Kero yangu majirani wanaoharibu ndoa za watu, andika na wewe ya kwako ili tuwarekebishe

Pedra buyer

Member
Apr 26, 2015
97
31
Hivi nyie majirani mnaoharibu ndoa za watu, mnagombanisha wanandoa wasielewane kwa maneno ya umbeya ukimuona baba flani kaka sehemu either bar au sehemu yeyote na mwanamke tayari umepeleka umbea kwa mama flani eti umemuona baba flani yupo na kimada na chumvi nyingi unaongeza.

Nikuulize kwani wewe unawajua dada zake na baba flani? Mtu anashangaa karudi nyumbani wife amenuna na maneno juu ya kashfa anakupa ukijitathmini hujafanya anayokuambia sasa jamani hapo kinachofuata ni nini? Kama sio kuchapana makonde kama Manny pacquio na Mayweather. Kwanini lakini? Mnagombanisha ili mpate nini? Wakiachana unalipwa na nani, mnisamehe kama nimekosea.
 
Pole sana mkuu! Mjenge mwenzio asiwe mtu wa kusikiliza maneno ya watu na kuchukua maamuzi haraka, picha chukulia hiyo kama changamoto isiyoepukika sehemu yoyote utakayoishi hapa duniani. Ukiwa na pesa au mafanikio na ukiwa na mtu mnapendana sana.. Watu watachukia! Ni kawaida, huna uwezo wa kuzuia wasiseme ila una uwezo wa kuzuia kuwasikiliza regardless wanachosema ni kweli au uongo! Ukiwa mtu wa kuwapuuzia, watapunguza speed ya kusema yasiyowahusu!
 
Mi naomba nikushauri.........Hama huo mtaa.........sio mtaa wa kuishi huo........am tellin ya......
 
Mi naona ni mazingira unayojijengea tu
Kuwa na privacy na maisha yenu uone kama yatatokea hayo ila mambo ya familia ukiyaweka wazi kwa majirani wanawazoea na wanakua na guts za kuwaletea umbeya
 
Mi naomba nikushauri.........Hama huo mtaa.........sio mtaa wa kuishi huo........am tellin ya......

mkuu atahama mitaa mingapi?? Watu wa namna hiyo wapo kila mahali!! Anapaswa atatue tatizo na si kulikimbia, maneno ya mafisadi viwembe hayakimbiwi! Wajenge tabia ya kuwapuuzia na kutozoeana nao na kutokuwa nao karibu!
 
Mi naona ni mazingira unayojijengea tu
Kuwa na privacy na maisha yenu uone kama yatatokea hayo ila mambo ya familia ukiyaweka wazi kwa majirani wanawazoea na wanakua na guts za kuwaletea umbeya

mkuu, nakubaliana nawe 100%
 
Hayo ni huko kwenu tu huku kwetu hayapo. By the way kwa nini unywe kwenye bar au pub za karibu na home? Kama ni hivyo si unywee nyimbani tu na hao jamaa zako?
 
Honestly binafsi huwa nachukizwa na baadhi ya wanawake wenzangu for some of their behaviors . Binafsi saa nyingine naona ni bora uwe na marafiki Wa kiume wenye tabia safi kuliko kuwa na urafiki na mwanamke mwenzangu... Yaani kuna chuki sana kati ya mwanamke na mwanamke .. Hata umpendeje as a friend or best friend just know one she will hurt you very bad and regret it... Women, women.

. Nilikutanishwa na mdada Fulani kwa ajili ya kumpa mzigo Fulani . She never knew me and I have never knew her at all ... My Love wanted me to deliver something for our special love ones.. Guess what happened? Since my little sister and I got there on the site She talked nonstop .. Finally we said goodbye to each other... We left from there and went home ... Can you believe after that what she did that woman..

She is married and have her own family .. She went to tell My Love crazy things plus criticized me so much one of the thing she told my Love that not to marry me .. Thanks be to God that He knows me better ... That woman judged me mpaka nilivyovaa ..Uwiiii .. Nilichoka... kumbuka alifanya kwa my Love kuhusu Mimi... ukija upande wangu Mimi kumuharibia mwenzangu akawa ananitumia texts kwa kujionyesha kuwa anaijua family ya my Love ili mimi nimuone mwenzangu muongo ...

you know imagine huyu Dada hanijui hata na hajawahi hata siku moja kuniona .. but just for one day to see me she got something to talk about me to my Love.. hebu je kama ingekuwa mimi na mwenzangu hatushei vitu na kuelewana tungekuwa wapi now ? .. so my dear hauko peke yako ..uliyopitia hayo.. if you know uko clean nothing to worry just talk to your wife . Make her understanding ... And next time try kujiepusha na mazingira ya utatanishi na mkeo .. Thanks ..
 
Honestly binafsi huwa nachukizwa na baadhi ya wanawake wenzangu for some of their behaviors . Binafsi saa nyingine naona ni bora uwe na marafiki Wa kiume wenye tabia safi kuliko kuwa na urafiki na mwanamke mwenzangu... Yaani kuna chuki sana kati ya mwanamke na mwanamke .. Hata umpendeje as a friend or best friend just know one she will hurt you very bad and regret it... Women, women.. Nilikutanishwa na mdada Fulani kwa ajili ya kumpa mzigo Fulani . She never knew me and I have never knew her at all ... My Love wanted me to deliver something for our special love ones.. Guess what happened? Since my little sister and I got there on the site She talked nonstop .. Finally we said goodbye to each other... We left from there and went home ... Can you believe after that what she did that woman.. She is married and have her own family .. She went to tell My Love crazy things plus criticized me so much one of the thing she told my Love that not to marry me .. Thanks be to God that He knows me better ... That woman judged me mpaka nilivyovaa ..Uwiiii .. Nilichoka... kumbuka alifanya kwa my Love kuhusu Mimi... ukija upande wangu Mimi kumuharibia mwenzangu akawa ananitumia texts kwa kujionyesha kuwa anaijua family ya my Love ili mimi nimuone mwenzangu muongo ... you know imagine huyu Dada hanijui hata na hajawahi hata siku moja kuniona .. but just for one day to see me she got something to talk about me to my Love.. hebu je kama ingekuwa mimi na mwenzangu hatushei vitu na kuelewana tungekuwa wapi now ? .. so my dear hauko peke yako ..uliyopitia hayo.. if you know uko clean nothing to worry just talk to your wife . Make her understanding ... And next time try kujiepusha na mazingira ya utatanishi na mkeo .. Thanks ..

Nimekuelewa Dada angu.asante
 
Ila kweli wanawake ni wambea sana ata baadhi ya wanaume nao ni wambea.
Ivi mtu anajisikiaje fulani na fulani wamegomban or hawaelewan or wameachana kwa ajili ya maneno yake? Aaaagrrrrrrrrrrrr.
Mimi ata nimkute shemeji yangu ana mega nje sisemi ng'ooo coz wataomban msamaha yataisha aya mie cha umbea nakuwa mgeni wanani niliyetaka kuvunja ndoa ya dada yangu?
Wadada tujifunze kumezea siri jamani lol
 
Mitaa ya uswahili hiyo.
Huku kwetu hatujuani na mtu, hadi msiba utokee ndo mwakutana.
Ila wengi wa hao watu wivu huwa wawasumbua wanaona kama unafaidi sana
 
Na wewe kama ni dada zako kwa nini usiwakaribishe nyumbani... Bar ndiyo kuna nini? ebooo... Tabia mbaya huanzia Bar... umalizikia Guest/Lodge/Hotelini...
 
Mi naomba nikushauri.........Hama huo mtaa.........sio mtaa wa kuishi huo........am tellin ya......
Hahaha!Atahama mitaa mingapi?Ataumaliza mji bure.Solution akae tu na mkewe amweleweshe aache kusikiliza ya watu.
 
Usilaumu majirani laumu mke wako mwenye akili yakushikiwa,ivi jairani anaanzaje kunambia nimemuona mumeo bar au sijui guest na mwanamke?
inaelekea hamuaminiani tangu zamani hao majirani wanakua chambo tuu huyo mkeo hata ukimuweka mwituni atakwambia wanyama wamemwambia, acheni kuogopa wake zenu mweleze ukweli ukiwa kama mwanmme umekuja kutoka kazini umechoka una hitaji mapumziko
sio stress.......
 
pole sana yamekukuta mwaaka huuu? au lini huo utakuwa mkosi wako nenda kaoge ,maana watu wengine mpaka wanazaa nje ya ndoa zao wake zao hawana taarifa ww pole .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom