Kero za uandishi mbaya wa maneno

decomm

JF-Expert Member
Dec 10, 2013
726
655
Habari?

Hongera CAG mstaafu kwa kustaafu kwa heshima na karibu CAG mpya.
__

Moja kwa moja niende kwenye mada.

Ninaamini wadau waliomo humu wamepata elimu angalau ya darasa la saba, kama wapo wa chini ya hapo basi ni wachache sana.

Lakini bado najiuliza hivi ni kweli bado watu wanakosea kuandika maneno kwa usahihi licha ya kukaa shuleni zaidi ya miaka minne?

Sizungumzii "typing errors", bali nazungumzia kutokujua tofauti ya neno fulani na fulani ambayo ni maneno ya kawaida sana na hutumika kila siku. (nitatoa mifano)

Pia sizungumzii wale wanaoandika neno kwa usahihi lakini kutokana na lahaja ya alipozaliwa au kukulia akalitamka neno hilo tofauti kidogo, hii hainipi kero.

Nakerekwa na uandishi kama huu:

1. Abari, habali, abali badala ya kuandika "habari".

2. Ongera, Hongela, ongela badala ya kuandika "hongera".

Meneno yakosewayo yapo mengi, sehemu za kuweka R wanaweka L na kinyume chake, lakini pia sehemu za kuweka H hawaweki na kadhalika.

"Haina shida" msomi mzima utakuta ameandika "aina shida".

"Weka namba", utakuta imeandikwa "eka namba"

Hivi ni kweli walimu hawakufundisha kuandika vizuri?

Tatizo ni nini?

JF siku hizi nyuzi nyingi zina kero za uandishi wa namna hiyo. Vijana mnakwama wapi? Hata lugha yetu wenyewe?
 
Hata wewe mleta uzi tayari umefanya makosa ya kiuandishi kwenye heading.
Ulipaswa usitumie neno "ya" na badala yake ungetumia neno "za" kwasababu neno la mwisho kwenye heading lime reflect wingi.

Na hata pale ulipaswa undike "m-baya" badala ya neno "mbaya" kwa sababu kwa msomaji asiye makini tayari utakuwa umeleta maana tofauti kabisa na kile ulicho kusudia kukiwasilisha.
 
Umepewa ya uso tayari...!!

Uandishi haujawahi kuwa kazi rahisi hasa kwa mtu ambaye kazi yake sio uandishi.

Ila usiache kusaidia pale kanuni za uandishi zinapokosewa Ila jitahidi kuwa mtu wa kutoa msaada na sio mkosoaji.
 
Umepewa ya uso tayari...!!

Uandishi haujawahi kuwa kazi rahisi hasa kwa mtu ambaye kazi yake sio uandishi.

Ila usiache kusaidia pale kanuni za uandishi zinapokosewa Ila jitahidi kuwa mtu wa kutoa msaada na sio mkosoaji.
Nimeamua kutobishana naye, nukta yangu haipo kwenye mukhtadha alio onesha yeye, hata hivyo nipo sahihi, angalia:-

1. Kero ya uandishi m-baya...
(Uandishi m-baya wa nini?)

2. ...wa maneno

Sahihi kabisa. Ni kero moja ya uandishi m-baya...

Tuachane na hilo, nukta yangu bado ipo pale pale kwa wale ambao NAAMINI WAMESOMA KISWAHILI, lakini bado wanashindwa kuandika vizuri baadhi ya maneno, tena kwa kurudia kosa ama makosa hayo hayo mara kadhaa.

Wale wanaofupisha neno ama maneno kwa usahihi wala kwangu siyo kero, ukiandika KTK badala ya KATIKA mie hainipi kero, labda wale wanaoandika XAXA badala ya SASA, sijui hata wanafupisha nini, aaaaggggrrrrr!

FORTUNATUS ukiandika 42&2C angalau inaeleweka, lakini siyo ASUBUHI uandike HASUBUI, ingawaje wale walio athiriwa na lafudhi za lahaja zao wakati wakitamka hawanikeri, ila wakiandika kwa kukosea napo kwangu inakuwo ni kero.

Sizungumzii "typing errors", makosa ya typing inaeleweka.

Msingi wa uzi ulikuwa kuangalia huko mashuleni walifundishwa hivyo!? Ama ni nini kimetokea, maana vijana wengi wanaandika hovyo.
 
Am one of those bt nafanya makusudically idk ni uvvu or what....
Nachukuwa mfano mmoja tu katika sentesi yako...

UVVU, imeeleweka umefupisha japo siyo kifupisho kilichokubaliwa, sasa vipi mtu akiandika HUVIVU

!

Kero kwangu ndio huja hapo.
 
Kiswahili somo la ajabu sana

Unaweza kupa A Masomo yote isipokuwa...

Kiswahili ukapata D au E au F

Tamathali za semi, ngeli nk

Maudhui

Uchambuzi wa sentensi ... njia ya Matawi au jedwali

Aina za maneno na longolongo zake

Fasihi andishi, fasihi simulizi

Hapana kabisa.. hili somo nachangamoto linapofikia kwenye taaluma....mtaani ni rahisi sana, ingia darasani upambane na tashtiti, tabaini, takrili, tafsida nknk
 
Hata wewe mleta uzi tayari umefanya makosa ya kiuandishi kwenye heading.
Ulipaswa usitumie neno "ya" na badala yake ungetumia neno "za" kwasababu neno la mwisho kwenye heading lime reflect wingi.

Na hata pale ulipaswa undike "m-baya" badala ya neno "mbaya" kwa sababu kwa msomaji asiye makini tayari utakuwa umeleta maana tofauti kabisa na kile ulicho kusudia kukiwasilisha.
Kiswahili hakina neno m-baya
 
Nukta yangu labda haionekani badala yake nashambuliwa!

Endeleeni kuandika "...HASUBUHI, KILOHO safi HAMBAPO kila mmoja HAKISOMA ataona AINA shida"

Nilitaka kuendelea kuandika lakini naona najikera mwenyewe.
 
Nukta yangu labda haionekani badala yake nashambuliwa!

Endeleeni kuandika "...HASUBUHI, KILOHO safi HAMBAPO kila mmoja HAKISOMA ataona AINA shida"

Nilitaka kuendelea kuandika lakini naona najikera mwenyewe.

Pole mkuu, usichoke kufundisha ni wito.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom