Kenya Yaipongeza Sana Tanzania

Kenyan-Tanzanian

JF-Expert Member
Nov 7, 2006
302
2
Naomba nafasi ili niwapongezeni Watanzania wote popote mulipo duniani.

1. Hongera kwa kuweza kutuonyesha ukomavu wa siasa zenu baada ya presha ya wananchi kumtimua Lowassa na wengineo waliohusika kwenye the Richmond Scandal.

2. Kwa Rais wenu stadi Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuteuliwa kama the first East African president of the African Union.

3. Wakati sisi huku kenya tunazidi kuzorota nyie mnatuonyesha njia.

Kifupi: I am proud of Tanzania!
 
Naomba nafasi ili niwapongezeni Watanzania wote popote mulipo duniani.

1. Hongera kwa kuweza kutuonyesha ukomavu wa siasa zenu baada ya presha ya wananchi kumtimua Lowassa na wengineo waliohusika kwenye the Richmond Scandal.

2. Kwa Rais wenu stadi Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuteuliwa kama the first East African president of the African Union.

3. Wakati sisi huku kenya tunazidi kuzorota nyie mnatuonyesha njia.

Kifupi: I am proud of Tanzania!

KT.

Tuna matatizo yetu ya kutosha... lakini kwa uongozi na utawala at least sio wabaya sana kulinganisha na nchi nyingi Afrika.

Binafsi kumwona Lowassa anatoka, Mwenzake anaingia hakuna kinyongo wanapongezana that was what we needed.
 
KT,

Poa tu ndugu! Je haujambo?

Ndo tunasubiri next cabinet- it was a good move for Lowasa kujiuzulu- ni symbol of Utawala bora -sii tu Tz, bali EA na Afrika kwa ujumla!

Je ile scandali ya Angloleasing na Gordenbereg sii pia wako Ministers waliojiuzulu?
 
Naomba nafasi ili niwapongezeni Watanzania wote popote mulipo duniani.

1. Hongera kwa kuweza kutuonyesha ukomavu wa siasa zenu baada ya presha ya wananchi kumtimua Lowassa na wengineo waliohusika kwenye the Richmond Scandal.

2. Kwa Rais wenu stadi Mh. Jakaya Mrisho Kikwete kuteuliwa kama the first East African president of the African Union.

3. Wakati sisi huku kenya tunazidi kuzorota nyie mnatuonyesha njia.

Kifupi: I am proud of Tanzania!

Ndungu KT,
Tunashukuru sana kwa pongezi, ila bado tuna kazi kama tatu za kumalizia kuwakaba koo hawa mafisadi. Bado tunasubiri ripoti ya wizi wa pesa zetu pale benki kuu, na bado tunachunguza mikataba yenye utata ya madini. Tuna kazi ya tatu ya kuhakikisha kwamba wale wote waliokataa kuhojiwa na tume wanachukuliwa hatua kali za kisheria. Huenda panapo majaliwa kila kitu kitakuwa wazi na tutawawajibisha wezi wote.
 
TUNAIPOKEA SANA HII PONGEZI YAKO.

TANZANIA INAONGOZWA NA CHAMA MAKINI CHA CCM AMBACHO KWA MISINGI YAKE IMARA NA ITIKADI YAKE MAKINI IMETUFIKISHA HAPA.

TUNAWASHUKURU SANA WAASISI WETU MZEE KARUME(RIP) NA MWALIMU NYERERE(RIP) KWA MISINGI MEMA WALIOTUEKEA


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI NA MAPINDUZI DUMU DAIMA
 
KT,

Poa tu ndugu! Je haujambo?

Ndo tunasubiri next cabinet- it was a good move for Lowasa kujiuzulu- ni symbol of Utawala bora -sii tu Tz, bali EA na Afrika kwa ujumla!

Je ile scandali ya Angloleasing na Gordenbereg sii pia wako Ministers waliojiuzulu?

Sina neno Mh Mzalendo.

Tunashkuru Mungu huku Anaani akiendelea na Peace Talks zake hapa Nairobi. Ndani ya wiki hii wengi wanatumaini kutapatikana na way forward ili Kenya iweze jikomboa kutoka kwa hii political mess iliomo ndani sasa. Kwa maoni yangu, pasipo na haki basi amani hata ikiwepo ni amani bandia tu. Ni kama kujalibu na kufunika kidonda sugu na benjeji huku ukisema "eee babu kishapona kidonda!"

Ndio kuna walojiuzulu huku Kenya baada ya presha toka kwa wananchi kuhusu sakata la Goldernberg na Anglo-leasing mwaka jana. Wakiwemo Saitoti na Kiraitu. Aibu isiyo na kifani ni kwamba wawa hawa wapo tena strong sana ndani ya serikali mpya ya bwana Kibaki! Saitoti sasa ni kama kapandishwa mamlaka na ndio Waziri wa Mambo ya Ndani akisimamia idara za polisi, ujasusi na vikosi za askari mbali mbali. Kiraitu ndio waziri wa Energy.

Ni muhimu kkukumbuka kwamba JK amesimama kidete kwenye kutomtambua Kibaki hadi pale zogo litatatuliwa. Inapendeza kwamba ni JK yuyu huyu ambaye sasa amepewa ofisi ya Rais wa AU, shirika ambalo ndilo lilimtuma Anani Kenya asaidie kwenye upatinishi. I am sure, viongozi wengi wa Afrika na hata sisi wananchi tutakubaliana kwamba JK anaweza kujenga image na developement bomba sana Tanzania, East Africa na hata kwenye zogo la Zimbabwe. Ila apunguze udini jamani hii ndio itakuwa weakspot au Achilles Heel yake....

Mungu mbariki Mh. PM Peter Pinda na Mungu ibariki Tanzania.
 
TUNAIPOKEA SANA HII PONGEZI YAKO.

TANZANIA INAONGOZWA NA CHAMA MAKINI CHA CCM AMBACHO KWA MISINGI YAKE IMARA NA ITIKADI YAKE MAKINI IMETUFIKISHA HAPA.

TUNAWASHUKURU SANA WAASISI WETU MZEE KARUME(RIP) NA MWALIMU NYERERE(RIP) KWA MISINGI MEMA WALIOTUEKEA


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI NA MAPINDUZI DUMU DAIMA

KT
Mimi ni CCM mzuri sana tangia mwaka TANU na sasa CCM lakini kwa hili nawapongeza Watanzania na Upinzani Bungeni , nawapongeza Mwana Halisi , Jambo Forums wote kabisa wakiwemo wachovu wachache wa CCM ambao huweka CCM mbele kila mahali na magazeti imara ambayo hayakutishika sana na vitisho . Hapa siwapo hongera CCM hapana .
 
KT
Mimi ni CCM mzuri sana tangia mwaka TANU na sasa CCM lakini kwa hili nawapongeza Watanzania na Upinzani Bungeni , nawapongeza Mwana Halisi , Jambo Forums wote kabisa wakiwemo wachovu wachache wa CCM ambao huweka CCM mbele kila mahali na magazeti imara ambayo hayakutishika sana na vitisho . Hapa siwapo hongera CCM hapana .

????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????
 
Naomba nafasi ili niwapongezeni Watanzania wote popote mulipo duniani.

1. Hongera kwa kuweza kutuonyesha ukomavu wa siasa zenu baada ya presha ya wananchi kumtimua Lowassa na wengineo waliohusika kwenye the Richmond Scandal.


Kifupi: I am proud of Tanzania!
Zaidi mnaweza kujifunza mengi kupitia muafaka wa CCM na CUF....
 
..kt,

..uzuri wa tz ni kutokuwa warahisi kutatua "matatizo" kwa kuua!

..kenya maslahi ya mtu yanapokuwa hatarini,wazo la kwanza huwa ni kutafuta maadui na kuua!

..sasa,kuua si kutatua "matatizo" bali ni kutafuta laana zaidi,kwani "damu ya mtu nzito".

..wakenya wanahitaji kuvumiliana,kuheshimiana na kutunziana utu.
 
Nipokee pongezi hizi toka nchi ya jirani kwa mtizamo tofauti.

Nazipokea kwa kuwapelekea salamu mafisadi sugu waliobaki hapo nyumbani Tz kuwa . ...wakiona Lowasa amenyolewa..nao waoshe vichwa vyao kwa maji mengi, kwani karibu wanafikiwa na zamu zao haziko mabali!

Mafsadi sugu wa tanzania fanyeni kitu kimoja kabla mambo hayajawa mabaya....come foward and honestly apologise publicaly msiogope hatutawaumiza..we will understand you, kama mkifanya kuomba msamaha na kutubu kweli!!

Mkikosa media ..sahihi Karibuni JF. Lakini kama mkifanya mzaha mkachelewa kupokea nafasi...You know what happended To EL , mliona moto ukimshukia pale bungeni bila simile mbele ya umati wa Tv dunia nzima, mliona mkewe akitoamachozi..Niwaambie tu kuwa hamtabakia salama,..I tell you it willnt be easy for you!

Mkiona nchi za jirani wameanza kuona jambo kama hili na kulipa uzito satahii..Mjue kuwa there is no way out for you!! Hata Mwai Kibaki..na wenzie wameanza kutuelewa Wt katika sura za kazi na style yetu!!Mungu ibariki tz.
 
Mkiona nchi za jirani wameanza kuona jambo kama hili na kulipa uzito satahii..Mjue kuwa there is no way out for you!! Hata Mwai Kibaki..na wenzie wameanza kutuelewa Wt katika sura za kazi na style yetu!!Mungu ibariki tz.

Ndugu yetu KT,
Kwanza tunafurahi kusikia sauti yako na kwamba ungali hai baada ya balaa lililotokea nchini mwako.Nawatakieni amani na haki katika mazungumzo yanayoendelea nchini. Kwa hili la mafisadi hata sisi tumefurahi kuona mafisadi wanafikishwa hatiani. Hii ni hatua ya mwanzo tu. Hatutapumzika mpaka mafisadi wote watimuliwe kwenye ngazi za uongozi wa nchi na wachukuliwe hatua zinazohitajika.
 
TUNAIPOKEA SANA HII PONGEZI YAKO.

TANZANIA INAONGOZWA NA CHAMA MAKINI CHA CCM AMBACHO KWA MISINGI YAKE IMARA NA ITIKADI YAKE MAKINI IMETUFIKISHA HAPA.

TUNAWASHUKURU SANA WAASISI WETU MZEE KARUME(RIP) NA MWALIMU NYERERE(RIP) KWA MISINGI MEMA WALIOTUEKEA


KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI NA MAPINDUZI DUMU DAIMA

Imetufikisha wapi? IPTL, NETGROUP, TANZANIA GREEN COMPANY, CITY WATER, NBC, KIWIRA....?[/COLOR. Let's be serious.
 
Mkuu,
Mwafaka gani unaouongelea?
Ni huu ambao hauishi ama kuna mwingine?

..kt,

..uzuri wa tz ni kutokuwa warahisi kutatua "matatizo" kwa kuua!

..kenya maslahi ya mtu yanapokuwa hatarini,wazo la kwanza huwa ni kutafuta maadui na kuua!

..sasa,kuua si kutatua "matatizo" bali ni kutafuta laana zaidi,kwani "damu ya mtu nzito".

..wakenya wanahitaji kuvumiliana,kuheshimiana na kutunziana utu.[/QUOTE]


Mkuu IDIMI,
Soma mstari wa mwisho wa DAR si LAMU, nadhani unatoa jibu zuri sana.
 
pamoja na Mkapa kuwepo huko kwenu kusaidia muafaka, akirudi huku na yeye tunaye tu. Ni fisadi aliyekubuhu. Tunamsubiri kwa hamu sana ili atueleze alichotuibia kwa miaka 10, halafu arudishe. Otherwise Ukonga panamsubiri ili akatoe taarifa ya machafuko ya Kenya kwa wafungwa kule.
 
Back
Top Bottom