KENYA: Wahadhiri wa Vyuo Vikuu waanza mgomo tena kushinikiza Serikali nyongeza ya mishahara yao

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
a250a832bca1ae9357fe305506cb1560.jpg
Shughuli masomo katika vyuo vikuu vya umma zinatarajiwa kulemazwa kuanzia Alhamisi, baada ya Wahadhiri kutangaza mgomo wa Kitaifa.

Wahadhiri hao wanalenga kushinikiza Serikali kutoa Sh5.2 bilioni za kugharamia nyongeza ya mishahara yao.

Katibu Mkuu wa Chama cha Wahadhiri UASU Constantine Wasonga, alisema mgomo huo ulianza rasmi jana saa nane mchana.

Dkt. Wasonga alisema mgomo huo unatokana na hatua ya Serikali ya kukataa kutekeleza mkataba wa maelewano kuhusu nyongeza ya mishahara (CBA) wa 2013 - 2017.

"Tumeagiza Wahadhiri wa vyuo 31 vya umma kote nchini wasuse kazi na kujiunga na mgomo ambao ndio njia pekee inayoelewa Serikali", alisema Dkt. Wasonga jana baada ya Baraza Kuu la Uasu kukutana jijini Nairobi.

Alisema Serikali iliahidi kuwaongezea mishahara lakini kufikia sasa haijatimiza ahadi hiyo wala kuwasiliana na viongozi wa chama cha Uasu.
 
Back
Top Bottom