Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,489
- 13,608
Baada ya uchaguzi wa Kenya kumalizika, kama kawaida ya tamaduni za chaguzi za kiafrika, yamesikika malalamiko mengi.
Raila Odinga na kambi yake wamelalamika vya kutosha, wamelalamikia rafu za chini chini zilizompatia Uhuru Kenyatta nafasi ya kuendelea kubakia ikulu.
Ni wakenya hawa hawa waliobadilisha katiba yao na kubariki uwepo wa tume huru ya uchaguzi. Tofauti na malalamiko ya wapiga kura wa Tanzania wanaotaka kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi.
Lakini pamoja na uwepo wa tume hiyo, bado inaonekana sio muarobaini wa kuondoa kabisa na malalamiko ya kisiasa. Bado ni kama vile serikali inayoingia kwenye uchaguzi inakuwa na ushawishi wa ziada wakati wa uchaguzi.
Tanzania inalilia katiba mpya ambayo mapendekezo yake yatakuwa ndio msingi wa kuzaliwa kwa tume huru ya uchaguzi. Kwa uzoefu wa uchaguzi wa Kenya wa mwaka huu, nadhani hata tutakapokuwa na tume huru, vilio vya kuibiwa kura vitakuwa pale pale.
La muhimu kwa wanasiasa wetu wa siku zijazo, ni kutomuangalia yule mtu anayekusikiliza siku za kampeni akiwa yupo hoi kimaisha, halafu ukajidanganya kwa kudhani kuwa hata kiakili yupo hoi.
La muhimu ni kutoushusha thamani uwezo wa mpiga kura katika kumchambua mwanasiasa anayemsikiliza jukwaani.
Tume inaweza kuwa huru na isiwe huru kwa uwezo wa mtu mmoja mmoja katika kuifanyia uchambuzi wa kina, lakini mpiga kura ndiye mfalme. Haya maneno ya kwamba eti tumeibiwa kura yanaweza yasiwe na msaada sana kwa mpiga kura.
Uchaguzi wa Kenya haswa kwa maana ya uwepo wa tume huru, ni funzo kwa wanasiasa wetu, ambao huishi kwa kuuamini ule msemo usemao kuwa mbazi ikinyauka husingizia jua.
Raila Odinga na kambi yake wamelalamika vya kutosha, wamelalamikia rafu za chini chini zilizompatia Uhuru Kenyatta nafasi ya kuendelea kubakia ikulu.
Ni wakenya hawa hawa waliobadilisha katiba yao na kubariki uwepo wa tume huru ya uchaguzi. Tofauti na malalamiko ya wapiga kura wa Tanzania wanaotaka kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi.
Lakini pamoja na uwepo wa tume hiyo, bado inaonekana sio muarobaini wa kuondoa kabisa na malalamiko ya kisiasa. Bado ni kama vile serikali inayoingia kwenye uchaguzi inakuwa na ushawishi wa ziada wakati wa uchaguzi.
Tanzania inalilia katiba mpya ambayo mapendekezo yake yatakuwa ndio msingi wa kuzaliwa kwa tume huru ya uchaguzi. Kwa uzoefu wa uchaguzi wa Kenya wa mwaka huu, nadhani hata tutakapokuwa na tume huru, vilio vya kuibiwa kura vitakuwa pale pale.
La muhimu kwa wanasiasa wetu wa siku zijazo, ni kutomuangalia yule mtu anayekusikiliza siku za kampeni akiwa yupo hoi kimaisha, halafu ukajidanganya kwa kudhani kuwa hata kiakili yupo hoi.
La muhimu ni kutoushusha thamani uwezo wa mpiga kura katika kumchambua mwanasiasa anayemsikiliza jukwaani.
Tume inaweza kuwa huru na isiwe huru kwa uwezo wa mtu mmoja mmoja katika kuifanyia uchambuzi wa kina, lakini mpiga kura ndiye mfalme. Haya maneno ya kwamba eti tumeibiwa kura yanaweza yasiwe na msaada sana kwa mpiga kura.
Uchaguzi wa Kenya haswa kwa maana ya uwepo wa tume huru, ni funzo kwa wanasiasa wetu, ambao huishi kwa kuuamini ule msemo usemao kuwa mbazi ikinyauka husingizia jua.