Kesho Bajeti kwanza Mchanga baadae!

Salvatory Mkami

Senior Member
Apr 17, 2013
146
244
Kwa wale mtakaopata muda siku ya kesho msiache kufuatilia vikao vya Bunge ambapo kambi rasmi ya upinzani Bungeni itasoma bajeti mbadala ya wizara ya fedha kwa mwaka 2017/2018.

Kwa wale wasiotambua au kusahau niwakumbushe tu kwamba kilichosomwa na waziri wa fedha Dk. Mpango ni "Bajeti Pendekezwa" Bunge ndilo hupitisha Bajeti. Kwahiyo tunapaswa kuisikiliza kwa makini "Bajeti Pendekezwa" ya upande wa pili (Upinzani) ili kuona kama kuna mambo muhimu ambayo yanaweza kuiboresha bajeti hiyo ya Dk Mpango, ila tu ninaamini hilo linawezekana iwapo tuna watu wanaojitambua na kukubali kushauriwa kwa maslahi mapana ya taifa!

Natumai kama ilivyo kawaida Kambi rasmi ya upinzani Bungeni itapongeza bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 pale inapotakiwa kupongezwa na kuikosoa pale inapohitaji kukosolewa. Kwa wale vijana wa Lumumba waliozoea kushabikia na kupongeza kila jambo hususani maamuzi na ripoti ambazo hazitakiwi kukosolewa waendelee kushabikia tamthilia namba2 ya mchanga lakini wasisahau kwamba nyeupe haiwezi kuitwa nyeusi!

Hata hivyo sintashangaa iwapo vyombo mbalimbali vya habari vitaelekezwa zaidi katika kurusha tukio la makabidhiano ya ripoti namba2 ya mchanga kuliko bajeti!
 
CCM wa hovyo sana badala wangerusha bajeti mbadala ili Wananchi wachambue pumba na mchele, kwa roho mbaya waliyonayo hawatarusha.
 
Bungeni natarajia kusikia yaleyale ninayoyasikia kila mwaka wa bajeti(Another silly season).
Kesho nasikiliza taarifa ya makinikia.
 
Kwa wale mtakaopata muda siku ya kesho msiache kufuatilia vikao vya Bunge ambapo kambi rasmi ya upinzani Bungeni itasoma bajeti mbadala ya wizara ya fedha kwa mwaka 2017/2018.

Kwa wale wasiotambua au kusahau niwakumbushe tu kwamba kilichosomwa na waziri wa fedha Dk. Mpango ni "Bajeti Pendekezwa" Bunge ndilo hupitisha Bajeti. Kwahiyo tunapaswa kuisikiliza kwa makini "Bajeti Pendekezwa" ya upande wa pili (Upinzani) ili kuona kama kuna mambo muhimu ambayo yanaweza kuiboresha bajeti hiyo ya Dk Mpango, ila tu ninaamini hilo linawezekana iwapo tuna watu wanaojitambua na kukubali kushauriwa kwa maslahi mapana ya taifa!

Natumai kama ilivyo kawaida Kambi rasmi ya upinzani Bungeni itapongeza bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 pale inapotakiwa kupongezwa na kuikosoa pale inapohitaji kukosolewa. Kwa wale vijana wa Lumumba waliozoea kushabikia na kupongeza kila jambo hususani maamuzi na ripoti ambazo hazitakiwi kukosolewa waendelee kushabikia tamthilia namba2 ya mchanga lakini wasisahau kwamba nyeupe haiwezi kuitwa nyeusi!

Hata hivyo sintashangaa iwapo vyombo mbalimbali vya habari vitaelekezwa zaidi katika kurusha tukio la makabidhiano ya ripoti namba2 ya mchanga kuliko bajeti!
Bajeti mbadala ya Wizara ya fedha so ilishasomwa au Silinde anairudia tena?!
 
Kwa wale mtakaopata muda siku ya kesho msiache kufuatilia vikao vya Bunge ambapo kambi rasmi ya upinzani Bungeni itasoma bajeti mbadala ya wizara ya fedha kwa mwaka 2017/2018.

Kwa wale wasiotambua au kusahau niwakumbushe tu kwamba kilichosomwa na waziri wa fedha Dk. Mpango ni "Bajeti Pendekezwa" Bunge ndilo hupitisha Bajeti. Kwahiyo tunapaswa kuisikiliza kwa makini "Bajeti Pendekezwa" ya upande wa pili (Upinzani) ili kuona kama kuna mambo muhimu ambayo yanaweza kuiboresha bajeti hiyo ya Dk Mpango, ila tu ninaamini hilo linawezekana iwapo tuna watu wanaojitambua na kukubali kushauriwa kwa maslahi mapana ya taifa!

Natumai kama ilivyo kawaida Kambi rasmi ya upinzani Bungeni itapongeza bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 pale inapotakiwa kupongezwa na kuikosoa pale inapohitaji kukosolewa. Kwa wale vijana wa Lumumba waliozoea kushabikia na kupongeza kila jambo hususani maamuzi na ripoti ambazo hazitakiwi kukosolewa waendelee kushabikia tamthilia namba2 ya mchanga lakini wasisahau kwamba nyeupe haiwezi kuitwa nyeusi!

Hata hivyo sintashangaa iwapo vyombo mbalimbali vya habari vitaelekezwa zaidi katika kurusha tukio la makabidhiano ya ripoti namba2 ya mchanga kuliko bajeti!
naona wanahaika kuandaa sherehe ya uzinduzi wa ripoti wanamuziki maarufu watatumbuiza
 
Bajeti imeshapita hiyo,wabunge wengi unajua ni wa upande upi.Watu watasikiliza ripoti ya mchanga.
 
Ni tusi kubwa sana mtu kukwambia wewe ni CHADEMA!

Hivi Chama ambacho Hakina Wabunge wengi nacho kinasoma Budget halafu watanzania wafuatilie?

Kama CHADEMA ingekua na Wabunge wengi ambapo nafikiri hata waziri Mkuu angetoka Chadema hapo Ndo Ingekua Bonge la Budget na ndo budget ambayo ingeweza Kupita.

Lakini Kwa Sasa Vuteni madawa ya Kulevya kwa Mara ya Mwisho Kesho muwe fiti kwa Ripoti kwa sababu Budget ya Upinzani ni geresha/formalities tuu!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom