KERO: Makonda kujisahaulisha kurudisha chenji kwa abiria

Bujoro

JF-Expert Member
Jan 30, 2018
3,046
2,131
Ndugu zangu Makonda acheni tabia hii ni mbaya sana yaani haifai.

Ndugu zangu wana JF, sitaki kuwachosha sana,

mimi nachukia sana hii tabia mbaya ya ndugu zetu makondakta ya kujisahaulisha kurudisha au kutoa chenji kwa abiria wanapopewa hela kubwa na abiria mfano elf 2 au 5 hata 10 wanakuwa wazito sana kumpa chenji abiria.

Hivi wanafanya makusudi ili usahau ile kwako na iwe faida kwao au inakuwaje hasa? Kwanini yeye sio rahisi kukusahau kama hujalipa nauli ila ukitoa hera kubwa ndio akusahau.

Hivi mnajua watanzania sasa hivi hali sio nzuri sana wanawaza sana mda mwingi tunastres kwa kitendo cha kuchelewa kunipa chenji yangu unanifanya nisahau na kushuka bila kunipa chenji yangu na kuniongezea stress zaidi.

Acheni tabia hii unakuta mtu ndo unayo hiyo hiyo sasa uonapoisahau kwa kondakta roho inauma sana sana na tunaharibiana bajeti.

Je wewe umeshawahi sahau chenji kwa daladala au bado na ulijiskiaje uliumia au ni mimi tu nanaeumia pekee yangu.Au ndo yale yale ya vita vya panzi ni furaha ya kunguru au kufa kufaana.

Tiririka hapa.
 
Hahahaha Umenikumbusha Daladala Za Kishiri Buhongwa Ile Alfajiri Wengi Wa Abiria Wanawahi Mabasi Ya Kwenda Mikoani Ole Wako Utoe 10000 Konda Anakwambia Ngoja Nikatafute Chenji Hapo Ndiyo Imetoka Hivyo
 
Hahahaha Umenikumbusha Daladala Za Kishiri Buhongwa Ile Alfajiri Wengi Wa Abiria Wanawahi Mabasi Ya Kwenda Mikoani Ole Wako Utoe 10000 Konda Anakwambia Ngoja Nikatafute Chenji Hapo Ndiyo Imetoka Hivyo
Hahahaha ndo zao hizo we akili yako yote iko kwwny kuwahi mabasi au unakoenda yy ndo fursa yake jmn
 
Mkuu ushaulifu wako ni wa kiwango cha juu zama hizi ni za kusahau chenji ya elf tano au kumi kwel kwa konda?
Wewe acha kusema hivo ushawahi kuchelewa unakoenda harafu ukatoa hera kubwa ukaona kama utakumbuka kama we haijawahi kukutokea ipo siku utanikumbuka.
 
Back
Top Bottom