Kenya: Mwanamke mmoja afariki baada ya kuruka kwenye gari la wagonjwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,009
9,874
Naiso Leslie (26) amekufa baada ya kuruka kutoka kwa gari la wagonjwa baada ya mtoto wake Solomon Lesie (2) kufa akiwa njiani kwenda hospitalini

Mama huyo aliruka kutoka kwenye gari la wagonjwa baada ya kuona hali ya mtoto wake inazidi kuwa mbaya alipokuwa akikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kajiado

Mvulana huyo alikuwa katika Kituo cha Afya cha Bisil kabla ya kupewa rufaa ya kuhamishiwa katika hospitali ya rufaa. Mama yake alifungua mlango wa nyuma wa gari la wagonjwa na kuruka, akapata majeraha yaliyopelekea kufa. Aliruka baada ya kuona hali ya mtoto wake ilizidi kuwa mbaya.

Wote walikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kajiado ambapo mtoto huyo alitangazwa kuwa amekufa wakati alipofika mama huyo akishikwa na majeraha wakati akipatiwa matibabu.

Miili hiyo ilihamishiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali hiyo wakati gari la wagonjwa lilipowekwa kwenye Kituo Kikuu cha Polisi cha Kajiado kwa ukaguzi.
 
Back
Top Bottom