Kesi ya akina Halima Mdee, itafanyiwa "delaying tactics" hadi ifike wakati wa uchaguzi mkuu mwaka 2025?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Nimeanza kuingiwa na wasiwasi, kutokana na sakata hili la akina Halima Mdee, kwa Kesi yao waliopeleka mahakamani na kinachoendelea, Mahakama inaweza kufanya "delaying tactics" Hadi shauri hilo lije kupata hukumu, itakuwa mwaka 2025, wakati wa uchaguzi mkuu mwingine unaokuja!

Kwa hiyo ninachokiona Mimi hivi sasa, Hawa akina Halima Mdee, wanachofanya kwa kushirikiana na Spika wa Bunge, Tulia Ackson, pamoja na mhimili wa Mahakama, ni kufanya "delaying tactics" Ili Kesi hiyo waicheleweshe Hadi ifike mwaka 2025, tutakapofanya uchaguzi mkuu.

Nayasema hayo nikiwa na ushahidi wa mazingira, kwa yanayotokea hivi sasa, nikifanya utabiri wangu huo.

Inajulikana wazi, hata na Jaji anayesikiliza Kesi hiyo, kuwa hao akina Halima Mdee, wameshapoteza sifa za kuendelea na ubunge wao, kwa mujibu wa ibara ya 71(1)(e) ambayo inasema hivi nanukuu "Mbunge atakoma kuwa Mbunge litokeapo moja ya mambo yafuatayo, ikiwa Mbunge huyo ataacha kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa" mwisho wa kunukuu.

Sasa nimuulize Spika Tulia Ackson, anaposema kuwa akina Halima Mdee, bado wataendelea kuwa wabunge, Hadi pale mchakato wa mhimili wa Mahakama utakapoamua shauri lao.
Hivi Katika kipindi hicho tunaposubiri uamuzi wa Mahakama, yeye Spika Tulia Ackson, atakuwa anawatambua wabunge hao kuwa wanatoka chama gani?

Kwa kuwa vikao vyote viwili vikubwa vya chama cha Chadema, kile cha Kamati Kuu, kilichokaa mwaka 2020 na hiki cha majuzi cha Baraza Kuu, vimethibitisha kuwa vimewavua uanachama wao hao wabunge 19 wa viti maalum kwa kosa la kukisaliti chama hicho.

Je wabunge hao wataendelea kukumbatiwa na Spika Tulia Ackson, wakiwa wabunge wa mhimili wa Mahakama??

Kwa kuwa hii siyo mara ya kwanza matukio ya kuvukiwa uanachama, yamewahi kutokea, huko siku za nyuma na Bunge hilo hilo limekuwa likitekeleza kwa mujibu wa Katiba ya nchi yetu, ambapo mara tu wanapopata taarifa ya kuvukiwa uanachama wao "automatically" pia Bunge linawaua ubunge wao.

Nitoe mifano michache, mwaka 2017, wabunge wa viti maalum wa CUF, chini ya Profesa Lipumba, alimpa taarifa Spika wa wakati huo Job Ndugai, kuwa weshafukuzwa na chama chao cha CUF, Spika Ndugai aliwafukuza ubunge wao papo kwa papo.

Licha ya wabunge hao kukimbilia mahakamani na Mahakama hiyo kutoa "court injunction" ya suala hilo, Hadi pale Mahakama hiyo itakapotoa uamuzi kwa Kesi hiyo ya msingi.

Wengi mnakumbuka kwa yaliyotokea wakati huo, ni kwa Spika Ndugai kuugomea mhimili wa Mahakama, akidai kuwa yeye Spika Ndugai, ndiye atakayeonekana kuwa anavunja Katiba ya nchi, kwa kuwa Katiba hiyo inatamka wazi kuwa kuwa Mbunge yeyote ni LAZIMA atokane na chama cha siasa!

Tukio la pili ni kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa kinamama wa CCM, Sofia Simba, ambaye naye alivuliwa uanachama wake na chama hicho cha CCM, Spika pia hakusita kumvua ubunge wake mara moja!

Swali ninalouliza, hivi kuna "double standards" Katika kutekeleza sheria hizi?

Iweje hivi sasa kwa hili suala la akina Halima Mdee, sheria zitafsiriwe tofauti??

Hivi ni nani yuko sahihi, je ni mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa CCM, Pius Msekwa, aliyetamka wazi kuwa Mbunge yeyote ambaye chama chake, kikimfukuza uanachama wake "automatically" anakuwa hana sifa za kuendelea kuwa Mbunge au ni huyu Spika Tulia Ackson, ambaye anadai kuwa ataheshimu uamuzi wa Mahakama?
 
CHADEMA imegoma kupeleka wabunge wapya kama hao wakitolewa .. Hivyo dhana ya bunge la vyama vingi haitafanya kazi na itakuwa ni pigo na aibu kwa serikali ya Tanzania kimataifa na kwa mabeberu wafadhili na zaidi kupelekea kunyimwa fungu la ruzuku na misaada
Hivyo basi afe kipa afe refa lazima uviko 19 wafike 2025
 
Upo sahihi mengine yote ni maigizo
Dalili za mvua ni mawingu...........

Katika hatua za awali tu, tumeona figisu figisu zinazofanywa na ofisi ya msajili wa Mahakama, kwa kupeleka summons kwa chama cha Chadema, siku hiyo hiyo inayoongelewa Kesi hiyo tarehe 15/5/2022 saa 6 mchana, wakati Kesi hiyo ikisikilizwa siku hiyo hiyo saa 8 mchana!🥺
 
CHADEMA imegoma kupeleka wabunge wapya kama hao wakitolewa .. Hivyo dhana ya bunge la vyama vingi haitafanya kazi na itakuwa ni pigo na aibu kwa serikali ya Tanzania kimataifa na kwa mabeberu wafadhili na zaidi kupelekea kunyimwa fungu la ruzuku na misaada
Hivyo basi afe kipa afe refa lazima uviko 19 wafike 2025
Aliyekataa siyo Freeman Mbowe ni.mh.Benson Kigaila

Chadema ina wenyewe.akima. Owenya, Kihwelu, Nkya nk....nk
 
CHADEMA imegoma kupeleka wabunge wapya kama hao wakitolewa .. Hivyo dhana ya bunge la vyama vingi haitafanya kazi na itakuwa ni pigo na aibu kwa serikali ya Tanzania kimataifa na kwa mabeberu wafadhili na zaidi kupelekea kunyimwa fungu la ruzuku na misaada
Hivyo basi afe kipa afe refa lazima uviko 19 wafike 2025
EU wanapiga jaramba na rungu kubwa mabegani....
 
Tanzania tuna mihimili mitatu(Bunge,mahakama,serikali).lakini miwili kati ya hiyo huwa inamtegemea mtu mmoja.kifupi serikali ndio imewabeba wenzake wawili.hivyo basi Bunge na Mahakama havina uwezo wa kufanya maamuzi yake kama chombo kinachojitegemea.hii yote ni kwa sababu jaji anateuliwa na spika vilevile ni kana anateuliwa tu.

Spika na jaji huwa hawana uwezo wa kufanya maamuzi wao kama wao hadi wamshirikishe serikali.kifupi maamuzi ya kisiasa mtu pekee wa kutoa ni Serikali(Raisi).

Hata hivyo hii inaonesha ni namna gani waafrika tunapenda madaraka.kwa sababu haiwezekani mbunge ameshavuliwa uanachama na hakuwa mbunge wa kuchaguliwa kwamba labda anawatumikia wananchi wa jimbo fulani lakini bado anang’ang’ania ubunge hadi anaenda mahakamani.

Mbunge wa viti maalumu anatumikia chama na chama hakimtaki lakini wao wanaendelea kupambania huo ubunge.halafu ikifika 2025 utakuta wanaenda ACT wazalendo na wanagombea tena huo ubunge..
 
Daliki za mvua ni mawingu, Katika hatua za awali tu, tumeona figisu figisu zinazofanywa na ofisi ya msajili wa Mahakama, kwa kupeleka summons kwa chama cha Chadema, siku hiyo hiyo inayoongelewa Kesi hiyo tarehe 15/5/2022 saa 6 mchana, wakati Kesi hiyo ikisikilizwa siku hiyo hiyo saa 8 mchana!🥺
Ni uhuni mkubwa sn
 
Nimeanza kuingiwa na wasiwasi, kutokana na sakata hili la akina Halima Mdee, kwa Kesi yao waliopeleka mahakamani na kinachoendelea, Mahakama inaweza kufanya "delaying tactics" Hadi shauri hilo lije kupata hukumu, itakuwa mwaka 2025, wakati wa uchaguzi mkuu mwingine unaokuja...
Wanaume tuna kazi aisee!! sasa huyo jamaa aliyemuoa Tulia anasema ana mke au kavulana fulani kenye sura mbaya kama tumbili. Kuna wanawake wengine ukioa bahati mbaya kutwa kucha lazima ushinde klabu ukiwinda michepuko iliyotakata ili ukirudi nyumbani uendeleze mbinu ya kumfunika kichwa ili asikuone ulivyo na kinyaa wakati wa kumnyandua.

Au upate uwe umeangalia picha za wanawake wazuri ili angalau uvute hisia! kha wanaume kuna siri kuu ya kuwa na umri mfupi! Kuangukia kwa akina tulia sharti ufe mapema!!
 
Wanaume tuna kazi aisee!! sasa huyo jamaa aliyemuoa Tulia anasema ana mke au kavulana fulani kenye sura mbaya kama tumbili. Kuna wanawake wengine ukioa bahati mbaya kutwa kucha lazima ushinde klabu ukiwinda michepuko iliyotakata ili ukirudi nyumbani uendeleze mbinu ya kumfunika kichwa ili asikuone ulivyo na kinyaa wakati wa kumnyandua. Au upate uwe umeangalia picha za wanawake wazuri ili angalau uvute hisia! kha wanaume kuna siri kuu ya kuwa na umri mfupi! Kuangukia kwa akina tulia sharti ufe mapema!!
Hahaaaaa........😄😅
 
Back
Top Bottom