Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,801
- 11,961
Kesi ya Jinai namba 458 ya mwaka 2016 ya Jamhuri dhidi ya Maxence Melo na mwenzake Micke William kuhusu kuendesha mtandao nchini bila kutumia Kikoa cha do.TZ na Kuzuia Upelelezi wa Polisi imeshindwa kuendelea na ushahidi leo Agosti 26, 2019 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu baada ya shahidi wa upande wa Jamhuri kutofika Mahakamani kwa mara ya 3 sasa
Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Daisy Makakala akiambatana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Saimon huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala mbele ya Hakimu Huruma Shahidi
Wakili wa Jamhuri ameiambia Mahakama kuwa shauri hilo lilikuwa mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikilizwa lakini kutokana na kukosekana kwa shahidi ambaye ni Tully Esther Mwambapa kutoka CRDB aliomba tarehe nyingine ambapo ameihakikishia Mahakama watakuja na jibu kuhusu shahidi huyo na mwendelezo kuhusu shauri
Hakimu Huruma Shahidi ameutaka upande wa mashtaka kuleta mashahidi Mahakamani hapo ili kesi hiyo iweze kumalizika kwa kuwa imeshachukua muda mrefu sana na ameahirishwa tena kesi hiyo hadi Oktoba 01, 2019 itakapoendelea na ushahidi.
Katika shauri hilo lililofunguliwa Desemba 2016 na kuanza kusikilizwa Februari 2017, tayari mashahidi zaidi ya Watatu kutoka upande wa Jamhuri wameshasikilizwa na shahidi wa mwisho kusikilizwa ilikuwa mnamo Novemba 07, 2018. Baada ya hapo shauri limekuwa likiahirishwa huku sababu kadhaa zikitolewa na kubwa ikiwa ni kukosekana kwa shahidi.
Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Daisy Makakala akiambatana na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Saimon huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala mbele ya Hakimu Huruma Shahidi
Wakili wa Jamhuri ameiambia Mahakama kuwa shauri hilo lilikuwa mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikilizwa lakini kutokana na kukosekana kwa shahidi ambaye ni Tully Esther Mwambapa kutoka CRDB aliomba tarehe nyingine ambapo ameihakikishia Mahakama watakuja na jibu kuhusu shahidi huyo na mwendelezo kuhusu shauri
Hakimu Huruma Shahidi ameutaka upande wa mashtaka kuleta mashahidi Mahakamani hapo ili kesi hiyo iweze kumalizika kwa kuwa imeshachukua muda mrefu sana na ameahirishwa tena kesi hiyo hadi Oktoba 01, 2019 itakapoendelea na ushahidi.
Katika shauri hilo lililofunguliwa Desemba 2016 na kuanza kusikilizwa Februari 2017, tayari mashahidi zaidi ya Watatu kutoka upande wa Jamhuri wameshasikilizwa na shahidi wa mwisho kusikilizwa ilikuwa mnamo Novemba 07, 2018. Baada ya hapo shauri limekuwa likiahirishwa huku sababu kadhaa zikitolewa na kubwa ikiwa ni kukosekana kwa shahidi.