Kesi ya kina Mbowe: Wakili John Mallya naye alimbananisha SSP Ngichi

chidayo

JF-Expert Member
Sep 5, 2016
435
870
_
MALYA: Ulipojiunga na Jeshi la polisi ulikuwa na miaka mingapi?

SSP Ngichi: 28

MALYA: Kwa mujibu wa PGO ni sahihi kwamba mtu akiwa na miaka 28 haruhusiwi kujiunga na jeshi la Polisi?

SSP Ngichi: Inategemea na elimu yake

MALYA: Kesi unayoitolea ushahidi inahusiana na maswala ya uchaguzi, nyie kama wadau mlipewa elimu ya usimamizi wa uchaguzi?

SSP Ngichi: Natolea ushahidi kesi ya maandamano sio mambo ya uchaguzi

MALYA: Lakini hayo maandamano si yanatokana na uchaguzi?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Ulipewa ratiba ya mikutano ya vyama vya siasa?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Nani alikupatia?

SSP Ngichi: RPC Kinondoni

MALYA: Yeye alipewa na nani?

SSP Ngichi: Mkurugenzi wa Manispaa Kinondoni

MALYA: Kifungu cha 51 (5) cha sheria ya Uchaguzi kinamtaka Mkuu wa Wilaya ndiye awape polisi nakala ya Ratiba za kampeni. Kwa kifungu hiki, huoni kwamba mmevunja sheria?

SSP Ngichi: Kimya

MALYA: Vituo vya kupiga kura vilikuwa vingapi?

SSP Ngichi: Sikumbuki idadi yake

MALYA: RCO unasimamiaje uchaguzi ambao hujui hata idadi ya vituo?

SSP Ngichi: Vilikua zaidi ya hamsini

MALYA: Unafahamu mawakala lazima wale kiapo?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Unafahamu kila mgombea anaweka utaratibu na Mkurugenzi wa namna mawakala wake kuapa?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Kwahiyo mlifanya makosa kuvuruga mawakala wa Chadema kwenda kuapa?

SSP Ngichi: Walifanya maandamano

MALYA: Ulijuaje ni maandamano?

SSP Ngichi: Walivuka barabara

MALYA: kama walivuka barabara ulijuaje kama walikuwa wanafanya kampeni za nyumba kwa nyumba?

SSP Ngichi: Hazifanyiki barabarani

MALYA: Zinafanyika wapi?

SSP Ngichi: Nyumbani

MALYA: Ili ufike nyumbani unapita wapi?

SSP Ngichi: Barabarani

MALYA: Kwahiyo unakubali walikua wanavuka barabara ili wakafanye kampeni za nyumba kwa nyumba?

SSP Ngichi: Waliandamana

MALYA: Kwanini?

SSP Ngichi: Kwa sababu walikua na viongozi wao

MALYA: Wataje

SSP Ngichi: Heche, Matiko, Msigwa na wengine

MALYA: Unajua sifa za mtu kuwa wakala?

SSP Ngichi: Hapana

MALYA: Unajua kuwa Heche, Matiko na Msigwa walikua mawakala?

SSP Ngichi: Sifahamu

MALYA: Je unakubali kwamba viongozi hao walikua wanaongozana na mawakala wenzao kwenda kwa Mkurugenzi kula kiapo?

SSP Ngichi: Kimya
 
Sehemu ya mahojiano kati ya Wakili msomi John Malya na Mkuu wa upelelezi mkoa wa kipolisi Kinondoni, Mrakibu mwandamizi wa Polisi (SSP) Gerald Ngichi.

MALYA: Una miaka mingapi?

SSP Ngichi: 47

MALYA: Ulizaliwa mwaka gani?

SSP Ngichi: 1972

MALYA: Wakati unajiunga na Jeshi la Polisi ulikuwa na Miaka mingapi?

SSP Ngichi: Kimya

HAKIMU: Shahidi jibu tafadhali

MALYA: Kama hukumbuki nikusaidie?

SSP Ngichi: Nilikua na miaka 28

MALYA: Ulikuwa na taaluma gani?

SSP Ngichi: Degree ya Sheria

MALYA: Kwa mujibu wa PGO ni sahihi kwamba mtu akiwa na miaka 28 haruhusiwi kujiunga na jeshi la Polisi?

SSP Ngichi: Inategemea na elimu yake

MALYA: Kesi unayoitolea ushahidi inahusiana na maswala ya uchaguzi nyinyi kama wadau mlipewa elimu juu ya usimamizi wa uchaguzi?

SSP Ngichi: Natolea ushahidi kesi ya maandamano sio mambo ya uchaguzi

MALYA: Lakini hayo maandamano si yanatokana na uchaguzi?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Ulipewa ratiba ya mikutano ya vyama vya siasa?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Nani alikupatia?

SSP Ngichi: RPC Kinondoni

MALYA: Yeye alipewa na nani?

SSP Ngichi: Mkurugenzi wa Manispaa Kinondoni

MALYA: Kifungu cha 51 (5) cha sheria ya Uchaguzi kinamtaka Mkuu wa Wilaya ndiye awape polisi nakala ya Ratiba za kampeni. Kwa kifungu hiki, huoni kwamba mmevunja sheria?

SSP Ngichi: Kimya

MALYA: Vituo vya kupiga kura vilikuwa vingapi?

SSP Ngichi: Vingi sikumbuki idadi yake

MALYA: Unasimamiaje uchaguzi ambao hujui hata idadi ya vituo?

SSP Ngichi: Vilikua zaidi ya Hamsini

MALYA: Unafahamu mawakala lazima wale kiapo?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Unafahamu kila mgombea anaweka utaratibu na Mkurugenzi wa namna mawakala wake kuapa?

SSP Ngichi: Ndio

MALYA: Kwahiyo mlifanya makosa kuvuruga mawakala wa Chadema kwenda kuapa?

SSP Ngichi: Walifanya maandamano yasiyo halali

MALYA: Ulijuaje ni maandamano?

SSP Ngichi: Walivuka barabara

MALYA: kama walivuka barabara ulijuaje kama walikuwa wanafanya kampeni za nyumba kwa nyumba?

SSP Ngichi: Hazifanyiki barabarani

MALYA: Zinafanyika wapi?

SSP Ngichi: Nyumbani

MALYA: Ili ufike nyumbani unapita wapi?

SSP Ngichi: Barabarani

MALYA: Kwahiyo unakubali walikua wanavuka barabara ili wakafanye kampeni za nyumba kwa nyumba?

SSP Ngichi: Waliandamana

MALYA: Kwanini?

SSP Ngichi: Kwa sababu walikua na viongozi wao

MALYA: Wataje

SSP Ngichi: Heche, Matiko, Msigwa na wengine

MALYA: Unajua sifa za mtu kuwa wakala?

SSP Ngichi: Hapana

MALYA: Unajua Heche alikua Wakala?

SSP Ngichi: Sifahamu

MALYA: Unajua Matiko alikua wakala?

SSP Ngichi: Sifahamu

MALYA: Unajua Msigwa alikua Wakala?

SSP Ngichi: Sifahamu

MALYA: Je unakubali kwamba viongozi hao walikua wanaongozana na mawakala wenzao kwenda kwa Mkurugenzi kula kiapo?

SSP Ngichi: Kimya


Hawa jamaa watamuua huyu SSP NGICHI
FB_IMG_1557920104464.jpeg
 
MALYA: Vituo vya kupiga kura vilikuwa vingapi?

SSP Ngichi: Sikumbuki idadi yake

MALYA: RCO unasimamiaje uchaguzi ambao hujui hata idadi ya vituo?


Ni sawa na kumtaka mwanafunzi (STD VII, F4, F6, UE nk.k) ajue wanafunzi wanaofanya mtihani ni wangapi.

"These qn even if are not answered, they do not go to the root of the case"
 
Inategemea na charge sheet ilivyokuwa drawn. Je waliweka zile ingrindients za uchochezi.
hapana
? The Newspapers Act [Cap 229 R.E. 2002] does not define this term. However, section 31 of the Act provides for what constitutes seditious intention. It says seditious intention is an intention

a) To bring into hatred or contempt or to excite disaffection against the lawful authority of the United Republic of Tanzania or the Government thereof;

b) To excite any of the inhabitants of the United Republic to attempt to procure the alteration, otherwise than by lawful means of any other matter in the United Republic as by law established;

c) To bring into hatred or to excite disaffection against the administration of Justice in the United Republic;

d) To raise discontent or disaffection amongst any of the inhabitants of the United Republic;

e) To promote feelings of ill-will and hostility between different categories of the population of the United Republic; It follows therefore that any publication is said to be seditious if it fits in any one of the above described seditious intentions. Besides providing for seditious intentions the Act also offers a yardstick for determination of whether act done, words spoken or document published is seditious. This is provided under section 31 (3) of the Newspaper Act which provides:- “In determining whether the intention with which any act was done any words spoken or any document was published, was or was not seditious, every person shall be deemed to intend the consequences which would naturally follow from his conduct at the time and in the circumstances in which he so conducted himself” In my view for an act, word spoken or document published to be held to be seditious such act, spoken words or publication need to be followed by certain consequences. It is my further humble view that mere publication without consequences of causing hatred, contempt, excitation of disaffection, attempt to procure alteration of any matter by unlawful means, to raise discontent and promoting feelings of ill-will cannot amount to sedition.
copied from Mtikila case on sedition
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom