Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,805
- 11,964
Kesi namba 456 (Jamhuri v Maxence Melo na mwenzake Micke William) ambapo Kampuni ya Oilcom iliandikwa katika mtandao wa JamiiForums ikidaiwa kukwepa kodi na kuchakachua mafuta bandarini Dar imeahirishwa tena leo Februari 19, 2020 hadi Aprili 02, 2020.
Hukumu hii awali ilipangwa kusikilizwa Novemba 26, 2019 ikapangwa tena kutolewa Disemba 06, 2019 na baadae ikapangwa kutolewa Januari 22, 2020 na ikapangwa kuwa lazima leo Februari 19, 2020 hukumu ingetolewa saa 6 mchana.
Kesi hiyo leo imesikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar chini ya Hakimu Huruma Shaidi kwa niaba ya Hakimu Mwandamizi Thomas Simba anayeendesha kesi hiyo.
Katika kesi hiyo, Washtakiwa wanatuhumiwa kutotoa ushirikiano kwa Jeshi Polisi walipotakiwa kutoa taarifa za aliyeandika kuhusu Oilcom.
Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Faraji Nguka huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala na Wakili Benedict Alex
Hakimu Simba alitakiwa kutoa hukumu ya Kesi hiyo leo baada ya Upande wa Utetezi kumaliza kujitetea, lakini uamuzi wa hukumu katika kesi hiyo umeshindikana kutolewa kutokana na kwamba Hakimu hajamaliza kuandika hukumu hiyo
Wakili Nguka amesema, “Shauri hili lilikuja mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikiliza hukumu lakini hukumu haijakamilika kwa hivyo tunaomba siku nyingine kwa ajili ya kesi kuja kutolewa uamuzi”
Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 19, 2020 kwa ajili ya kutajwa tena huku akisema siku ya hukumu itakuwa Aprili 02, 2020
****
Kujua ilipotokea kesi hii, tembelea Kesi Na. 456 (Jamhuri v JamiiForums): Hukumu yaahirishwa hadi Februari 19, 2020 saa sita mchana
Kujua kinachoendelea kwenye kesi zote za JamiiForums, tembelea Muendelezo wa Kinachojiri Kisutu: Kesi za Jamhuri dhidi ya JamiiForums
ORIGINAL CHARGE SHEET
AMENDED CHARGE SHEET
Charge-sheet mpya ilibadilishwa Novemba 2017 > Kesi dhidi ya JF: Mahakama ya Kisutu yabariki Jamhuri kubadilisha hati ya mashtaka! Ni kesi ile ya Oilcom - JamiiForums
Hukumu hii awali ilipangwa kusikilizwa Novemba 26, 2019 ikapangwa tena kutolewa Disemba 06, 2019 na baadae ikapangwa kutolewa Januari 22, 2020 na ikapangwa kuwa lazima leo Februari 19, 2020 hukumu ingetolewa saa 6 mchana.
Kesi hiyo leo imesikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar chini ya Hakimu Huruma Shaidi kwa niaba ya Hakimu Mwandamizi Thomas Simba anayeendesha kesi hiyo.
Katika kesi hiyo, Washtakiwa wanatuhumiwa kutotoa ushirikiano kwa Jeshi Polisi walipotakiwa kutoa taarifa za aliyeandika kuhusu Oilcom.
Upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Faraji Nguka huku upande wa Utetezi ukiwakilishwa na Wakili Peter Kibatala na Wakili Benedict Alex
Hakimu Simba alitakiwa kutoa hukumu ya Kesi hiyo leo baada ya Upande wa Utetezi kumaliza kujitetea, lakini uamuzi wa hukumu katika kesi hiyo umeshindikana kutolewa kutokana na kwamba Hakimu hajamaliza kuandika hukumu hiyo
Wakili Nguka amesema, “Shauri hili lilikuja mbele ya Mahakama kwa ajili ya kusikiliza hukumu lakini hukumu haijakamilika kwa hivyo tunaomba siku nyingine kwa ajili ya kesi kuja kutolewa uamuzi”
Hakimu Shaidi ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 19, 2020 kwa ajili ya kutajwa tena huku akisema siku ya hukumu itakuwa Aprili 02, 2020
****
Kujua ilipotokea kesi hii, tembelea Kesi Na. 456 (Jamhuri v JamiiForums): Hukumu yaahirishwa hadi Februari 19, 2020 saa sita mchana
Kujua kinachoendelea kwenye kesi zote za JamiiForums, tembelea Muendelezo wa Kinachojiri Kisutu: Kesi za Jamhuri dhidi ya JamiiForums
ORIGINAL CHARGE SHEET
AMENDED CHARGE SHEET
Charge-sheet mpya ilibadilishwa Novemba 2017 > Kesi dhidi ya JF: Mahakama ya Kisutu yabariki Jamhuri kubadilisha hati ya mashtaka! Ni kesi ile ya Oilcom - JamiiForums