Kenya Yaipongeza Sana Tanzania

pamoja na Mkapa kuwepo huko kwenu kusaidia muafaka, akirudi huku na yeye tunaye tu. Ni fisadi aliyekubuhu. Tunamsubiri kwa hamu sana ili atueleze alichotuibia kwa miaka 10, halafu arudishe. Otherwise Ukonga panamsubiri ili akatoe taarifa ya machafuko ya Kenya kwa wafungwa kule.

Nafikiri Moto Lazima Umuungunguze huyu Mkapa. Ikiwa pamoja na Karamagi na Lowassa kuachia madaraka lakini umeme tunalipa gharama kubwa sana. Tuna uhakika wananchi kuwa tunawekeza katika miradi mbali mbali ya karamagi na Lowassa.

Kama bunge halitatoa adhabu kali ya kuturudishia gharama zetu, mapendekezo ni kufanya yaliyofanyika kwa Balali. Wananchi watajigawia mali zao, potelea mbali kila mtu akipata gurudumu, mitambo ya kunyanyulia mizigo(hata watano watagawana), nk.

Tutajilipa tu. Kwa hiyo K-T kazi bado ndo inaanza lazima mnyonge apate haki yake kabisa. Lazima wananchi wapate fidia, na bado nafikiri IPTL(tujue ni nani anafaidi), Netgroup(wameisha kimbia lakini tutataka kujua nani walifaidi na wana nini), Songas(Nilishawahi kukutana na mtaalamu wa Maswala ya Umeme Zimbabwe-(si Mtanzania) akasema hapa kuna Rushwa nzuri tu). Swali Kiwira ni akina nani? (Simple-Mkapa).
 
Angloleasing ilikuwa kashfa inayofanana na sana na hii ya benki kuu. Hata hivyo, wenzetu walifanikiwa kurudisha mapesa yao yaliyoibiwa. Nafikiri hii ya kupongezana ingekuja baada ya kurecover fedha yetu. kama mbunge fulani alivyosema bungeni, kama waziri anaiba mabilioni halafu anajiuulu, wewe mwananchi una kitu gani cha kushangilia ?
 
I propose tumpe huyu jamaa EXCEPTIONAL LEAVE TO REMAIN IN TANZANIA

KISHA BAADAE TUTANGALIA KAMA TUNAWEZA KUMPA INDEFINITE LEAVE TO REMAIN
 
Nitashukuru sana hili likifanyika. Naipenda Tanzania na sio tu kiubinafsi ila nikipewa Greencard ya USA au Bongo watasema watakaosema ila mimi Bongo tuu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom