Troll JF
JF-Expert Member
- Feb 6, 2015
- 7,804
- 12,224
Dar es Salaam. Wakati aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu akidai yupo ubalozi wa Ujerumani, ameomba kupatiwa hifadhi ya kisasa kwa maelezo ya kuwa ametishiwa maisha.
Kauli hiyo imekuja wakati Mahakama ya Hakimu ya Hakimu Mkazi, ikitoa hati ya wito kumtaka Lissu afike mahakamani Novemba 30, Desemba 3, 10 na Desemba 17, kusikiliza kesi zake tano zinazomkabili.
Hii ni mara ya nne, kwa Lissu kushindwa kufika mahakamani kuhudhuria kesi hiyo, tangu aliporejea nchini Julai 29, 2020, akitokea Ubelgiji alipokuwa anapatiwa matibabu baada ya kupigwa risasi na watu ambao hadi sasa hawajafahamika.
Hadi sasa, Lissu anakabiliwa na kesi tano za jinai, zote zikiwa na mashtaka ya uchochezi na zipo kwa mahakimu tofauti.
Kesi hizo ni ya jinai namba 208/2016; 233/2016; 279/2016; 236/2017 na 123/17 zote zikiwa katika hatua ya kutajwa, kusomewa hoja za awali( PH) na usikilizwaji.
Kauli hiyo imekuja wakati Mahakama ya Hakimu ya Hakimu Mkazi, ikitoa hati ya wito kumtaka Lissu afike mahakamani Novemba 30, Desemba 3, 10 na Desemba 17, kusikiliza kesi zake tano zinazomkabili.
Hii ni mara ya nne, kwa Lissu kushindwa kufika mahakamani kuhudhuria kesi hiyo, tangu aliporejea nchini Julai 29, 2020, akitokea Ubelgiji alipokuwa anapatiwa matibabu baada ya kupigwa risasi na watu ambao hadi sasa hawajafahamika.
Hadi sasa, Lissu anakabiliwa na kesi tano za jinai, zote zikiwa na mashtaka ya uchochezi na zipo kwa mahakimu tofauti.
Kesi hizo ni ya jinai namba 208/2016; 233/2016; 279/2016; 236/2017 na 123/17 zote zikiwa katika hatua ya kutajwa, kusomewa hoja za awali( PH) na usikilizwaji.