Kenyatta anaichana live Tanzania now cheki Citizen

Hiyo EAC itajengwa bila kushirikisha wenye nchi ambao ndiyo mnataka kuwaendeleza au ni utashi wa biashara?
kama ni biashara kenya siyo mmbiya mzuri wa biashara kwani mara kadhaa imekwisha wakatia wenzake access na kuna wakati huyo huyo museveni alifikiria kuachana kabisa na kenya.
Umoja wowote ule unapaswa kujengwa kwa kuaminiana na wote kuwa na dira na muelekeo mmoja na siyo mwanachama mmoja kujifanya kuwa yeye ndiye kiongozi na wengine wafuate nyayo.
Vipi, mbona unamshambulia mwekezaji mgeni namba moja Tanzania mbele ya South Africa na UK!
 
Anasema ni siasa za upuuzi nchi nyingine kusema kuwa wanaachwa kwenye ujenzi wa reli na kasema mbona wanapangankuunganisha reli kutoka Nairobi hadi Arusha na Moshi. Amesema yeye hawezi kufuatilia siasa za kipuuzo kwani kazi yake ni kuunganisha maendeleo ya Afrika Mashariki.
Kumbe Adam Kimbisa, mbuge wa Afrika Mashariki, alivyomwambia UK jana (?) eti "tulikuwa nawe, tuko nawe na tutakuwa nawe" kuhusiana na ile kesi ya UK the Hague alikuwa anajikomba??????
 
Siajelewa.

1. Ameichana Tanzania? Tanzania ni karatasi?

2. Kwa hiyo sasa hivi Tanzania ni vipande vipande? Asa mi niko kipande gani saa hii?

3. Ameichana kwenye TV? Asa hiyo TV inaukubwa gani? Kwamba kaiingiza Tanzania humo afu akaichana chana?

4. Nani alimsaidia kuichana? Kaichana kwa Panga? Ama mkasi? Au kaipiga nyundo ndio ikaparaganyika?

5. Mkuu, Weka Picha nipate Taswira tafadhali.
Kweli Akili nyingine ni za Kitembele, tembele.
 
Ngojea tumuundie huyu Kenyatta kamati ya uchunguzi ili ije itoe muongozo wa sera za namna ya kumjibu huyu!
Atajengaje reli bila kwanza kukaa na kujadiliana ili iundwe tume kwa ajili ya kuchunguza mapendekezo hayo ya reli halafu ya jadiliwa na kamati ya maendeleo ya EAC ili itengeneze sera na taratibu za ukamilishaji wa zoezi hilo???

Hehehe!
 
...hana lolote huyo, hayo ni maneno ya kutapatapa na kuficha mpango wao na wenzake, yeye analetaje maendeleo ya East Africa kwa kuwa ndumilakuwili?, tatizo anakurupuka wakati nchi yake bado itahitaji kutetewa na jumuiya siku za usoni maana mpaka sasa mwelekeo wake tunaujua, Kenya haina safari ndefu kisiasa na kimaisha ya wananchi, kuibeza Tanzania ni sawa na kuzidi kufupisha maisha ya nchi yao ambayo itaanguka ghafla. huo ni uchambuzi mdogo tu wa hili jambo niaonavyo mimi. maana kuna moto unaoendelea kuwaka chini chini na wananchi wa kenya bado wana dukuduku ambalo siku likilipuka...
....bila kuficha hata hii kitu Tz ipo, ila kwa wakenya wanabomoa mpaka nguzo za kuegamia nikimaanisha migogoro wanayoipanda sasa siku ikija kuiva au kukomaana itahitaji mataifa ya nje kuingilia kati, moja wapo ikiwa ni Tanzania ambayo ndo itakuwa nchi yenye ujirani wa kweli na kenya maana zinaingiliana mambo mengi kuliko hata Rwanda, Sudan na e.t.c

Ndugu zangu acheni jazba kwa maneno yasiyo yakini. Mleta mada anawaingiza mtegoni nanyi mwaingia kichwakichwa bila kujiuliza wala kutafakari. Ni busara kutoa mchango panapo mada dhahiri kuliko kutumia nguvu nyingi kwa swala lisilo thibitika. Baadhi ya waleta mada wana ajenda zao. Kama mada haijitoshelezi sion haja ya kuchangia. Ahsanteni ndugu zangu kwa kuwa wavumilivu.
 
sisi tumelala wacha atuchambue kabisa
tunalia lia kutaka jumuia isivunjike wakati hatujitambui
wenzetu kenya wanafundishwa kujitambua sisi tumefundishwa kukariri wapi na wapi
nenda hata restaurant wahudumu hawana haraka hawakuchangamkii wamekaa kaa tu
nenda maofisini mtu anakunywa chai saa nzima kisha mchana lunch saa nzima hatuwezi kushindana na kenya
ukiwa ofisini unachapa kazi na wako creative sana katika kazi na biashara
tumebaki tunaimba kidumu chama, au Zito mara chadema hatujishughulishi kutafuta suluhu la umaskini
hicho chama kitadumu hata makaburini labda,,shame on us
 
Ngojea tumuundie huyu Kenyatta kamati ya uchunguzi ili ije itoe muongozo wa sera za namna ya kumjibu huyu!
Atajengaje reli bila kwanza kukaa na kujadiliana ili iundwe tume kwa ajili ya kuchunguza mapendekezo hayo ya reli halafu ya jadiliwa na kamati ya maendeleo ya EAC ili itengeneze sera na taratibu za ukamilishaji wa zoezi hilo???

Hehehe!
Mkuu upo sahihi !
Wameruka steji nyingi sana.
Kwanza ilitakiwa pawe na hoja. Halafu hoja ijadiliwe na bunge, halafu bunge liunde kamati kufanya upembuzi ili hatimaye waje na sera madhubuti itakayowasilishwa serikalini kwa ajili ya kufanyiwa feasibility study kabla ya kurudishwa kwa wapiga kura ili hatimaye mazungumzo rasmi yaanze
 
Ujenzi wa reli kutoa ajira zaidi ya elfu 30. Ndio mradi mkubwa kulioko yote EA.
 
Kumbe Adam Kimbisa, mbuge wa Afrika Mashariki, alivyomwambia UK jana (?) eti "tulikuwa nawe, tuko nawe na tutakuwa nawe" kuhusiana na ile kesi ya UK the Hague alikuwa anajikomba??????
Tena aliniboa sana yule mzee....yaani kule ni kujikomba kwa kishamba tena kwa mtu naekuonesha madharau dailly... bora angekaa kimya aonekane ----...
 
Kumbe Adam Kimbisa, mbuge wa Afrika Mashariki, alivyomwambia UK jana (?) eti "tulikuwa nawe, tuko nawe na tutakuwa nawe" kuhusiana na ile kesi ya UK the Hague alikuwa anajikomba??????

Mie ilinisikitisha sana.
Ndio maana hasa tunaonekana Cheap.
Sera za nje kiuchumi hatuna kabisa.
Bora Sitta alielekea DRC.
 
Kumbe Adam Kimbisa, mbuge wa Afrika Mashariki, alivyomwambia UK jana (?) eti "tulikuwa nawe, tuko nawe na tutakuwa nawe" kuhusiana na ile kesi ya UK the Hague alikuwa anajikomba??????
kule the hague haendi tena atawakilishwa na wakili.
 
Back
Top Bottom