Kesi dhidi ya JamiiForums zaelekea hatua mpya: Asanteni watanzania, asante wana JF!

Endelea kutulinda mkuu mana ukiviolate sheria za kutunza siri za wateja wako (sisi) utatutisha kuibua mapya kwa mustakabali wa taifa.
Wala sina shaka na wewe nikuamini kamanda .
Best wishes tuko pamoja.
 
Maxence, binafsi nimemuunga mkono JPM kuanzia kampeni hadi juhudi zake mbalimbali. Lakini hili la uhuru wa vyombo vya habari na hasa hizi kesi za JF ni moja ya doa kubwa na issue iliyoturudisha chini wengine.

Msingi wa hizi kesi hauna faida kwa Taifa zaidi ya kuwakatisha tamaa watoa taarifa.

Bila Jamii Forums sehemu kubwa ya ufisadi unaopigwa vita leo isingekuwa na nguvu iliyo nayo leo. JPM anayo fursa kubwa ya kuwa Rais wa kihistoria akibadili vitu vinavyomchafua kama uhuru wa kutoa maoni au taarifa bila kubughudhiwa kama umetumia lugha ya staha na umesema ukweli.

Lazima tujenge taifa la wasema ukweli bila uoga na kila anayesema uongo au kutoa hoja kwa lugha zisizo za staha achukuliwe hatua kali.

Kila lakheri Cde Maxence Melo ....Tunafatilia kwa karibu kila nukta ....
Mbona umeandika kiuwogauwoga? Kuna haja gani ya kumstahi mtu asiyejistahi?

Kama dot com nalo ni kosa siku hizi na wamkammate na huyu www.millardayo.com.

Pumbavu kabisa.
 
Tuombe Mungu awe upande wetu ....Maxence anasimamia kwa niaba yetu tu ....ndio maana inapocheza Taifa Stars tunasema Mungu awe upande wetu ili wachezaji wajue wao ni wawakilishi wetu ila tupo pamoja nao ....ingemgharimu nini Maxence kutoa address ya huyo infomer ( na tusijue) ....mamlaka zijue Maxence anasimama kwa niaba yetu watumiaji na wasio watumiaji wa JF .....

kwa hiyo sasa uko upande wa JF dhidi ya upande wa serikali ya magufuli?! unapinga juhudi za rais eti!
 
Tuko pamoja Mkurugenzi kwa sasa Jamii forum pekee ndio chombo ambacho watu wako huru kuzungumza maoni yao bila kuvunja sheria za nchi.

Nawatakia kila la kheri katika mchakato wa kesi hizo na InshaAllah Mwenyezi Mungu atakuwa Upande wa Haki.
Nawaza bila forum hii nyongo zetu sijuwi wapi tungezitoa
 
View attachment 644127

Ndugu, jamaa na marafiki...

Nachukua fursa hii kukushukuruni kwa support ambayo mmetupa tangu kuanza kwa kesi 3 zinazoendelea mahakamani Kisutu tangu Disemba 19, 2016 hadi leo.

Kuanzia kesho, Disemba 05 hadi Disemba 07 (siku 3 mfululizo) kesi mbili zimewekwa kwenye ‘session’ ili zifike tamati. Mwisho wowote wa kesi hizi bado utakuwa ndio mwisho wenyewe, uwe mbaya au mzuri kwa upande wetu.

Na mnamo Disemba 18-20 (siku 3 mfululizo) kesi ya 3 itaunguruma katika Mahakama ya Kisutu.

Tangu nakamatwa mnamo Disemba 13, 2016 hadi leo, nimepata salaam nyingi za kunitakia kila la heri pamoja na timu yangu na wengine ambao hata hawakunijua physically walijikuta wakisimama nami katika kutetea uhuru wetu wa kujieleza na faragha ya watoa taarifa wenye nia njema!

Kesi tatu zenyewe ni hizi:
1) Kampuni ya Oilcom ilidaiwa kukwepa kodi bandarini, Jeshi la Polisi linataka taarifa za aliyeanzisha mjadala huo; sisi tunaamini chanzo cha taarifa hii kilitakiwa kulindwa na si kukamatwa bali Polisi wangefanya uchunguzi.
2) Kampuni ya CUSNA Investment ilidaiwa kufoji nyaraka bandarini na kuwatesa wafanyakazi wazalendo na kupendelea wageni toka nje ya nchi; Polisi walitaka kumkamata mwanzisha mada lakini sisi tunaamini chanzo hiki cha taarifa kilikuwa na nia njema, tulitarajia iwepo Hati ya Mahakama inayoridhia kukamatwa kwa mhusika na kuelezwa kosa lake.
3) Kuwa na Tovuti ambayo ni .COM. Hapa sitii neno...

Yeyote aliyetuunga mkono (kwa namna yoyote) hata bila kujua tunapigania nini nasema ASANTE. Karibuni tujumuike pamoja Kisutu tarehe hizi hadi hatma ya kesi hizi.

Asanteni sana watanzania!
Mi nataka nije kupiga selfie na wewe mkuu
 
112 Reactions
Reply
Back
Top Bottom