kenyans and their mistrusted hypocritical behavior

papa jones hataki ujinga.
IMG_20190112_132134.jpeg
 
bila shaka mnakumbuka tukio la baraza la sanaa nchini tanzania(basata) kufungia wimbo wa nyegezi ulioimbwa na mwanamziki rayvanny ft diamond platnumz.

basata imewapiga marufuku diamond platnumz na rayvanny kutoimba wimbo wa nyegezi mahali popote pale wanapo tumbuiza kutokana mashahiri yake kutozingatia maadili.

baada ya siku chache, mamlaka ya kenya inayohusika na ku control maudhui ya kazi za sanaa ikatoa tamko la kuutambua wimbo huo na kudai kwamba mashahiri yake hayana shida yoyote.

kwa maana hiyo diamond platnumz na rayvanny wapo huru kuuimba kwenye majukwaa ya kenya kama walivofanya hivi karibuni kwenye tamasha lao sikukuu za mwisho wa mwaka.

jana mwanamziki wa kenya khaligraph jones ambaye binafsi huwa nakubali sana ngoma zake, alipost video fupi kwenye ukurasa wake wa instagram ikimuonyesha akimuimbia mtangazaji wa tv betty kyallo mashairi ya wimbo wake wa "nataka kukupiga miti".

wakenya walewale waliodai wimbo wa nyegezi hauna shida yoyote, wame react kwa hasira kumlaumu khaligraph jones kwamba mashahiri ya wimbo wake wa "nataka kukupiga miti" hayana maadili.
kwa kweli huu ni unafiki wa hali ya juu sana.

tafadhali wakenya, mwacheni khaligraph jones afanye kazi yake. mkiendelea kumsumbua, tutamshawi ahamie tanzania.
huwa hatushwindwi kitu.

na kwa kuonyesha jeuri, tutamkabidhi 100 hectares of land for free ili afanye investment yoyote ile atakayojisikia.

tunajua moja ya kero kubwa miongoni mwa wakenya ni ukosefu wa ardhi kutokana na ardhi kubwa kunyakuliwa na wanasiasa na wafanyabiashara wachache.
View attachment 991903View attachment 991904

Hiyo kitu ni simple Sana, msamiati miengine na maneno mengine Yana nguvu zaidi kuliko maneno mengine kulingana na jamii .... Kwa mfano mtoto wa dadngu hutumia neno 'makalio' Kwa sentensi, hatamaliza siku kabla aingize Neno makalio Kwa sentensi na hakuna mtu hua anashida naye, lakini pale anapojisahau na kusema 'matako' anakanywa mbio mbio na kuambiwa asitumie Hilo Neno....
Vile vile hio nyimbo ya nyege ya diamond, yanayosemwa hayana nguvu huku tofauti na huko Tanzania , lakini hio nyimbo ya khaligraph inasumbua watu zaidi kwavile anaimbia huyo mwanahabari Betty kyalo na mistari explicit.....
And speaking of Nyege, nakumbuka kuna wakati flani Gavana wa Nairobi aki piga kampeni ya kupigana Kura alimtukana Ester passaris Kwa kudai ana Nyege nyingi Hadi akipewa cheo atabaki akizunguka akitafuta wanaume ---- Na hayo maneno yalionyeshwa Kwa habari za jioni!!!!!!

Ni kama vile mtu akutukane kum@mako na mwengine akutukane motherfucker .... Yote yanamaanisha kitu kimoja lakini Hilo la Kiswahili Lina nguvu zaidi kwasababu ya kule tunakoishi...
 
Back
Top Bottom