Kenya ni nchi ya kidikteta; Katiba inasaidia nini?

Kingmaja

Member
Sep 15, 2018
68
109
Oct 03, 2020

UTEUZI WA WANAJESHI SERIKALINI WAZUA TAHARUKI

HATUA ya Rais Uhuru Kenyatta kukabidhi wanajeshi usimamizi wa idara na mashirika ya kiraia imezua hofu ya kuchochea utawala wa kidikteta nchini.

Lakini kwa upande mwingine kuna wachanganuzi wanaounga mkono hatua hiyo wakisema kutumia wanajeshi kumetokana na haja ya kulainisha usimamizi wa idara za serikali wakati wasimamizi wa kiraia wanaposhindwa kutekeleza majukumu yao ifaavyo ama kuhusishwa na ufisadi.

Kufikia sasa Rais Kenyatta amewateua maafisa wa jeshi ama Idara ya Ujasusi (NIS) kusimamia mashirika kadhaa ya umma.

Kati ya maafisa hao ni Meja Jenerali Mohammed Badi wa Idara ya Huduma za Jiji la Nairobi (NMS) akisaidiwa na maafisa wengine sita wa kijeshi.

Bw Badi pia atakuwa akihudhuria vikao vya Baraza la Mawaziri ingawa hajastaafu kutoka jeshini.

Mapema mwezi jana, Rais Kenyatta aliagiza Kampuni ya Nyama ya Kenya (KMC) iwekwe chini ya usimamizi wa KDF.

Mkurugenzi wa Idara ya Ujasusi (NIS) Meja Jenerali Philip Wachira Kameru pia ni mwanajeshi.

Waliotoka NIS ni Inspekta Jenerali wa polisi Hillary Mutyambai, Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) Twalib Mubarak.

Kudhoofisha utawala wa kiraia
 
Back
Top Bottom