chiefnyumbanitu
JF-Expert Member
- Nov 28, 2015
- 906
- 426
Naomba nielekewe nataka nihame tigo chap kwenda halotel nafanyaje
Siyo kweli wamesema zinazobadilika ni code numbers za mwanzoMfano una namba yako ina zaidi ya miaka mitano hata saba, ni tigo.
watu wengi wanaifahamu.
Wateja wako wa ndani na nje ya nchi wanaifahamu hiyo namba.
Unaona tigo inakuzingua siku zote uwa unatamani kuhamia mtandao mwingine lakini unachelea kuhama kwakuwa watu wengi wanaijua hiyo namba na una wateja unahisi unaweza wapoteza kwa kuhama.
So TCRA kwa hii huduma unaweza badilisha hiyo namba ikawa voda au halotel au smart n.k pasipo kubadili hata tarakimu moja itabaki vile vile.
Mfano wake ndiyo huo..
Siyo kweliMkuu! Namba yako Tanzania ni moja tu; hakuna hata mmoja mwenye nambs kama yako hata huko mitandao mingine
Mkuu ingekuwa hivyo basi haina maana ya kusema namba ile ile halafu itakuwa na tofauti gani na special number maana kuna mtu unakuta ana namba ziko hivi..Siyo kweli wamesema zinazobadilika ni code numbers za mwanzo
Hamna tofauti kubwa zaidi ya kuweza kutumia chip moja na kubadili namba upendavyo..Mkuu ingekuwa hivyo basi haina maana ya kusema namba ile ile halafu itakuwa na tofauti gani na special number maana kuna mtu unakuta ana namba ziko hivi..
0712800400
0755800400
0784800400
Hizo namba zinafanana kasoro code ya mwanzo na ni special number hata mimi niliwahi tengeneza mwaka juzi ya tgo na voda.
Sasa kwa maelezo yako inayofauti gani na special number
Mngelisoma bachelor ya Telecommunications Engineering UDSM.
Then mkaenda kuchukua Postgraduate diploma ya Computer Science with Business Information Copenhagen Denmark
Mwisho mkamalizia na degree ya Upadri nchini Uholanzi kama mimi...
Nadhani msingeuliza maswali hayo!!
Kama kweli ni hivyo it doesnt make any sense at allHamna tofauti kubwa zaidi ya kuweza kutumia chip moja na kubadili namba upendavyo..
namba yako haibadiliki hata tarakimu moj itabaki hiyo hiyo 0713..... lakini mtandao unasoma vodacom, nimemuelewa sana kwa alivofafanuAsante kwa ufafanuzi,lakini swali lingine ni hili,kule nnakohamia hakutakua na muingiliano wa mawasiliano? Mf. Namba yangu ya tigo ni 07130000,nataka kuhamia voda ambako kuna mtu ana the same namba kasoro mtandao tu,me ni tgo na yey ni voda,hakutakua na muingiliano? Au voda watalazimika kuisoma namba yangu km ilivyo pasipo kubadilisha namba za mwanzo km 0755........
Kwa kifupi hakutakuwa tena na code namba za Voda, Tigo au Halotel. Unahama na namba yako kama ilivyo. Kama ulikuwa na namba ya Tigo na inaanzia na 071 ukienda Voda itaendelea kuanza na hizo hizo 017. Faida yake ni kuwa kuna watu wenye namba ambazo wamezitumia muda mrefu na wana nia ya kuhama mtandao lakini wanakwamishwa na kubadilisha namba ambayo wanaipenda na imeshazoeleka na watu wake wengi. Hapo wana uwezo wa kuhama na kuendlea kutumia ile ile namba (eg ya Tigo).Hivi karibuni tumesikia kuwa kuna utaratibu wa kuhama mtandao mmoja kwenda mwingine ukitumia Namba ileile, kwa kweli mimi binafsi sijui sababu za msingi za kuhamia mtandao mwingine,
Ninawaomba sana wahusika wa TCRA waelezee umma faida za huo utaratibu na hasara zake. Je endapo nimeridhika na utaratibu wa kumiliki namba tofauti za mitandao tofauti (nikibaki na utaratibu niliozoea) je nitaathirika kwa kiasi gani? Utaratibu huu una lengo gani na una faida gani kwa mtumiaji au serikali? Namba wakati mwingine huwa zinafanana na hutofautishwa na aina ya mtandao je ikitokea mtu mmoja anatoka mtandao mmoja na kuhamia mwingine ambako kuna mtu anayemiliki namba inayofanana ambayo ilikuwa ikitofautishwa na namba za mwanzo je uhamaji huu hautasababaisha mwingiliano wa mawasiliano?
Mimi binafsi na watu kadhaa niliojaribu kuwauliza wengi hawajui kitu gani kinaendelea. TCRA pamoja na mashirika ya simu hebu tuambieni ni kitu gani hiki?
Kama mpigaji, anayekucall atakupigia kwa tigo, akijua ni tigo mwenzake na kajipanga kwa bando la tigo to tigoMfano una namba yako ina zaidi ya miaka mitano hata saba, ni tigo.
watu wengi wanaifahamu.
Wateja wako wa ndani na nje ya nchi wanaifahamu hiyo namba.
Unaona tigo inakuzingua siku zote uwa unatamani kuhamia mtandao mwingine lakini unachelea kuhama kwakuwa watu wengi wanaijua hiyo namba na una wateja unahisi unaweza wapoteza kwa kuhama.
So TCRA kwa hii huduma unaweza badilisha hiyo namba ikawa voda au halotel au smart n.k pasipo kubadili hata tarakimu moja itabaki vile vile.
Mfano wake ndiyo huo..
Analiwa kama aliyepgia mtandao mwingine hakuna namnaKama mpigaji, anayekucall atakupigia kwa tigo, akijua ni tigo mwenzake na kajipanga kwa bando la tigo to tigo
Hapo pakoje mkuu!
We will read numbers brother.Analiwa kama aliyepgia mtandao mwingine hakuna namna
It doesn't make any sense for you only! Watanzania tuna vichwa vigumu sana. Ngoja nikueleze kwa mfano: Kuna bwana mmoja anaitwa John. John ana duka la kuuza nguo kwa jumla na rejareja na ana wateja wengi sana. Mara nyingi wateja wake humpigia simu kumuuliza kama ana mzigo mpya na mambo mengine ya biashara. Namba ya simu anayotumia John ni 0714242420 ambayo ni ya mtandao wa Tigo. Mara ghafla Tigo wamepandisha gharama zao. John anataka kuhamia mtandao mwingine wenye unafuu zaidi lakini anaogopa akihama atawapoteza mawasiliano na wateja wake wa simu kwani itabidi asajili namba mpya ambayo wateja wake hawaijui. Na zaidi itabidi aingie gharama ya kuwafahamisha wateja wake wote kuwa amebadilisha namba. Na hamna uhakika kuwa ataweza kuwafahamisha wote. Basi kwa shingo upande anaendelea kubakia kwenye mtandao wa Tigo na kila siku utamsikia analalamika: ''kama sio watu kuzoea hii namba nakuapia ningehamia Voda. Sasa huu utaratibu ulioanzishwa umemwondolea John hilo tatizo. John atakuwa na uwezo wa kuhamia Voda na namba zile zile za Tigo i.e. 0714242420 hivyo wateja wake wataweza kuendelea kumpata hewani.Kama kweli ni hivyo it doesnt make any sense at all
Umedandia treni kwa mbele braza hukujua kwanini nimemjibu hivyo...It doesn't make any sense for you only! Watanzania tuna vichwa vigumu sana. Ngoja nikueleze kwa mfano: Kuna bwana mmoja anaitwa John. John ana duka la kuuza nguo kwa jumla na rejareja na ana wateja wengi sana. Mara nyingi wateja wake humpigia simu kumuuliza kama ana mzigo mpya na mambo mengine ya biashara. Namba ya simu anayotumia John ni 0714242420 ambayo ni ya mtandao wa Tigo. Mara ghafla Tigo wamepandisha gharama zao. John anataka kuhamia mtandao mwingine wenye unafuu zaidi lakini anaogopa akihama atawapoteza mawasiliano na wateja wake wa simu kwani itabidi asajili namba mpya ambayo wateja wake hawaijui. Basi kwa shingo upande anaendelea kubakia kwenye mtandao wa Tigo na kila siku utamsikia analalamika: ''kama sio watu kuzoea hii namba nakuapia ningehamia Voda. Sasa huu utaratibu ulioanzishwa umemwondolea John hilo tatizo. John atakuwa na uwezo wa kuhamia Voda na namba zile zile za Tigo i.e. 0714242420 hivyo wateja wake wataweza kuendelea kumpata hewani.
Ndio maana una kitufe cha quote na reply! Ili watu waelewe unamjibu nani! Jaribu kuvitumia kwani haviko kwa urembo!Umedandia treni kwa mbele braza hukujua kwanini nimemjibu hivyo...
Kasoma comment ya tatu ya hii thread mimi ndiye mtu wa kwanza kuwaelewesha watu hayo uliyoyaandika mimi ndiye mtu wa kwanza kuyaandika kwenye hii thread.
TCRA wamechemka sana. Huo uhamaji wao hauna maana yoyote ingekuwa enzi zile za laini moja angalau tungewaelewa. Waache kutuletea mambo yao ya kitutusa hapa.Hivi karibuni tumesikia kuwa kuna utaratibu wa kuhama mtandao mmoja kwenda mwingine ukitumia Namba ileile, kwa kweli mimi binafsi sijui sababu za msingi za kuhamia mtandao mwingine,
Ninawaomba sana wahusika wa TCRA waelezee umma faida za huo utaratibu na hasara zake. Je endapo nimeridhika na utaratibu wa kumiliki namba tofauti za mitandao tofauti (nikibaki na utaratibu niliozoea) je nitaathirika kwa kiasi gani? Utaratibu huu una lengo gani na una faida gani kwa mtumiaji au serikali? Namba wakati mwingine huwa zinafanana na hutofautishwa na aina ya mtandao je ikitokea mtu mmoja anatoka mtandao mmoja na kuhamia mwingine ambako kuna mtu anayemiliki namba inayofanana ambayo ilikuwa ikitofautishwa na namba za mwanzo je uhamaji huu hautasababaisha mwingiliano wa mawasiliano?
Mimi binafsi na watu kadhaa niliojaribu kuwauliza wengi hawajui kitu gani kinaendelea. TCRA pamoja na mashirika ya simu hebu tuambieni ni kitu gani hiki?
Mkuu itakuwa huoni vizuri...Ndio maana una kitufe cha quote na reply! Ili watu waelewe unamjibu nani! Jaribu kuvitumia kwani haviko kwa urembo!
Mimi ni makini na usiniletee janja ya nyani! UMEKUBALIANA nae ndio maana ukasema hivyo... it doesnt make any sense.Mkuu itakuwa huoni vizuri...
Umeni quote quote niliyokuwa namjibu mtui.
Na nimemquote.
Narudia tena bado unadandia treni kwa mbele braza...