Kesi dhidi ya kupinga ubunge wa Mwambe yatupiliwa mbali kwa mara ya pili

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
Shauri la Kikatiba Na.12 la mwaka 2020 lililofunguliwa na Asasi ya Civic and Legal Aid Organization dhidi ya Mhe. Spika, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Cecil Mwambe ili kupinga ubunge wa Mwmbe imetupiliwa mbali Leo tarehe 15 Juni,2020 na Mahakama Kuu.

Hii ni mara ya pili ambapo Mahakama Kuu inaiondoa kesi hiyo Mahakamani kwa kukosa msingi.

Akitoa uamuzi wake kwenye hoja za Pingamizi dhidi ya shauri hilo zilizowasilishwa na upande wa Serikali, Mhe Jaji Stephen Magoiga amesema kuwa, hakuona hoja za msingi za Mahakama kuendelea kusikiliza kesi hiyo ambayo maudhui yake yanafanana na Shauri la Kikatiba Na. 10 la 2020 lililofunguliwa awali Mahakamani hapo na Wakili Paul Revocatus Kaunda kuhusu Mbunge huyo huyo.

Katika shauri hilo la awali, Mahakama ilitupilia mbali kesi kwa kuwa ilionekana haina msingi na ililenga
katika kuleta usumbufu na kuvuruga taratibu za kimahakama.

Kwa uamuzi huo, Mhe. Cecil Mwambe bado ni Mbunge wa Jimbo la Ndanda.

Kwenye shauri hilo la Kikatiba Na. upande wa Civic and Legal Aid Organization uliwakilishwa na Wakili wa kujitegemea John Seka na Mwambe aliwakilishwa Bw. Dismas Raphael wakati Serikali iliwakilishwa Mahakamani na Wakili wa Serikali Mkuu, Bw. George Mandepo na Erigh Rumisha.
 
Hiyo kesi ilikuwa yakijinga. Hivyo hukumu hiyo itasaidia wabunge kuwa huru , hukumu hiyo itawalinda wanapotaka kufukuzwa na vyama vyao.

Maana watu wanachangishwa ovyo ovyo, wanadharirishwa kingono na kushindwa kulalamika ktk vyombo vya dola kwahofu yakufukuzwa ubunge, hii safi sana , hongera serimari, hongera bunge.
 
Kuna Sehemu katika pekua pekua zangu wameandika katika Histria ya Nchi yetu, Mabunge yenye nguvu yalikuwa Bunge la 9 na la 10, i.e la Mzee Sitta na Mama Makinda wakimaanisha Mabunge yaliyokuwa wakati wa Jk lakin hapo haoo tunaambiwa tangu Uhuru Serikal dhaifu zaid ni ya awamu ya 4

Ninachojiuliza kwanini Bunge Imara huzaa Serikal dhaifu na kinyume chake?
 
Hivi huyu Magoiga sio yule mwanaharakati wa ccm kweli anajiitaga magoiga sn
Nadhani, simjui...it might be!
jamiiforums.com/threads/vexatious-frivolous-scandalous-trivial-case-against-ndugai-and-mwambe.1744628/
 
Shauri la Kikatiba Na.12 la mwaka 2020 lililofunguliwa na Asasi ya Civic and Legal Aid Organization dhidi ya Mhe. Spika, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Cecil Mwambe ili kupinga ubunge wa Mwmbe imetupiliwa mbali Leo tarehe 15 Juni,2020 na Mahakama Kuu.

Hii ni mara ya pili ambapo Mahakama Kuu inaiondoa kesi hiyo Mahakamani kwa kukosa msingi.

Akitoa uamuzi wake kwenye hoja za Pingamizi dhidi ya shauri hilo zilizowasilishwa na upande wa Serikali, Mhe Jaji Stephen Magoiga amesema kuwa, hakuona hoja za msingi za Mahakama kuendelea kusikiliza kesi hiyo ambayo maudhui yake yanafanana na Shauri la Kikatiba Na. 10 la 2020 lililofunguliwa awali Mahakamani hapo na Wakili Paul Revocatus Kaunda kuhusu Mbunge huyo huyo.

Katika shauri hilo la awali, Mahakama ilitupilia mbali kesi kwa kuwa ilionekana haina msingi na ililenga
katika kuleta usumbufu na kuvuruga taratibu za kimahakama.

Kwa uamuzi huo, Mhe. Cecil Mwambe bado ni Mbunge wa Jimbo la Ndanda.

Kwenye shauri hilo la Kikatiba Na. upande wa Civic and Legal Aid Organization uliwakilishwa na Wakili wa kujitegemea John Seka na Mwambe aliwakilishwa Bw. Dismas Raphael wakati Serikali iliwakilishwa Mahakamani na Wakili wa Serikali Mkuu, Bw. George Mandepo na Erigh Rumisha.
Hivi hakuna nafasi ya rufaa Court of appeal kuilazimisha Mahakama Kuu iisikilize?
 
Kuna Sehemu katika pekua pekua zangu wameandika katika Histria ya Nchi yetu, Mabunge yenye nguvu yalikuwa Bunge la 9 na la 10, i.e la Mzee Sitta na Mama Makinda wakimaanisha Mabunge yaliyokuwa wakati wa Jk lakin hapo haoo tunaambiwa tangu Uhuru Serikal dhaifu zaid ni ya awamu ya 4

Ninachojiuliza kwanini Bunge Imara huzaa Serikal dhaifu na kinyume chake?
Muundo wa kiuongozi unataka serikali, bunge na mahakama visimamiane, sio kimoja kuvisimamia vingine. Sasa serikali ikiwa dhaifu, bunge na mahakama hazina budi kuonesha njia ili mambo yasiende kombo.

Sent from my LM-Q710(FGN) using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom