Kero ya kelele za miziki kutoka Makumbusho usiku wa manane

kbm

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
5,222
1,667
Ndugu wanajamvi, awali nawapa pole kwa uchovu unaotokana na majukumu ya ujenzi wa taifa letu. Niko maeneo ya ocean road Dar. karibia na makumbuko ya taifa, usiku siku hizi, hasa weekend days kumegeuka kuwa kero kwa majirani, hasa taasisi mbalimbali zinazozunguka eneo hili lenye jengo linaloitwa National Museum Dar es salaam, kumbuka makumbusho yetu imepakana na Chuo cha IFM, Ocean road hospital, ukumbi wa bunge, Chuo cha taifa cha Utalii, na taasisi nyingine nyingi, pia kuna baadhi ya apartments za makazi ya raia. Eneo la wazi la sehemu ya Makumbusho limekuwa likikodishwa kwa sherehe mbalimbali; harusi, sendoff, kitchen party n.k, Tatizo kubwa ni kero ya inayotokana na kelele za sauti ya miziki inayopigwa hadi usiku wa manane, kwakweli, majirani wa eneo hili hasa wanafunzi wanashindwa kusoma, na wagonjwa wa hospitali ya ocean road, mbali ya magonjwa wanapata kero ya kelele za muziki kutoka eneo la makumbusho; kwa mfano usiku wa leo kulikuwa na kelele za muziki kwa sauti ya juu hadi muda wa saa saba na nusu. Mimi ninavyofahamu makumbusho ni sehemu yenye utulivu, na panapaswa kuheshimiwa, lakini hapa tanzania ni tofauti kabisa. Kwa ufupi naomba mamlaka zinazohusika kusimamia sheria zinazokataza kero za sauti na miziki, ili kutupa nafasi ya kupumzika na kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa taifa letu kwa siku inayofuata. Pia nashauri kuwe na udhibiti wa hizi kero kwa wanaoishi jirani kumbi za starehe, wakati mwingine nyumba za ibada zinazofanya shughuli zao wakati wa usiku. Asanteni naomba kuwakilisha.
 
Tamaa ya pesa inafanya viongozi wetu wahatarishe afya za wananchi. Pole sana mkuu, hapo kisheria unaweza kuwashtaki kwa bughudha mnazopata, lakini kwa vile kile sehemu zimewekwa mfukoni basi ni tabu tupu.
 
Harusi, Kitchen parties, Guest Houses, Glosaries na Pharmacies ndiyo biashara kubwa inayoabudiwa na wengi wa watu wetu. Hawaoni umuhimu wa kuwaachia watu wengine fursa ya kuishi maisha yao. Ukienda shule ya Uhuru Kariakoo unaweza kugeuka kichaa kutokana na miziki. Bado kelele toka misikitini tena alfajiri. Nchi yetu ni kama ya wendawazimu vile.
 
Harusi, Kitchen parties, Guest Houses, Glosaries na Pharmacies ndiyo biashara kubwa inayoabudiwa na wengi wa watu wetu. Hawaoni umuhimu wa kuwaachia watu wengine fursa ya kuishi maisha yao. Ukienda shule ya Uhuru Kariakoo unaweza kugeuka kichaa kutokana na miziki. Bado kelele toka misikitini tena alfajiri. Nchi yetu ni kama ya wendawazimu vile.

Kwingine koooote sawa, hapo kwenye nyekundu sijapakubali na nahisi comment hii ina chuki. Adhana ya alfajiri ni inadumu kwa muda gani kiasi cha kuwa kero. Tuheshimiane na tutambue haki za majority.
 
Tamaa ya pesa inafanya viongozi wetu wahatarishe afya za wananchi. Pole sana mkuu, hapo kisheria unaweza kuwashtaki kwa bughudha mnazopata, lakini kwa vile kile sehemu zimewekwa mfukoni basi ni tabu tupu.

ni kweli mkuu' inawezekana kabisa ni ka-mradi ka boss. Leo asubuhi nimejaribu kufuatilia nikaambiwa maboss ndiyo wanaohusika. Eti na vyombo na vifaa vya muziki vinatunzwa hapohapo makumbusho.
 
nchi hii kila mtu anafanya atakalo.....poleni sana

Asante mkuu' baadaya kufanya kudodosa zaidi kwa wakazi wamaeneo haya' wanaseme eti' hata eneo la Karimjee hall ni vilevile, hizi taasisi mbili imekuwa ni kero wakazi wa maeneo' kila mwisho mwa juma ni mtindo moja, kelele kwa kwenda mbele. Fikiria ni karibia sana IKULU, kwa mh JK, kweli nchi yetu inaelekea kubaya, sidhani henzi za Kambarage kama yangefanyika haya!
 
Harusi, Kitchen parties, Guest Houses, Glosaries na Pharmacies ndiyo biashara kubwa inayoabudiwa na wengi wa watu wetu. Hawaoni umuhimu wa kuwaachia watu wengine fursa ya kuishi maisha yao. Ukienda shule ya Uhuru Kariakoo unaweza kugeuka kichaa kutokana na miziki. Bado kelele toka misikitini tena alfajiri. Nchi yetu ni kama ya wendawazimu vile.

... Kweli viongozi wetu wamepoteza mwelekeo. Najiuliza sasa nani atasimamia sheria na kanuni za nchi, kama wenye mamlaka wanapuuza utaratibu mzima wa kuongoza nchi?
 
ni kweli mkuu' inawezekana kabisa ni ka-mradi ka boss. Leo asubuhi nimejaribu kufuatilia nikaambiwa maboss ndiyo wanaohusika. Eti na vyombo na vifaa vya muziki vinatunzwa hapohapo makumbusho.
Hatuthamini maisha yetu wenyewe na ndipo tunapoonekana wajinga kila kukicha mbele ya mzungu, mzungu anatoka shamba, akifika tanzania anapewa heshima kuubwa! Ukiacha ajali zinazoua ndugu zetu kila siku kwa uzembe wa wenye dhamana, kuna vitu vingine sana ambavyo tunajidhalilisha wenyewe! utakuta eneo la uwazi watu wanapiga bei ijengwe hoteli au ubadili matumizi, huu ni uwenda wazimu wa viongozi wetu vilaza. Kuuza kiwanja cha wazi auu kubadili matumizi maana yake kiongozi ameshindwa kufikiria namna ya kuuendeleza huo uwanja. Ni sawa na hiyo sehemu ya makumbusho, badala ya kuvutia watu kwenda kutalii wanajaza makelele, upuuzi mtupu.
 
Hao wenye ukumbi ndio wanatakiwa waweke sound proof kwani wanawabughuzi wananchi wengine ambao wana haki ya kuishi bila bughuza
Wekeni sound flufuuu masikioni mwenu acheni watu wapige pesa bwana
 
Wekeni sound flufuuu masikioni mwenu acheni watu wapige pesa bwana

mkuu, wewe tukuweke kundi gani? au ndiyo vilaza? Kumbuka eneo hili ni sehemu ya taasisi nyeti kuliko hata Ikulu.
 
hivi kelele hizi hazifiki IKULU maana iko karibu sana, au anaona raha akisikia miziki ya saa sita hasa ya Wazee wa Ngwasuma, naye anaamuka kucheza!!
 
Kwingine koooote sawa, hapo kwenye nyekundu sijapakubali na nahisi comment hii ina chuki. Adhana ya alfajiri ni inadumu kwa muda gani kiasi cha kuwa kero. Tuheshimiane na tutambue haki za majority.

Issue siyo muda kiasi gani,muhimu ni kelele toka ktk vipaza sauti vyenye sauti kali. Mfano,adhana toka Kariakoo inasikika mpaka Sinza ama maeneo mengine mbali sasa hizo si fujo jamani? Pili ktk dunia iliyopiga hatua hivi ktk kupashana habari bado tunahitaji njia hizi za kijima kuamshana kuswali?
 
Issue siyo muda kiasi gani,muhimu ni kelele toka ktk vipaza sauti vyenye sauti kali. Mfano,adhana toka Kariakoo inasikika mpaka Sinza ama maeneo mengine mbali sasa hizo si fujo jamani? Pili ktk dunia iliyopiga hatua hivi ktk kupashana habari bado tunahitaji njia hizi za kijima kuamshana kuswali?

Na chumvi mma, sinza na kariakoo wapi na wapi, nshakufahamu. Eh na ibada nazo mnataka ku digitalize? kweli kizazi hiki kina mambo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom