
Hili suala la mamlaka nchini kuonekana kutumia nguvu isiyokua ya kawaida kuidhibiti chadema isiweze kuwavua wanachama wake uanachama linastaajabisha wengi.

Tumeona na kuzoea kuona chama cha mapinduzi kuweza kumng'oa kirahisi mbunge wake anayeenda kinyume na chama bungeni kwa kumfuta uanachama.

Hili linawezekana kutokana na haki iliyokua nayo chama cha siasa kumfuta mwanachama wake uanachama kufuatana na katiba na taratibu waliyojiwekea.

Akina Halima mdee baada ya chama chao kuona walifanya ulaghai kuteuliwa kuwa wabunge viti maaluum kwa kugushi nyaraka kiliwafukuza uanachama.

Katika hali ya kawaida speaker alitakiwa kusitisha ubunge wao ila la ajabu danadana zinaendelea wakiendelea kula mishahara na posho za ubunge karibu mwaka wa pili utaisha.

Inaelekea fedha inatumika kuhakikisha wanabakia wabunge ikiwezekana kwa muhula wote wa miaka mitano huku wakiwa sio wanachama wa chama chochote.

Haki ya kumtimua mtu uanachama isiwe jambo gumu kwa chama chochote cha siasa. Ukiona linaingiliwa na utawala hadi mahakama basi kuna matatizo makubwa kuhusu demokrasia nchini.
 
Kuna upande mara nyingi hudhani wanawakomoa CHADEMA.Nakuhakikishia ndiyo kwanza wanazidi kuwapa ujasiri.Na hilo si kwa CHADEMA tu,bali kwa wananchi walio wengi.

Imezoeleka kuwa,wananchi wengi huogopa na kukataa kwenda mahakamani kwa hofu ya kupoteza shauri.Au mara nyingine, kwa kutojua taratibu za kimahakamani na kuogopa tu ile hali ya kuwepo pale, huwa wanazikimbia kesi na kujipotezea haki zao.Sasa ni muda Watanzania wamejua kuwa mahakamani ndiyo sehemu sahihi ya kupata haki.
 
Usihangaike na Wajinga
Huyo siyo "mjinga", bali ni MPUMBAVU.

Wakati nikirekebisha hilo, mara nikaingiwa na swali la 'kijinga', na nikaona niliwasilishe kwako.

Hivi CHADEMA hawawezi kwenda mahakamani na kuweka pingamizi la hao wabunge kujitambulisha kama wabunge wa CHADEMA?
Wakiweka zuio hilo, na mahakama ikaridhia, sijui itakuwaje?
Hili ni swali tu, mkuu wangu Erythro., kama unajibu lake natanguliza shukrani.
 
Hili suala la mamlaka nchini kuonekana kutumia nguvu isiyokua ya kawaida kuidhibiti chadema isiweze kuwavua wanachama wake uanachama linastaajabisha wengi.

Tumeona na kuzoea kuona chama cha mapinduzi kuweza kumng'oa kirahisi mbunge wake anayeenda kinyume na chama bungeni kwa kumfuta uanachama.

Hili linawezekana kutokana na haki iliyokua nayo chama cha siasa kumfuta mwanachama wake uanachama kufuatana na katiba na taratibu waliyojiwekea.

Akina Halima mdee baada ya chama chao kuona walifanya ulaghai kuteuliwa kuwa wabunge viti maaluum kwa kugushi nyaraka kiliwafukuza uanachama.

Katika hali ya kawaida speaker alitakiwa kusitisha ubunge wao ila la ajabu danadana zinaendelea wakiendelea kula mishahara na posho za ubunge karibu mwaka wa pili utaisha.

Inaelekea fedha inatumika kuhakikisha wanabakia wabunge ikiwezeka kwa muhula wote wa miaka mitano huku wakiwa sio wanachama wa chama chochote.

Haki ya kumtimua mtu uanachama isiwe jambo gumu kwa chama chochote cha siasa. Ukiona linaingiliwa na utawala hadi mahakama basi kuna matatizo makubwa kuhusu demokrasia nchini.
NI AIBU KWA NCHI ILIYOKUWA YA UCHUMI WA KATI IMEPOROMOKA NA KURUDI NCHI MASIKINI INAWAPIGANIA WABUNGE FAKE KWA KUWATETEA kwa NGUVU KUBWA NA kuendelea KUWALIPA MISHAHARA NA POSHO AMBAZO NI KODI ZA MASIKINI
 
Kuna upande mara nyingi hudhani wanawakomoa CHADEMA.Nakuhakikishia ndiyo kwanza wanazidi kuwapa ujasiri.Na hilo si kwa CHADEMA tu,bali kwa wananchi walio wengi.

Imezoeleka kuwa,wananchi wengi huogopa na kukataa kwenda mahakamani kwa hofu ya kupoteza shauri.Au mara nyingine, kwa kutojua taratibu za kimahakamani na kuogopa tu ile hali ya kuwepo pale, huwa wanazikimbia kesi na kujipotezea haki zao.Sasa ni muda Watanzania wamejua kuwa mahakamani ndiyo sehemu sahihi ya kupata haki.
SAHIHI!!!
 
Back
Top Bottom