kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,222
- 1,667
Ndugu wanajamvi, awali nawapa pole kwa uchovu unaotokana na majukumu ya ujenzi wa taifa letu. Niko maeneo ya ocean road Dar. karibia na makumbuko ya taifa, usiku siku hizi, hasa weekend days kumegeuka kuwa kero kwa majirani, hasa taasisi mbalimbali zinazozunguka eneo hili lenye jengo linaloitwa National Museum Dar es salaam, kumbuka makumbusho yetu imepakana na Chuo cha IFM, Ocean road hospital, ukumbi wa bunge, Chuo cha taifa cha Utalii, na taasisi nyingine nyingi, pia kuna baadhi ya apartments za makazi ya raia. Eneo la wazi la sehemu ya Makumbusho limekuwa likikodishwa kwa sherehe mbalimbali; harusi, sendoff, kitchen party n.k, Tatizo kubwa ni kero ya inayotokana na kelele za sauti ya miziki inayopigwa hadi usiku wa manane, kwakweli, majirani wa eneo hili hasa wanafunzi wanashindwa kusoma, na wagonjwa wa hospitali ya ocean road, mbali ya magonjwa wanapata kero ya kelele za muziki kutoka eneo la makumbusho; kwa mfano usiku wa leo kulikuwa na kelele za muziki kwa sauti ya juu hadi muda wa saa saba na nusu. Mimi ninavyofahamu makumbusho ni sehemu yenye utulivu, na panapaswa kuheshimiwa, lakini hapa tanzania ni tofauti kabisa. Kwa ufupi naomba mamlaka zinazohusika kusimamia sheria zinazokataza kero za sauti na miziki, ili kutupa nafasi ya kupumzika na kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa taifa letu kwa siku inayofuata. Pia nashauri kuwe na udhibiti wa hizi kero kwa wanaoishi jirani kumbi za starehe, wakati mwingine nyumba za ibada zinazofanya shughuli zao wakati wa usiku. Asanteni naomba kuwakilisha.