Kesi Ya Dr. Slaa, ushahidi ni wa kutungwa

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Nimekuwa nikiifuatilia kesi hii kwa karibu sana na jambo la kukatisha tamaa na kusikitisha ni kuwa mashahidi wa CCM wamepeleka ushahidi wa uongo mahakamni.

Hapa ni mchezo wa kumfanya Dr. Slaa awe bize muda wote na haswa wakati huu ambapo ripoti ya BOT inafanyiwa kazi.... ili kupunguza kelele za mjadala wake ,

Nafikiri kama shahidi anakiri kuwa vielelezo vimepikwa hakuna haja ya kupoteza muda wa slaa any more,

Someni hapa , source mwananchi.

Posted Date:12/4/2007

Shahidi akiri kuwasilisha vielelezo vya kugushi
Na Mussa Juma, Arusha

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya kupinga matokeo ya Jimbo la Karatu, Joseph Haimu(3, amebanwa na wakili wa upande wa utetezi, Tundu Lissu na kukiri kuwa baadhi vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo vimegushiwa.

Haimu alidai, fomu za matokeo ya uchaguzi zilizowasilishwa na mahakamani hapo na upande wao, zina baadhi ya vipengele ambavyo vimefutwa.

Akihojiwa na Lissu, anayemtetea mlalamikiwa wa pili, Mbunge wa Karatu (Chadema), Dk Wilbroad Slaa, shahidi huyo alidai hatambui aliyegushi matokeo hayo kwani, fomu walizokuwa wanatumia kama ushahidi wao walipata kutoka kwa mawakala wa CCM.

Haimu alikiri kuwa hata fomu zilizokuwa na alama za siri katika matokeo hayo ambazo zimewasilishwa mahakamani hapo kama vielelezo baadhi vina upungufu.

Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano kati ya wakili Lissu na shahidi huyo:

Lissu: Je, unatambua fomu hii kama kilelelezo P 39 ambacho mlikiwakilisha mahakamani ambayo ni matokeo ya Kituo cha Ngiting na unaweza kutusomea?

Shahidi: Najua. Mgombea wa ubunge wa CCM alipata kura, 124, CHADEMA 69, NCCR 1 na CUF 0.

Lissu: Je, hii fomu ina upufungu unaouona?

Shahidi: Ndio, kwenye matokeo ya Chadema inaonekana kama namba moja imefutwa kabla ya 69.

Lissu: Kwa hiyo unaithibitishia mahakama kuwa kuna kufutwatutwa hapo?

Shahidi: Ndio, ila naomba nitoe ufafanuzi kidogo.

Jaji Robert Makaramba anayesikiliza kesi hiyo anaingilia kati na kusema: "Wewe jibu swali la wakili kama hataki maelezo".

Lissu: Mimi sitaki ufafanuzi huo nataka ujibu ndio au hapana!

Shahidi: Ndio.

Lissu: Naomba usome kielelezo P 43 cha fomu 21B matokeo ya kituo hicho yanasomekaje?

Shahidi: CCM 124, CHADEMA 109 na NCCR 1

Lissu: Je, kuna tofauti ya kura ngapi za Chadema ambazo hazipo katika kielelezo p 39?

Shahidi: Kura 40.

Lisssu: Je, ni nani aliyefuta namba moja na kuifanya sifuri kuwa sita, ni wewe au ni nani?

Shahidi: Sijui!

Pia, wakili huyo alitoa fomu nyingine mbalimbali ambazo zimewasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashtaka ambazo matokeo yake yanatofautiana na matokeo ya Tume ya

Uchaguzi na matokeo ya kumbukumbu za Chadema.

Awali, shahidi huyo alisema fomu za matokeo ambazo wamekuwa wakizilalamikia zilikuwa hazina alama ya siri, hivyo ni rahisi kugushiwa, ingawa alidai hata hizo zenye alama ya siri pia zina upungufu.

Baada ya mahojiano hayo yaliyochukua takriban saa 4:00, Jaji Makaramba aliahirisha kesi hadi leo na shahidi huyo anatarajia kuendelea kuhojiwa na upande wa utetezi.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa wa kwanza ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anayetetewa na Patience Mgwina na mshtakiwa wa pili ni Dk Slaa, ambaye awali hakuwepo kwenye kesi hiyo baada ya kuomba kujumuishwa.
 
Kumbe hii kesi Slaa ameomba kuingizwa na kwamba mlalamikiwa ni AG.Anyway, labda aliona ni muhimu naye aingie ili kumdhibiti AG maana haaminiwi mtu hapa.Japo wote ni wa upande mmoja, mtu aweza kuuzwa hapa.
 
Angemwachia AG angeweza kuuzwa kwani wangeweza kufuta matokeo hayo na hii ilikuwa ni kesi ya kutumia mbinu kuwa Slaa hajashitakiwa ili asiende huko kwa pilato na baadae watoe hukumu kuwa serikali imeshindwa na kutengua matokeo.

Ndio maana hujawahi kusikia mawakili wa serikali wakiwabana hawa mashahidi hata mara moja kwani hawakujua kuwa mchezo wao na Slaa .

Hapa ni kupoteza muda tuu kwani hata ushahidi hawana na wapo wapo tuu naambiwa kuna kigogo mmoja mwenye mkopno hapo ili kumngoa Slaa ......
 
Haya maji marefu, wakiangalia vibaya watazama! Ni kazi sana kumfundisha mtu kuufanya uongo ugeuke ukweli. Tundu Lissu ubarikiwe na kaza buti mpaka kielweke!
 
CCM has been used to take us Tanzanians for a ride. Kama Mahakama ikithibitisha kuwa hawa watu (CCM cadres) wameghushi hizo fomu ili kujipatia ushindi wa Kimahakama kwa hila basi Dk. Slaa, his Lawyers and Poice must take stern actions against them maana ni kosa la jina kughushi na kupeleka ushahidi wa Uongo Mahakamani.
 
Hongera sana Tindu Lissu kwa machimbo hayo unayoyafanya maana kwa kweli inaelekea walikuwa wamejizatiti sana nia yao hao ni moja tu kumwondoa Dr Thlaa (Slaa) katika kiti chake cha enzi kwa kuwa ameitikisa CCM na orodha yake ya mafisadi. Tupo nanyi Chadema.
 
Haya maji marefu, wakiangalia vibaya watazama! Ni kazi sana kumfundisha mtu kuufanya uongo ugeuke ukweli. Tundu Lissu ubarikiwe na kaza buti mpaka kielweke!

My Man Tundu Lissu, kumbe ni mtundu eeehhh. Kwa kweli hao mashahidi watakiona cha mtema kuni kwa uvivu wa kuchagua. Kama aliweza kuwataja mafisadi wa ikulu hadharani atashindwa kweli kuwaanika hao mafisadi walioghushi ushahidi? Lol

Asha
 
Hawa jamaa inasemekana kuwa ni makda ambao hawana cha kupoteza klwani ni watu wa kawaida sana na inaelekea waliwekwa hao ili hata kama kutakuja kuwa na kesi za kuwadai gharama basi mahakama isemae hawana uwezo hawa.

Ila wamegushi nyaraka nyingi sanan sana mpaka inatia aibu.
 
Hawa jamaa inasemekana kuwa ni makda ambao hawana cha kupoteza klwani ni watu wa kawaida sana na inaelekea waliwekwa hao ili hata kama kutakuja kuwa na kesi za kuwadai gharama basi mahakama isemae hawana uwezo hawa.

Ila wamegushi nyaraka nyingi sanan sana mpaka inatia aibu.

Hao kesi ikiisha, ama hata kabla haija isha, dawa yao Lissu awafungulie kesi ya kugushi nyaraka za serikali?? naamini itakuwa ni fundisho kwa wengine!

Afu kumbuka mahakimu sasa hivi wana donge kwa vile wanakandamizwa kwamba ni wala rushwa, hivo itakuwa kazi sana kupokea chochote ili kuwaachia hao jamaa.. sheria itawapata! Japo cjui adhabu ya kughushi nyaraka ni kali kiasi gani.
 
News Alert:

Mahakama huko Karatu imeamuru upande wa mashtaka kuleta nakala halisi katika vielelezo vya ushahidi wao. Hiyo imetokea baada ya wakili wa wa utetezi kushinda hoja mbele ya hakimu kuwa kutokana na baadhi ya nyaraka kuonekana ni za kughushi, anataka nakala halisi na siyo za vivuli ziletwe.
 
Mmhhh si muache mambo ya watu ya mahakama yaishi, si mutajadili kumbe siku hizi nanyi mumekuwa majaji du! ushabiki kitu kibaya sana
 
Tatizo ni kuwa hawa jamaa wako kifisadi fisadi tuu.

Wamepewa hadi j4 wawe wameleta nyaraka halisi mahakamani sijui watazitoa wapi na hapo ndio patakuwa patamu kwelikweli tusubiri ili tuone mambo yanavyokwenda .
 
Vumbi kesi ya Dk. Slaa

na Mustafa Leu

UTATA unaotokana na tofauti za takwimu umeibuka mahakamani wakati kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Karatu, Dk. Willbrod Slaa (CHADEMA) ilipokuwa ikiendelea kusikilizwa jana.
Kuibuka kwa utata huo kulikuja baada ya aliyekuwa wakala wa jimbo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Joseph Hayim, kuwasilisha takwimu alizodai kuwa ni za matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005 zinazotofautiana na zile za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Katika kesi hiyo ambayo wanachama watatu wa CCM wanapinga ushindi wa Dk. Slaa, wakala huyo anadaiwa kuwasilisha majina ya baadhi ya vituo vya kupigia kura ambavyo havimo katika orodha ya vituo rasmi vya NEC.

Wakala huyo ambaye ni shahidi wa walalamikaji, aliiambia Mahakama Kuu Kanda ya Arusha inayosikiliza kesi hiyo kwamba, matokeo katika kituo cha Shangit B yaliyoandaliwa na CCM yalikuwa hayafanani na matokeo sahihi ya NEC.

Hayim alidai mahakamani hapo kuwa kutokana na tofauti hiyo ya matokeo kati ya yale ya NEC na aliyoletewa na mawakala wa chama hicho kutoka vituoni ni vigumu kujua ni mgombea gani wa ubunge kati ya yule wa CCM au CHADEMA (Slaa) alishinda.

Shahidi huyo alidai pia kuwa, katika kituo kingine cha Mamsai kulikuwa na tofauti katika fomu za CCM na zile za NEC na hivyo kuleta utata wa kutojulikana mshindi halisi.

Katika kituo kingine cha Njia Panda, Hayim alidai hakukuwa na kituo kama hicho, ingawa katika fomu za CCM zimeonyeshwa kilikuwepo na karatasi zake za malalamiko ziliwasilishwa kwa bahati mbaya mahakamani kama kielelezo.

Aliiambia mahakama hiyo kuwa yeye alipokea karatasi za matokeo kutoka kwa mawakala wa Chama chake Cha Mapinduzi ambazo zilionyesha kuwepo kwa kituo cha Njia Panda, lakini ukweli ni kuwa kituo hicho hakikuwepo.

Alipoulizwa na Wakili Tundu Lissu, anayemtetea Dk. Slaa kuhusu taarifa za kituo kimoja kuwa na fomu mbili za matokeo, shahidi huyo alisema kuwa swali hilo hawezi kulijibu na alikuwa anaiachia mahakama, kwani kila kituo kilikuwa na fomu moja ya matokeo na fomu 20 za CCM zilizoongezeka zilipelekwa mahakamani kwa bahati mbaya.

Akiendelea kutoa ushahidi, alisema kuwa katika kituo cha Getamol, matokeo yalibadilishwa na yale ya CCM yakawekwa kama ya CHADEMA na ya CHADEMA yakaandikwa kama ya CCM, na taarifa ya msimamizi wa uchaguzi inaonyesha kuwa CHADEMA ilishinda kwa kura 79 katika kituo hicho.

Alipotakiwa kutoa ufafanuzi ni fomu zipi basi za matokeo zipokelewe na mahakama kama kielelezo, alisema yeye amezileta mahakamani ili mahakama ndiyo iangalie.

Shahidi huyo alikiri kuwapo kwa fomu ambazo ziliandaliwa na CCM zinazoonyesh matokeo, ingawa hazina majina na sahihi za mawakala, na nyingine zilizowasilishwa mahakamani hapo kwa makosa ambayo yalitokea katika vituo vya kupigia kura wakati wa kuzijaza.

Hayim aliiambia mahakama hiyo kuwa mawakala wote 253 wa CCM hawakujaza fomu za malalamiko ya matokeo, ingawa walikuwa na haki ya kufanya hivyo kupitia fomu namba 16 inayotolewa na msimamizi wa uchaguzi kwa madai kuwa walinyimwa.

Alidai pia kuwa katika matokeo hayo, CCM iliandaa taarifa yenye kuchanganya kura za madiwani na kuzifanya kuwa ndizo za wabunge.

Kuhusu hilo, alieleza kuwa, walalamikaji wenzake walibadilisha herufi moja katika fomu kwenye kituo cha Mango'ra kwa kuongeza herufi A, badala ya ile ya awali, ambapo hakuna herufi hiyo, na taarifa yake aliyoiandaa ilikuwa haina muhuri wa msimamizi na akaiomba mahakama iikubali.

Aliiambia mahakama kuwa alipokea fomu hizo Novemba 25 mwaka 2006, na siku iliyofuata wakafungua kesi. Shahidi huyo ataendelea kutoa ushahidi wake leo.
 
Shahidi kumpinga Slaa akiri fomu za madai zina utata

Na Mussa Juma, Arusha.


KESI ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Jimbo la Kararu, iliendelea jana ambapo shahidi wa kwanza wa upande mashitaka, Joseph Haimu aliimbia mahakama kuwa ni baadhi tu ya waliokuwa mawakala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) walalamikia matokeo hayo. CCM ilikuwa na mawalaka 253.


Katika uchaguzi huo, Mgombe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilibrod Slaa alimshinda mgombea wa CCM Patrick Tsere.


Akihojiwa na Wakili wa Utetezi, Tundu Lissu Shahidi huyo pia alikiri kuwa fomu za matokeo ambazo wamewasilisha mahakamani hapo baadhi matokeo yake ?yamegushiwa?.


Sehemu ya mahojiano baina ya Lissu na shahidi huyo ambaye ni mmoja ya waliofungua kesi ya kupinga matokeo hayo yalikuwa hivi.


Wakili: katika uchaguzi wa Karatu ni kweli CCM ilikuwa na mawakala katika vituo vyote.


Shahidi: Ndio


Wakili: Je ni kweli kuwa CCM ilikuwa na mawakala 253 na kati yao ni Emanuel Bura ambaye ni mmoja wa walalamikaji katika kesi hii.


Shahidi: Ni kweli.


Wakili: Je, katika uchaguzi wa Karatu kuna wakala ambaye alijaza fomu za kulalamikia matokeo kwenye fomu ya Tume ya Uchaguzi namba 16.


Shahidi: Hakuna ila nina sababu kwani walinyimwa fomu.

Wakili: Katika malalamiko yenu ya kupinga matokeo mbona hili halipo kama mawakala wote walinyimwa fomu na msimamizi wa uchaguzi.


Shahidi: Kimya


Awali Lissu aliwasilisha mahakamani hapo vielelezo vya fomu za matokeo ambazo zimewasilishwa mahakamani hapo ambazo zinabadilishwa matokeo.


Wakili: Naomba utusomee vielelezo P255 na D257 ambazo ni fomu za matokeo na je ni za kituo kimoja au la.


Shahidi. Ni za kituo kimoja cha Mang?ola NTC, P2555 CCM kura 172, CHADEMA kura 122 na D 257 CCM kura 122 na CHADEMA kura 172.


Wakili: Je, ni kweli matokeo yamepinduliwa.


Shahidi: Ndio


Wakili: Je, haya ni matokeo ya kituo kimoja


Shahidi: Ndio


Wakili: Matokeo ya fomu P255 yamesainiwa na yana jina la wakala wa Chadema na

jina lake


Shahidi: Hayajasainiwa na wakala na jina halionekani vizuri.


Jaji: Robert Makaramba anayesikiliza kesi anachukuwa fomu na kuitazama anaguna

kisha anamrudishia Lissu.


Wakili: Je matokeo ya D257 ambayo ndio ya tume ya uchaguzi yamesainiwa na mawakala


Shahidi Ndio.


Wakili: Jina lake ni nani?


Shahidi: Abasi Maoi


Wakili: Sasa mlipoleta fomu mbili za kituo kimoja mnataka jaji afuate ipi.


Shahidi: Ni uamuzi wa mahakama


Wakili: Msomee jaji fomu hizi, P 254 na D 258 ambazo ni za kituo kimoja cha Kandel

C, Barai


Shahidi: P 254 CCM kura 136 na CHADEMA kura 115 na D254, CCM 115 na CHADEMA 136.


Wakili: Ebu tusomee orodha ya matokeo yenu ya kifupi ya kata zote katika kielelezo

chenu namba P 256 kwa kituo hicho hicho.


Shahidi: CCM kura 115 na CHADEMA kura 36.


Wakili: Je, hapa tena jaji afuate fomu ipi na inaonekana tena mmepunguza kura 100

za CHADEMA na katika malalamiko yenu mnadai mlishinda kwa tofauti ya kura 177?


Shahidi: Mahakama itaamuwa.


Wakili: ni nani ambaye amepindua matokeo haya?


Shahidi :Sijui.


Wakili: Msomee jaji fomu D261 , D 256 na P 253. Je, matokeo yanafanana?


Shahidi: Ndio, isipokuwa kwenye p253 neno A limeongezwa.


Jaji: Wewe jibu swali unaloulizwa, unajua hapa ni sawa na polisi lazima uwe makini

na maelezo yako.


Wakili: Ni nani kaongeza?


Shahidi:sijui


Kesi hiyo ambayo inavuta umati wa watu inaendelea leo na shahidi huyo ataendelea kuhojiwa na wakili Lissu.


Katika kesi hiyo, Haimu na wenzake wanadai kuwa uchaguzi haukuwa wa haki kwani taratibu kadhaa zilikiukwa ikiwepo kuwepo fomu feki na pia kama matokeo yangehesabiwa vizuri CCM ilishinda ubunge kwa tofauti ya kura 177.

source, Mwananchi.

Haya vimbwanga vinaendelea mahakamani na naambiwa kuwa jumamosi hii DR.Slaa na Lissu watafanya mkutano mkubwa wa hadhara mjini Arusha na pia watapokewa kwa maandamano makubwa yaliyoandaliwa na wananchi wa Arusha.
 
Shahidi: CCM isingeshinda Karatu

na Mustafa Leu, Arusha

KATIKA kauli inayoongeza utata katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa Jimbo la Karatu, shahidi wa kwanza wa upande wa walalamikaji, jana aliiambia mahakama kuwa hata kama mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) angepewa kura ambazo hazijulikani zilipo, asingeibuka mshindi.

Shahidi huyo, Joseph Hayim, akihojiwa na wakili anayemtetea Dk. Willbrod Slaa (CHADEMA), Tindu Lissu, alisema kuwa katika uchaguzi huo, Dk. Slaa alipata kura 34,754 na mgombea wa CCM, Patrick Tsere, alipata kura 30,928.

Alisema kuwa kura 2,961 zilikataliwa na hazijulikani zilikokwenda, lakini hata kama kura hizo zingekubaliwa na kugawanywa kwa wagombea wote sita wa ubunge katika jimbo hilo, mgombea wa CCM asingepata kura nyingi za kumshinda Dk. Slaa.

Wagombea sita wa ubunge katika jimbo hilo walitoka katika vyama vya CCM, CHADEMA, NCCR Mageuzi, CUF, SAU na TLP.

Alisema kuwa katika hati yao ya madai waliyoiwasilisha mahakamani hapo, hawakuiomba mahakama ichunguze ziliko kura hizo na wala hakuna wakala yeyote kati ya 253 wa CCM aliyejaza fomu maalumu ya kutaka matokeo ya kituo chake kurudiwa kuhesabiwa upya.

Aliiambia mahakama hiyo kuwa licha ya mawakala kupewa semina maalumu kuhusu haki za msimamizi na taratibu za mwenendo wa uchaguzi, walinyimwa fomu za kujaza malalamiko na ni yeye tu aliyeomba kura za kituo cha Kambi ya Simba kurudiwa kuhesabiwa.

Alipotakiwa kueleza kuwa sh milioni 8 ambazo ni fedha za gharama ya kuendeshea kesi hiyo alizipata wapi huku akiwa hana ajira kwa wakati huu, na pia hana vyanzo vya mapato na yeye alikuwa akiwategemea wazazi, alisema kuwa fedha hizo zilichangwa na marafiki na wazee.

Hata hivyo, hoja hiyo ilipingwa na wakili wake, Mpaya Kamara, kwa maelezo kuwa aihusiani na kesi ya msingi na hoja hiyo iliungwa mkono na jaji anayesikiliza kesi hiyo, Robert Makaramba.

Akihojiwa na wakili wa serikali, Mary Lyimo, shahidi aliiambia mahakama hiyo kuwa aliteuliwa kuwa shahidi baada ya makubaliano kati ya CCM na mgombea wake wa Ubunge, Patrick Tsere.

Aliiambia mahakama kuwa sababu ya yeye kuungana na wanachama wenzake kukata rufaa ni kutokana na kutokuridhika na matokeo yaliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi, ambaye alishindwa kutoa sauti wakati wa kutangaza matokeo na hata alipomtaka kurudia aligoma kutangaza tena.

Alisema kuwa kutokana na hali hiyo, hakusikia matokeo ya kura na idadi ya wapiga kura hakuijua.

Aidha, alipoonyeshwa fomu za matokeo, ambazo zimesainiwa na mawakala wote akiwamo wa CCM, shahidi huyo alikaa kimya kwa sababu awali alidai kuwa mawakala wa CCM hawakusaini fomu hizo.

Alipopewa fomu hizo na kuzisoma alikubali kuwa walisaini fomu hizo za matokeo.
 
Back
Top Bottom