Kenyan Elections 2007: End Of An Era (error?)

Kenyan-Tanzanian

JF-Expert Member
Nov 7, 2006
302
2
--------Kenya Yakaribia Kanaan-------


Jamvi la kihistoria la mabepari wa kibaada-ukoloni nchini Kenya sasa ni bayana litajifunga mwishoni mwa mwaka huu. Hali hi ya kihistoria ambaye itaona mamlaka ikihamishwa toka katikati ya nchi hadi mashinani kwa namna mbalimbali (devolution of power) imetokana na kule kukubalika kwa chama cha ODM na mgombeakiti cha urais, Raila Odinga - mwanawe muanzilishi wa siasa za upinzani nchini Kenya, Marehemu Mzee Jaramogi Oginga Odinga.

Raila ambaye alikuwa kizingiti muhimu katika ile manwari (muungano wa vyama) ya kisiasa NARC iliyomng'oa Rais Mstaafu Moi mamlakani 2002 sasa anazidi kuvuma kama Musa ambaye waKenya waliowengi walidhani yupo ndani ya Rais Kibaki ila kwa maoni yao hawajaiona Kanani yake hadi wasasa. Mwaka wa 2005, baada ya Katiba Mpya iliyoonekana kuwa itazidikuzikita mizizi za mabepari waKenya na wameoziteka asasi za serekali kati (yaani centralized government)kupingwa vikali na wanachi waKenya wakiongozwa na Raila Odinga, Kibaki aliwatimua Raila na wenzake wengi tuu licha ya wao kumsaidia Kibaki mwenyewe kuingia ikulu japokuwa alikuwa kalazwa London baada ya ajali iliyotokea akiwa kwenye kampeni (2002).

Hivi leo, kila kuchao, kura za maoni, akina mama na maseela mitaani, wakongwe na watoto vitongojini kote nchini wanakubali kwamba Serekali ya ODM (Raila na wenzake waliotimuliwa na Kibaki)sio siri au ndoto tena ila wazo nyeti ambalo wakti wake umewadia. Uvumilivu umefika tamati. Mbegu ya fikra ya kisiasa iliyopandwa na waIngereza, ikapaliliwa na Serekali ya awamu ya kwanza ya Kenyatta pamoja na zile zilizofwata za Moi na Kibaki (sasa wanamlea mwanawe Kenyatta aiitwayo Uhuru pengine ariidhi Kibaki), mbegu hiyo imepanda mti wa sintofahamu nchini ambayo ni lazima ikatwe.

Nayo ile mbegu ya fikra ya kisiasa ya makamu wa Rais wa kwanza nchini chini ya Kenyatta yaani babke Raila aliyeitwa Jaramogi Oginga Odinga kumbe iliota hata ndani ya miiba. Sasa imewadia wakati ambayo mti huo wa kwanza wa siasa yaani ule wa Kenyatta ni lazima ukatwe ili ule mwingine yaani wa Jaramogi umee. WaKenya wanasema hapana Kibaki asiendelee kwasababu wako tayari kujaribu matunda ya uhuru yanayomea kwa mti tofuati wa kisiasa.

By voting for Raila and by proxy Jaramogi (posthumously)Kenyans will be symbolically saying to the Kibaki-Moi-Kenyatta clan a collective:

"No to our centralized government structure that has only favoured central province, central government officials, central towns, central capital, central human capital, central education and other institutions, central literature, central anticolonial history, central intellectuals, central judiciary, executive and legislative arms of governance and all that have made an unjust centre to hold for four decades and yes to decentralization in all its forms, major and minor (from politics to literature)".


Hivi ndio maana najiunga na wananchi wenzangu watokao maeneo ambayoyamekuwa pembeni mwa ulaji wa keki ya kitaifa kubashiri kuwadia kwa serekali ya awamu ya nne yenye ari, kazi, nguvu mpya na hata mawazo mapya ya uongozi nchini. Karibuni ODM. Tawaleni Kenya.

Hizi hapa picha mbali mbali zinazotuweka hai ndani ya bahari hili la homa ya kisiasa au ukipenda "Election Fever".

1. http://www.youtube.com/watch?v=wz3pXskASz4
2. http://www.youtube.com/watch?v=tpZhJaJVbMI
3. http://www.youtube.com/watch?v=dlusA1FcjtY
4. http://www.youtube.com/watch?v=OjmGlaUJbKk
5. http://www.youtube.com/watch?v=MSQ4ec_Lc78
6. http://www.youtube.com/watch?v=HLm6vPCM61U

PS: Ingawaje siasa za Kenya zimefananishwa na mawimbi ya bahari yaani zinaweza badilika wakati wowote ule na kupuliza upande tofauti na ule wa awali, hatakiwi mtu kuwa na akili za Albert Einstein kubashiri ni upande upe kati ya ODM (RAILA) na PNU (KIBAKI) utaingia Ikulu ya Nairobi, Januari 2008. Jameni tumpatieni Raila sikio ilituweze kupiga kura yenye hisia na fikra pia. Hii hapa tovuti ya huyu Shujaa wa Afrika ya Karne 21. www.raila2007.com

ODM! MAISHA BORA KWA WAKENYA WOTE (CCM! MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA)
 
Back
Top Bottom