Kenyatta anaichana live Tanzania now cheki Citizen

kiparah

JF-Expert Member
Sep 7, 2010
1,173
114
Wakati akizindua ujenzi wa reli kutoka Mombasa through Kigali, Kampala to Juba.
Anasema ni siasa za upuuzi nchi nyingine kusema kuwa wanaachwa kwenye ujenzi wa reli na kasema mbona wanapanga kuunganisha reli kutoka Nairobi hadi Arusha na Moshi.

Amesema yeye hawezi kufuatilia siasa za kipuuzi kwani kazi yake ni kuunganisha maendeleo ya Afrika Mashariki.
 
Hebu weka anachoongea mkuu,sio wote tuna access ya kuona hiyo channel, kasemaje?
 
Anasema ni siasa za upuuzi nchi nyingine kusema kuwa wanaachwa kwenye ujenzi wa reli na kasema mbona wanapangankuunganisha reli kutoka Nairobi hadi Arusha na Moshi.

Amesema yeye hawezi kufuatilia siasa za kipuuzo kwani kazi yake ni kuunganisha maendeleo ya Afrika Mashariki.
 
Wakati wa siasa umekwisha tufanye kazi kujenga kenya na EAC by Kenyatta

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Wakati wa siasa umekwisha tufanye kazi kujenga kenya na EAC by Kenyatta

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
Hiyo EAC itajengwa bila kushirikisha wenye nchi ambao ndiyo mnataka kuwaendeleza au ni utashi wa biashara?
kama ni biashara kenya siyo mmbiya mzuri wa biashara kwani mara kadhaa imekwisha wakatia wenzake access na kuna wakati huyo huyo museveni alifikiria kuachana kabisa na kenya.
Umoja wowote ule unapaswa kujengwa kwa kuaminiana na wote kuwa na dira na muelekeo mmoja na siyo mwanachama mmoja kujifanya kuwa yeye ndiye kiongozi na wengine wafuate nyayo.
 
Anasema ni siasa za upuuzi nchi nyingine kusema kuwa wanaachwa kwenye ujenzi wa reli na kasema mbona wanapangankuunganisha reli kutoka Nairobi hadi Arusha na Moshi. Amesema yeye hawezi kufuatilia siasa za kipuuzo kwani kazi yake ni kuunganisha maendeleo ya Afrika Mashariki.

Sasa hapo amichana Tanzania vipi, bana acha uzushi, ujenzi wa reli tokea Mombasa hadi Kigali na Sudan Kusini na nyingine tokea Nairobi hadi Arusha na Moshi ni jambo muhimu sana katika kanda ya EA.
 
...hana lolote huyo, hayo ni maneno ya kutapatapa na kuficha mpango wao na wenzake, yeye analetaje maendeleo ya East Africa kwa kuwa ndumilakuwili?, tatizo anakurupuka wakati nchi yake bado itahitaji kutetewa na jumuiya siku za usoni maana mpaka sasa mwelekeo wake tunaujua, Kenya haina safari ndefu kisiasa na kimaisha ya wananchi, kuibeza Tanzania ni sawa na kuzidi kufupisha maisha ya nchi yao ambayo itaanguka ghafla. huo ni uchambuzi mdogo tu wa hili jambo niaonavyo mimi. maana kuna moto unaoendelea kuwaka chini chini na wananchi wa kenya bado wana dukuduku ambalo siku likilipuka...
....bila kuficha hata hii kitu Tz ipo, ila kwa wakenya wanabomoa mpaka nguzo za kuegamia nikimaanisha migogoro wanayoipanda sasa siku ikija kuiva au kukomaana itahitaji mataifa ya nje kuingilia kati, moja wapo ikiwa ni Tanzania ambayo ndo itakuwa nchi yenye ujirani wa kweli na kenya maana zinaingiliana mambo mengi kuliko hata Rwanda, Sudan na e.t.c
 
Haswa...!!
Wakati Kenya, Uganda, Rwanda na South Sudan zinajenga reli za kisasa kabisa, Wa-Tanzania wako busy kujenga hoja kwenye swala la Zitto Kabwe.
Serikali nzima inatumia muda wake wote na vyombo vya habari vyake vyote 'kumjenga' Zitto.

we unatakaje yaaan....!!!au ulitakaje ulitaka wote tufunge safari kwenda kenya
 
Siajelewa.

1. Ameichana Tanzania? Tanzania ni karatasi?

2. Kwa hiyo sasa hivi Tanzania ni vipande vipande? Asa mi niko kipande gani saa hii?

3. Ameichana kwenye TV? Asa hiyo TV inaukubwa gani? Kwamba kaiingiza Tanzania humo afu akaichana chana?

4. Nani alimsaidia kuichana? Kaichana kwa Panga? Ama mkasi? Au kaipiga nyundo ndio ikaparaganyika?

5. Mkuu, Weka Picha nipate Taswira tafadhali.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom