Mdadamwema.
Senior Member
- Aug 7, 2014
- 150
- 169
Wakuu heshima kwenu,
Naombeni mnisaidie huyu konda amenidhalilisha sn,mimi ni jinsia KE, nilikuwa natoka kawe naelekra External Mabibo nilikuwa nimepanda daladala ya Kawe to Segerea,,nilikuwa na tiketi yangu mkononi ambayo nimeilipia sh 800 kwa sababu ilinibidi nizunguke na gari kutokana na wingi wa watu waliokuwepo pale Kawe wakielekea Segerea.
Mimi nilienda kupandia kituo cha nyuma ili nizunguke nalo gari kwa ajili ya kupata siti,sasa nimefika external nikawa nashuka huyo konda alikuwa pale mlangoni akaanza kunidai pesa ya nauli
Nikamwambia nimeshakulipa nikawa namwonyesha ticketi hataki hata kuishika yeye anataka pesa akanisukuma nikadondosha chupa yangu ya maji niliyokuwa nimeishika mkononi nikainama kuichukua,nilipoinuka akasema hiyo tiketi nimeikota chini yeye haitambui.
Watu wakajaribu kumwelewesha lakini hakuwasiklizana ikumbukwe kwamba ilikuwa ni giza kwenye saa tatu usiku hapakuwa na namna ya kuokota tiketi chini na giza,basi akanitukana matusi ya nguoni makubwa pale standi kisha akaingia ndani ya gari akaondoka zake.
Nimebaki na ticket yangu mimi kesho nataka nikamripoti kituo cha polisi kwa kunidhalilisha na kunisukuma na kunitukana matusi ya nguoni bila sababu au nitakuwa nimechelewa kwa kesho, ilitakiwa niende muda huo huo?
Mimi sijawahi kwenda polisi ila nataka niende kwa mara ya kwanza walahi ameniudhi sn,simwachi huyu.
Naombeni mnisaidie huyu konda amenidhalilisha sn,mimi ni jinsia KE, nilikuwa natoka kawe naelekra External Mabibo nilikuwa nimepanda daladala ya Kawe to Segerea,,nilikuwa na tiketi yangu mkononi ambayo nimeilipia sh 800 kwa sababu ilinibidi nizunguke na gari kutokana na wingi wa watu waliokuwepo pale Kawe wakielekea Segerea.
Mimi nilienda kupandia kituo cha nyuma ili nizunguke nalo gari kwa ajili ya kupata siti,sasa nimefika external nikawa nashuka huyo konda alikuwa pale mlangoni akaanza kunidai pesa ya nauli
Nikamwambia nimeshakulipa nikawa namwonyesha ticketi hataki hata kuishika yeye anataka pesa akanisukuma nikadondosha chupa yangu ya maji niliyokuwa nimeishika mkononi nikainama kuichukua,nilipoinuka akasema hiyo tiketi nimeikota chini yeye haitambui.
Watu wakajaribu kumwelewesha lakini hakuwasiklizana ikumbukwe kwamba ilikuwa ni giza kwenye saa tatu usiku hapakuwa na namna ya kuokota tiketi chini na giza,basi akanitukana matusi ya nguoni makubwa pale standi kisha akaingia ndani ya gari akaondoka zake.
Nimebaki na ticket yangu mimi kesho nataka nikamripoti kituo cha polisi kwa kunidhalilisha na kunisukuma na kunitukana matusi ya nguoni bila sababu au nitakuwa nimechelewa kwa kesho, ilitakiwa niende muda huo huo?
Mimi sijawahi kwenda polisi ila nataka niende kwa mara ya kwanza walahi ameniudhi sn,simwachi huyu.