Kesho ya Kikwete ni chungu kuliko leo ya Mkapa

Mkapa alifanya uozo, Jk akaja kuongezea uozo.
Yaani ni kama msingi wa nyumba tuu.
Mkapa alijenga msingi usioimara, Jk akaja kujenga juu ya msingi ulele ila alichoharibu akajenga jumba bovu kuliko hata ule msingi.
 
Ivi mamo yote haya yanayotokea unaweza kuta mwenzenu yuko poa tuu ila ninyi ndo mwaumiza vichwa
 
Kila awamu ina mapungufu yake ni makosa kudhani kuna awamu ya utawala haikuwa na mapungufu. Awamu ya nne inaweza kuwa na mapungufu lakini kusema anabomoa kazi za Mkapa ni lugha kali ambayo inaonyesha kwamba kikwete hajafanya lolote pengine kwamba hata chuo kikuu cha Dodoma anabomoa kazi ya Mkapa
 
Mkapa big up!!!!!!!!!!nakumbuka mshahara wa serikali ulikuwa unatoka tarehe 23 ya kila mwezi sasa imefika kati ya tarehe 31 hadi 4 ya mwezi mwingine
 
Ndg wanaJF,
Kwenye mojawapo ya threads zangu, niligusia suala hili kama utani tu kwamba wakati Mkapa anaingia madarakani nchi ilikuwa katika hali mbaya sana kiuchumi. Mapato ya serikali yalikuwa madogo mno ikilinganishwa na mahitaji. Migomo ya wanafunzi ilikuwa haiishi kudai siyo nyongeza ya posho bali kulipwa posho. Wafanyakazi serikalini walikuwa wanacheleweshewa sana mishahara. Ilifika hatua kesi mahakamani zilikuwa zinaandikwa kwenye makaratasi ya kaki na wakati mwingine hata kwenye vipande vya box. Fedha ilikuwa mikononi mwa wafanyabiashara wachache tena biashara za kihuni zisizo na tija kwa uchumi wa nchi yetu. Kwa ujumla, hali ilikuwa mbaya na Serikali ilikuwa haikopesheki tena.

Alipoingia Mzee Mkapa, mambo yalianza kubadilika. Japo wananchi tayari walianza kuona mabadiliko chanya, lakini miaka mitano ya mwanzo ya uongozi wa Mzee Mkapa ilitumika katika kujenga uchumi na kuongeza mapato ya Serikali. Ndani ya miaka mitano ya mwanzo, heshima ya Serikali mbele ya wananchi na jamii ya kimataifa ilianza kuongezeka. Shughuli za uzalishaji na uwekezaji zilianza kushamiri. Mbinu za kukusanya kodi zilibuniwa na kuimarishwa. Nchi ilianza kukopesheka. Uchumi ulianza kuimarika. Kwa mara ya kwanza ndani ya miaka kumi, wafanyakazi Serikalini hususan waalimu walianza kulipwa mishahara kabla hata ya tarehe 30, mwishoni mwa mwezi. Ofisi za Serikali zilianza kupendeza na kupata heshima yake. Miundombinu mingi ilianza kujengwa ikiwa ni pamoja na barabara, simu, miradi mikubwa ya maji, na mambo mengi kadha wa kadha. Ebu tujikumbushe barabara za ndani Jijini Dar zilikuwaje kabla Mkapa, barabara ya Ubungo - Mlandizi, barabara ya Chalinze - Segera, Dodoma - Mwanza, Dar - Mtwara, Daraja la Mkapa, Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria, Uwanja wa Mkapa, Uwanja wa Ndege Songwe Mbeya, Uwanja wa Mpira wa Taifa, Jengo la Bunge, Mradi wa Maji wa Wami Chalinze, n.k, n.k. Leo hii mabasi yanasafiri kutoka Dar na kufika siku hiyo hiyo Mwz kupitia Dodoma, Singida na Shinyanga na siyo kupitia Arusha, Nairobi, Kisumu na Mara. Nikikumbuka yote haya na mengine mengi, siyo siri, najisikia machozi yanaanza kutiririka.

Pamoja na mapungufu aliyofanya Mzee Mkapa mwishoni mwa utawala wake, kama vyombo vya habari vilivyotuhabarisha, kwangu mimi Mzee huyu atabaki kuwa shujaa na kadri siku zinavyokwenda, ndivyo ninavyomwona shujaa zaidi. Ukweli ni kwamba, tukiweka kwenye mizania ya mema na mabaya, kwa mimi mwananchi wa kawaida naamini kuwa Mkapa aliitendea nchi hii mema mengi kuliko mabaya. Tena basi, hata uchafu wa EPA na mengine mengi inaonekana yalifanywa kwa msukumo wa kikundi kidogo cha mafisadi ndani ya chama tawala ili kupalilia njia ya kumhakikishia ushindi Kikwete.

Baada ya kuingia Kikwete kwa mbwembwe za USHINDI WA KISHINDO nchi ilianza kuyumba taratibu na hata chama chake kilianza kuyumba. Tena basi, ni bora hata ange-maintain yale aliyofanya Mzee Mkapa ili kulinda wananchi wake. Lakini hali ya wananchi kiuchumi ilianza kuporomoka mara tu aliposhika madaraka, tena kwa kasi ya ajabu. Bidhaa muhimu anazohitaji mwananchi wa kawaida katika maisha yake ya kila siku kwa mara ya kwanza zilianza kupanda bei kwa kasi ya ajabu, tofauti na wakati wa Mzee Mkapa. Bidhaa kama unga wa sembe, sukari, unga wa ngano, mkaa wa kupikia, mchele, maharage, n.k. sasa hazishikiki. Ukienda Serikalini kasi ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo ilianza kupungua taratibu. Miradi mingi aliyoacha Mzee Mkapa imekamilishwa chini ya awamu ya kwanza ya Kikwete kwa mbinde. Kuna rafiki yangu mmoja yupo Serikalini aliniambia kwamba isingekuwa ni mikataba iliyosaini Serikali na wakandarasi, huenda hata miradi hiyo aliyoacha Mzee Mkapa inge-collapse. Kwa hiyo nguvu iliyosukuma miradi ikamilishwe ni mikataba. Chini ya awamu ya kwanza ya Kikwete jamii ya kitanzania imeshuhudia kuporomoka kwa hali ya wananchi kiuchumi na mbaya zaidi hata kijamii na kisiasa. Masuala ya udini yameibuka kwa kasi na kutishia mshikamano wa wananchi. Kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, wafanyakazi kupitia chama chao waligoma kuwaalika viongozi wa Serikali kuhudhuria sherehe za Mei Mosi. Kwa mara ya kwanza katika historia ya vyama vingi nchini, hotuba ya rais ya ufungzi wa Bunge inasusiwa na wabunge kwa kutoka nje ya ukumbi. Zipo rekodi nyingi sana zilizoweka chini ya uongozi wa Kikwete.

Sasa mwaka huu, Kiwete ndiyo ameanza awamu yake ya pili na ya mwisho. Hali ndiyo inaendela kuwa mbaya zaidi. Migomo mingi nchi nzima, maandamano kila kukicha, miradi ya maendeleo imesimama, bei za bidhaa zinapanda kila kukicha, mishahara imeanza kucheleweshwa, huduma muhimu kama umeme na maji zimeanza kuporomoka na bei zake kupanda, ada za shule zinaongezeka. Hivi sasa watumishi wengi wa Serikali waliokuwa busy na shughuli za miradi enzi za Mzee Mkapa wametulia maofisini wanasoma magazeti. Kwa ujumla, hali inaendelea kuwa mbaya siku hadi siku. Wananchi wengi mitaani wameanza kukata tamaa ya maisha. Wengi wanaona kama 2015 ipo mbali sana.

Sasa kwa mwenendo huu kwa nini nisiamini kwamba MKAPA ALIJENGA NA KIKWETE ANABOMOA?

Kulingana na uchambuzi wa wataalamu wa mambo ya siasa na matukio ya Tunisia, Misri, Jordan na Yemen dunia inaonekana inaanza kupita katika kipindi kigumu ambacho hakijapata kutokea jambo ambalo litapelekea nguvu ya uuma kuchukua nafasi yake. hali hii ndio inaelezwa kuwa hata kama Rais wa sasa asingekuwa Kikwete au mwislamu au mkristo bado utawala wake ungekuwa na kazi nguvu. katika kipindi hizi tawala nyingi zinaweza kuanguka kama hazitachukua hatua madhubuti kuhimili misukosuko ya dunia ambayo ya kiasi kikubwa imechochewa zaidi na mtikisiko wa fedha duniani.

na hii inatuonyesha kwamba mataifa ya Ulaya na Amerika yana nguvu kubwa sana ya kiuchumi duniani na hasa marekani. Uchumi mkubwa wa dunia uko mikononi mwa nchi hizo. Mtikisiko wa fedha ulizikumba nchi hizo na kuenea duniani umeleta matatizo makubwa kwa nchi zinazoendelea wakati huo nchi hizo zimefanikio kuthibiti kwa kiasi cha kutosha hali hiyo.
 
kila awamu ina mapungufu yake ni makosa kudhani kuna awamu ya utawala haikuwa na mapungufu. Awamu ya nne inaweza kuwa na mapungufu lakini kusema anabomoa kazi za mkapa ni lugha kali ambayo inaonyesha kwamba kikwete hajafanya lolote pengine kwamba hata chuo kikuu cha dodoma anabomoa kazi ya mkapa
huna jingine mkuu la kuongezea!???
 
Du hivi kweli mnasahau waandhishi wa habari walivyokuwa wanabanwa, leo dunia imepanuka vyombo vya habari vipo huru mwenye uwezo unangalia AlJazeera
Bunge letu waliokuwa wanaikosoa hasa kutoka CCMwalikuwa wanaitwa Chamwino kukosolewa na kubanwa wasiseme lolote.
JK kuachia vitu vyote kuwa na uwazi mnamfananisha na Mkapa? ni nani alimweka ROSTAM kuwa mweka hazina wa chama na kuchota hela BOT wakati JK akiwa Wizara ya NJE
Tangold,meremeta, Deep green, Kiwira, ANBEN, EPA angalieni ni za mwaka gani?
mm JK bado nampa
:first:
 
Du hivi kweli mnasahau waandhishi wa habari walivyokuwa wanabanwa, leo dunia imepanuka vyombo vya habari vipo huru mwenye uwezo unangalia AlJazeera
Bunge letu waliokuwa wanaikosoa hasa kutoka CCMwalikuwa wanaitwa Chamwino kukosolewa na kubanwa wasiseme lolote.
JK kuachia vitu vyote kuwa na uwazi mnamfananisha na Mkapa? ni nani alimweka ROSTAM kuwa mweka hazina wa chama na kuchota hela BOT wakati JK akiwa Wizara ya NJE
Tangold,meremeta, Deep green, Kiwira, ANBEN, EPA angalieni ni za mwaka gani?
mm JK bado nampa
:first:

Usimsingizie Mzee Mkapa tafadhali. Nyota ya Rostam imechomoza ndani ya uongozi wa JK. Aliposhika madaraka ya chama na serikali ndiye aliyemwibua Rostam na kumpatia cheo cha Mweka Hazina wa Sisiem. Wakati wa Mkapa Rostam hakuwa na cheo hicho.
 
Semeni yote lakini Mkapa is still a good leader than jk, mkapa when says he looks like a president. JK ambaye anafikiri kila jambo haliwezekani, umeme mgao anasema hana la kufanya hakumbuki kama tuna makaa ya mawe tunaweza kutengeneza umeme wetu, amekumbuka kukodisha mitambo ya dowans mil 150 kwa siku, je how much per month and per year, situngeweza nunua mitambo yetu na kuzalisha umeme kwa bei nafuu. Sasa yeye anafikiria kunyesha mvua mikoa yote, akili za kitoto. Pia sasa tuna uranium ambayo yakizalishwa tz itakuwa produza wa pili duniani haya jk hafikirii. Uwezo wake mdogo sana.
 
Uliyosema ni kweli lakini mwananchi wa kawaida anayekwenda kununua unga wa sembe kwa sh. 800 kwa kilo badala ya sh. 300, sukari sh. 2,000 badala ya sh. 600 na mchele sh. 1,800 badala ya sh. 650 lazima ATAMKUMBUKA DAIMA MKAPA. Hayo masuala ya NBC, Deep Green na ANBEN mnayayujua ninyi mnaosoma magazeti.

Now you are talking. JK alikiri mwenyewe kuwa alichukua nchi ikiwa katika hali nzuri ya uchumi. Ni kweli inflation inaendelea kwenda juu, (Kisingizio ni financial crisis lakini Kenya iliyokumbwa vibaya zaidi haijawa affected wala Uganda wala Rwanda). It is about time akiri kuwa uchumi sasa uko ovyo,ni jambo linaloonekana kwa kila mwenye kuona.

Lakini still wa kumlaumu ni Mkapa, maana alijua ni nani wanaingia kuitawala nchi na kwa lengo gani. He knew long before he left the office, alituzira.
 
mkapa kaharibu sana hakuna mfano mpaka kipindi cha chake kilitwa UKAPA,wengi tuliona miaka10 kama mia. Mkapa na mkewe wamepiga sana bizness ikulu. Acheni ugalatia kuweni wakweli
 
Mkapa,kikwete hao wote ni zero. Huyo wa kwanza alitutesa usiku na huyu wa pili anatutesa mchana
 
mkapa alikuwa mwizi wa mali za watanzania lkn kikwete ni jambazi sugu na ni mkuu wa majambazi
Kama rostam aziz.chenge.lowasa nk
 
huyu jk amesimama juu y amabega ya mkapa kwa miaka 5 yote na amekula kila kitu........

mbishi ni mbishi tu hata awekwe kwenye chupa bado atanyoosha kidole........ jk ni mbishi sana na hana maana kabisa
 
Kila awamu ina mapungufu yake ni makosa kudhani kuna awamu ya utawala haikuwa na mapungufu. Awamu ya nne inaweza kuwa na mapungufu lakini kusema anabomoa kazi za Mkapa ni lugha kali ambayo inaonyesha kwamba kikwete hajafanya lolote pengine kwamba hata chuo kikuu cha Dodoma anabomoa kazi ya Mkapa

yaani madudu ya udom hujayasikia?yale madudu ya maprofesa kina Kikula?nani kawaweka?
 
Hivi tukimlinganisha mkapa na kikwete kuna mtu atasema mkapa ni mbaya in overall? Acheni ushabiki hapa tuseme ukweli. Kikwete na mwinyi sawasawa hawana sifa za viongozi imara at all.
 
Hoja yako ni ya msingi na ninakubaliana na wewe. Nadhani unachotaka kieleweke ni kwamba udhaifu wa Kikwete usimtakase Mkapa. Sasa swali langu ni je, baada ya kugundua udhaifu huo ambao umepelekea umeme na huduma zingine kuwa juu, Kikwete amefanya nini ndani ya miaka takriban sita sasa ya uongozi wake? Mbona naona kama madudu yanazidi kuongezeka badala ya kupungua? Mwl. Nyerere aliwahi kutuasa kwamba kila serikali lazima itafanya makosa yake maana serikali haziongozwi na malaika. Jambo muhimu ni kwamba serikali mpya inapoingia inarekebisha makosa na kuendeleza mazuri na ya msingi ya serikali iliyopita. Kwa mtazamo ndugu yangu Nguruvi3 unadhani hali hii ndiyo inayotokea sasa chini ya uongozi wa Kikwete?? Nisaidie tafadhali.

Ukitaka kufahamu mafanikio ya kiongozi ni kuangalia hali ya uchumi kwa mwananchi wa kawaida kabisa. Mkapa alidhibiti sana inflation, kwa maneno mengine thamani ya pesa iliongezeka japo mshahara unaweza kuwa mdogo. Haya ni mafanikio ambayo hayapaswi kubezwa. Tatizo la Mzee huyu ni kiburi. Alikuwa anafanya mambo bila kujali wananchi wake wanasemaje. Alikuwa mbabe na ndiyo maana tuliwasikia akina Mramba wakisema ndege itanunuliwa hata kama watu wale nyasi. Mkapa akaidhinisha malipo ya rada ambayo leo tunajua ilikuwa deal mbaya kwa taifa labda nzuri kwakwe na familia yake. Ni mkapa aliyewalea akina Chenge wenye vijisenti dollar milion 2. Jeuri yake ni kuuza nyumba za serikali kwa rafiki zake leo tunajenga upya. Jeuri ni kuuza kiwira kwa familia yake leo tunalia na umeme. Jeuri ni kuuza NBC kwa bei ya kishikaji, kuleta Netgroup n.k. Alifanya madudu licha ya mazuri aliyoyafanya.
JK sijui niseme nini, inflation imepaa, uchumi hauna mweleleko. Kibaya zaidi kinachoudhi watu ni kutumia ujanja kuwahadaa ili aonekane mzuri kwa kila mtu. Akiwa ikulu anasema Dowans ilipwe, akienda Ubungo Plaza kuonana na wabunge anasema hapendi Dowans ilipwe.
Akija kwa wananchi anasema anataka orodha ya mafisadi. Akipewa orodha anaminya kimya! Akija kwa wananchi anasema iundwe tume wakati madudu yakifanyika aliyaona kama waziri wa Nishati, waziri wa fedha, waziri wa mambo ya nje. Sasa mambo kama haya ukichanganya na uswahiba wa marafiki zake yanajaza watu hasira. Leo ukiniambia nini mwelekeo wa nchi, sina jibu.
Lakini dhidi ya yote haya hakuna uzuri unaosafisha ubaya. Yale ya mkapa tuyaseme hadharani mazuri na mabaya, JK pia.
 
Back
Top Bottom