Kesi dhidi ya Mbowe: Ushahidi wa Luteni Denis Urio ni muhimu sana

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,384
26,733
Ndugu zangu!

Kwa wale tunaofuatilia kwa ukaribu hii kesi pendwa, tutakumbuka maelezo muhimu kutoka kwa mashahidi wa pande zote mbili.

Kwenye kesi ya msingi, tulisikia ushahidi wa ACP Kingai akimtaja Luteni Denis Urio kuwa alitumika kama mtego kwa sharti la kuripoti kila hatua.

Kwa maelezo yake, Urio alihusika 'kumtafutia' Mbowe wasaidizi aliowahitaji. Ikawa hivyo.

Hapa tulitegemea kuwa Urio 'amemchoma' kwa kuripoti mipango yake inayoitwa ya ugaidi.

Lakini kwenye ushahidi wa kesi ndogo uliotolewa na Komandoo Ling’wenya (mtuhumiwa), yeye kamtaja Urio kuwepo kwenye moja ya mahabusu za hao wanaoitwa magaidi na amemshuhudia akipitia mateso kama hao wengine.

Hii inatupa mwelekeo gani? Kwanini mtu aliyetajwa kufanikisha ukamatwaji wa magaidi naye anakula kichapo?

Urio yupo upande gani?

Japo si mmoja wa mashahidi katika hii kesi ya msingi, lakini sasa ni rasmi ameingizwa na itabidi apande kizimbani.

Ushahidi wake unaweza kutusogeza hatua nyingi kuelekea kuufahamu ukweli, tunamhitaji Luteni Denis Urio kizimbani bila kukosa.

Ncha Kali.
 
Hii kesi ikiendelea ni aibu kwa serikali na ikifutwa na DPP ni aibu kwa serikali. Aibu haikwepeki kwa serikali kwa njia yoyote ile, yani kunyoa au kusuka hawapendezi.

Pili, swala la Police kuwateka na kuwatesa Makomandoo wa JWTZ, ambao wana Mahakama, Mahabusu na Police wao (Military Police MP, Martial Courts, Martial Lock Ups) zao pindi wanapotenda kosa. Police walipata baraka kutoka wapi??? Kwa CDF Mabeyo au IGP Sirro au Rais???.

NOTE THAT: Luteni Denis Urio ni bado mkufunzi jeshini, yupo active kama mwanajeshi wa JWTZ na hajasimamishwa kazi bado, na ndio police waliosema wameshamtupa baada ya kumalizana nae kumtekenya TAZARA POLICE STATION.

Tatu, swala la usalama wa washtakiwa na mashahidi kwa hatua ya hii kesi ilipofikia, hatua gani zimechukuliwa kuwa hakikishia wana usalama huko mahabusu walipo hifadhiwa na pindi wanapo safirishwa kwenda mahakamani?

Tumeona wakisafirishwa kwa gari bovu lililogoma kuwaka mahakamani, je ikitokea msafara wao nje ya mahakama au barabarani kuvamiwa na watu wasiojulikana na kumiminiwa mzigo wa risasi ili kuficha aibu, hilo jambo litachukua taswira gani mbele ya dunia?

Swali la kizushi;

CDF wetu angekua ndio yule mwamba wa Guinea, bwana Kanali Mamady Doumbouya angekubaliana na mwenendo huu wa kuvunja katiba, kulinajisi jeshi la nchi kwa kuwateka Makomandoo na kuwafanya waliofanywa (Kupigwa, Kuteswa na Kuchomwa bisibisi za makalioni)?
 
Mtiririko wa kesi hii umeleta hamasa sana, kuifuatilia, kumbe mambo ya mahakamani yanapokuwa wazi hivi, sio tu kuonyesha haki imepatikana bali imepatikanaje!

Kwani hata ambaye hajui sheria kwa mahojiano yalivyokuwa baina ya upande wa mashitaka na upelelezi, anaweza kupata picha nini kinawezatokea! Hapa kwetu imefungua ukurasa mpya, kwani sheria , vizingiti kibao vilikuwa, mbona nchi nyingi tu siku hizi mambo ya mahakamani (mwenendo wa kesi )hata una kuwa live?

Hata ile ya sabaya, unaona kabisaa mmm!!akichomoka basi ni ki miujiza tu!!!
 
Mtiririko wa kesi hii umeleta hamasa sana, kuifuatilia, kumbe mambo ya mahakamani yanapokuwa wazi hivi, sio tu kuonyesha haki imepatikana bali imepatikanaje....
Sisi wengine tulitoa wito na hamasa kabla hata kesi hii haijaanza, irushwe LIVE COVERAGE kwenye channel maalum, ili wananchi wote wajionee. Kama ilivotokea katika baadhi ya kesi nchini Kenya na South Africa.

Ila mkanyuti wana kijiji cha JF. Mngejionea mauzauza ya ujinga wa Jamhuri kama ingerushwa live.

 
Hii kesi ikiendelea ni aibu kwa serikali na ikifutwa na DPP ni aibu kwa serikali. Aibu haikwepeki kwa serikali kwa njia yoyote ile, yani kunyoa au kusuka hawapendezi.

Pili, swala la Police kuwateka na kuwatesa Makomandoo wa JWTZ, ambao wana Mahakama, Mahabusu na Police wao (Military Police MP, Martial
Wangekuwa wanajeshi sheria na miongozo ya watumishi wa umma hussusani jeshi ingewalinda lakini walikuwa wameshafukuzwa kwa hiyo wameteswa kama wahalifu wengine raia, Ki ukweli hairuhusiwi kabisa kumtesa mtuhumiwa kwa sababu bado hajathibitika ni mhalifu na hata ikithibitika hukumu ya mahakama ndoo adhabu ,

Ki uhalisia kwa Africa yote wanaanza kumtesa mtuhumiwa ili kama anaweza kutoa taarifa za kuwaongoza polisi kupata taarifa nyingi na ushahidi kwa sababu hatuna technolojia na resource hela ya kufanya upelelezi kwa muda mrefu na kupitia chanel nyingi , kwa hiyo shotcut mtese afunguke chap chap
 
Possibly kabisa Urio pia aliteswa na akalazimishwa kusimama upande wa polisi. Kubwa zaidi Urio aitwe naye atoe ushahidi, hapa kuna watu wataaibika. Atoe ushahidi kisha awekwe sehemu salama

..Urio ataletwa na upande wa mashtaka wakati kesi ya msingi itakapoanza kusikilizwa.

..Ni shahidi muhimu sana wa upande wa mashtaka kwasababu yeye ndiye anayedaiwa kutoa tip kwa polisi kuhusu kuwepo kwa njama za ugaidi.
 
Ushahidi wake unaweza kutusogeza hatua nyingi kuelekea kuufahamu ukweli, tunamhitaji Luteni Denis Urio kizimbani bila kukosa.
Akiwa upande upi, mashtaka au utetezi?

Mashahidi kadhaa wa upande wa utetezi taarifa zao zimewekwa kapuni. Anaweza kuwa ni mmoja wa hao?

Kesi hii tokea mwanzo ilionekana kutokuwa na uzito, haya yatakayoendelea ni kulazimisha tu kisichowezekana kiwezekane.
Lakini inabidi niuelezee huu mstari wa "kisichowezekana kiwezekane" Wakati kesi hii inatengenezwa hapakuwepo na "kisichowezekana."
Nyakati zimebadilika haraka sana!
 
Hii kesi ikiendelea ni aibu kwa serikali na ikifutwa na DPP ni aibu kwa serikali. Aibu haikwepeki kwa serikali kwa njia yoyote ile, yani kunyoa au kusuka hawapendezi.

Pili, swala la Police kuwateka na kuwatesa Makomandoo wa JWTZ, ambao wana Mahakama, Mahabusu na Police wao (Military Police MP, Martial Courts, Martial Lock Ups) zao pindi wanapotenda kosa. Police walipata baraka kutoka wapi??? Kwa CDF Mabeyo au IGP Sirro au Rais???

Tatu, swala la usalama wa washtakiwa na mashahidi kwa hatua ya hii kesi ilipofikia, hatua gani zimechukuliwa kuwa hakikishia wana usalama huko mahabusu walipo hifadhiwa na pindi wanapo safirishwa kwenda mahakamani??? Tumeona wakisafirishwa kwa gari bovu lililogoma kuwaka mahakamani, je ikitokea msafara wao nje ya mahakama au barabarani kuvamiwa na watu wasiojulikana na kumiminiwa mzigo wa risasi ili kuficha aibu, hilo jambo litachukua taswira gani mbele ya dunia???

Swali la kizushi;

CDF wetu angekua ndio yule mwamba wa Guinea, bwana Kanali Mamady Doumbouya angekubaliana na mwenendo huu wa kulinajisi jeshi la nchi kwa kuwateka Makomandoo na kuwafanya waliofanywa (Kupigwa, Kuteswa na Kuchomwa bisibisi za makalioni)???
Acha upotoshaji wa makusudi, hao watu walishatimuliwa jeshini hivyo ni raia wa kawaida tu na wanakuwa treated kama raia, ndiyo maana waliweza hata kuomba kazi ya ulinzi kwa bwana Mwamba.
 
Ndugu zangu!

Kwa wale tunaofuatilia kwa ukaribu hii kesi pendwa, tutakumbuka maelezo muhimu kutoka kwa mashahidi wa pande zote mbili.

Kwenye kesi ya msingi, tulisikia ushahidi wa ACP Kingai akimtaja Luteni Denis Urio kuwa alitumika kama mtego kwa sharti la kuripoti kila hatua.

Kwa maelezo yake, Urio alihusika 'kumtafutia' Mbowe wasaidizi aliowahitaji. Ikawa hivyo.

Hapa tulitegemea kuwa Urio 'amemchoma' kwa kuripoti mipango yake inayoitwa ya ugaidi.

Lakini kwenye ushahidi wa kesi ndogo uliotolewa na Komandoo Ling’wenya (mtuhumiwa), yeye kamtaja Urio kuwepo kwenye moja ya mahabusu za hao wanaoitwa magaidi na amemshuhudia akipitia mateso kama hao wengine.

Hii inatupa mwelekeo gani? Kwanini mtu aliyetajwa kufanikisha ukamatwaji wa magaidi naye anakula kichapo?

Urio yupo upande gani?

Japo si mmoja wa mashahidi katika hii kesi ya msingi, lakini sasa ni rasmi ameingizwa na itabidi apande kizimbani.

Ushahidi wake unaweza kutusogeza hatua nyingi kuelekea kuufahamu ukweli, tunamhitaji Luteni Denis Urio kizimbani bila kukosa.


Ncha Kali.
Huyu ni muhimu sana kupanda kizimbani ili aseme na kuhojiwa kuhusiana na sakata zima.
 
Huyu dogo mpuuzi alitaka kupabda haraka vyeo kubumbulua deal ugaidi mjinga....ametumika kama toulet paper sasa kasaliti watu wenye lengo ulinzi Mbowe yeye alitaka kick hakuna kesi hapo attentipn nchi imehama sababu tip kijinga ndio maana nae kala kichapo ili kujirodhasha mjinga huyu Urio
 
Back
Top Bottom