Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 48,851
- 18,948
Kesi ya Karamagi yafutwa
Na Rabia Bakari
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imefuta kesi ya wizi iliyokuwa ikimkabili Bi. Nadya Karamagi, baada mlalamikaji katika kesi hiyo Bi. Maselina Rweyemamu, kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta kesi.
Akitoa uamuzi wa kufuta kesi hiyo, Hakimu Mkuu Mkazi, aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Bw. John Msafiri, alisema kuwa kesi hiyo imefutwa chini ya kifungu cha sheria namba 224 cha mwenendo wa makosa ya jinai (CPA).
Katika kesi ya msingi iliyokuwa ikikambili Bi. Karamagi ambaye ni raia wa Urusi, ilidaiwa kuwa Juni 17 mwaka huu katika maeneo ya Osterbay Kinondoni, aliiba simu na cheni ya dhahabu vyote vikiwa na thamani ya sh. 245,000 mali ya mlalamikaji.
Awali, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama aliiomba mahakama kumnyima dhamana mtuhumiwa kwa kuwa si raia wa Tanzania au awasilishe hati ya kusafiria mahakamani hapo, masharti ambayo mtuhumiwa aliyakamilisha na hatimaye kupewa dhamana.
Wakati wa kufuta kesi hiyo, Bw. Sisiwaya alisema kuwa upande wa mashtaka hauna pingamizi na ombi la mlalamikaji kwani amekubali kuyamalizia nyumbani.
Na Rabia Bakari
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, imefuta kesi ya wizi iliyokuwa ikimkabili Bi. Nadya Karamagi, baada mlalamikaji katika kesi hiyo Bi. Maselina Rweyemamu, kuwasilisha barua ya maombi ya kufuta kesi.
Akitoa uamuzi wa kufuta kesi hiyo, Hakimu Mkuu Mkazi, aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Bw. John Msafiri, alisema kuwa kesi hiyo imefutwa chini ya kifungu cha sheria namba 224 cha mwenendo wa makosa ya jinai (CPA).
Katika kesi ya msingi iliyokuwa ikikambili Bi. Karamagi ambaye ni raia wa Urusi, ilidaiwa kuwa Juni 17 mwaka huu katika maeneo ya Osterbay Kinondoni, aliiba simu na cheni ya dhahabu vyote vikiwa na thamani ya sh. 245,000 mali ya mlalamikaji.
Awali, Mwendesha Mashtaka wa Mahakama aliiomba mahakama kumnyima dhamana mtuhumiwa kwa kuwa si raia wa Tanzania au awasilishe hati ya kusafiria mahakamani hapo, masharti ambayo mtuhumiwa aliyakamilisha na hatimaye kupewa dhamana.
Wakati wa kufuta kesi hiyo, Bw. Sisiwaya alisema kuwa upande wa mashtaka hauna pingamizi na ombi la mlalamikaji kwani amekubali kuyamalizia nyumbani.