MOTOCHINI
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 27,574
- 29,959
WATU wanne wamefariki, 11 wamejeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakitumia kusafiri kukanyaga kilipuzi saa sita adhuhuri Ijumaa mjini Mandera.
Kamishna wa Kaunti ya Mandera, Fredrick Shisia, amethibitisha tukio hilo la saa sita akisema gari aina ya Toyota Landcruiser lililokuwa limebeba watu 15 kutoka Elwak kwenda mjini Mandera limekanyaga kilipuzi.
“Gari hilo husafirisha abiria na lilikuwa na wasafiri 15 lilipokanyaga kilipuzi hicho," amesema Bw Shisia.
Mwenyekiti wa usalama katika kaunti amesema machifu wawili ni miongoni mwa waliotembelewa na mkasa huo.
Walioumia wamelazwa katika hospitali ya kaunti ndogo ya Lafey.
Bw Shisia amesema eneo hilo ni hatari sana kwa sababu wahalifu wamezidisha makuruhu.
Amesema idara ya usalama inafanya kulihali kuimarisha hali.
Maeneo hatari ni Fino, Lafey na Arabia kwa sababu yako karibu na mpaka.
Mei 2017 msafara wa gavana wa Mandera Ali Roba ulishambuliwa na maafisa wa polisi watano wakauawa.
Hata hivyo Shisia amekataa kuhusisha tukio la leo Ijumaa na lile la msafara wa gavana akisema katika moja lake, Al-Shabaab walikiri kuhusika.
Hajasema ni lipi hasa linahusishwa moja kwa moja na Al-Shabaab.
Kamishna wa Kaunti ya Mandera, Fredrick Shisia, amethibitisha tukio hilo la saa sita akisema gari aina ya Toyota Landcruiser lililokuwa limebeba watu 15 kutoka Elwak kwenda mjini Mandera limekanyaga kilipuzi.
“Gari hilo husafirisha abiria na lilikuwa na wasafiri 15 lilipokanyaga kilipuzi hicho," amesema Bw Shisia.
Mwenyekiti wa usalama katika kaunti amesema machifu wawili ni miongoni mwa waliotembelewa na mkasa huo.
Walioumia wamelazwa katika hospitali ya kaunti ndogo ya Lafey.
Bw Shisia amesema eneo hilo ni hatari sana kwa sababu wahalifu wamezidisha makuruhu.
Amesema idara ya usalama inafanya kulihali kuimarisha hali.
Maeneo hatari ni Fino, Lafey na Arabia kwa sababu yako karibu na mpaka.
Mei 2017 msafara wa gavana wa Mandera Ali Roba ulishambuliwa na maafisa wa polisi watano wakauawa.
Hata hivyo Shisia amekataa kuhusisha tukio la leo Ijumaa na lile la msafara wa gavana akisema katika moja lake, Al-Shabaab walikiri kuhusika.
Hajasema ni lipi hasa linahusishwa moja kwa moja na Al-Shabaab.