Wakuu,
Kwa kadri mambo yanavyoenda Kenya , Afrika Mashariki ijiandae kuwa koloni la Kenya. Hawa watu wako serious kwa kila kitu na si mizaha inayoendelea hapa kwetu. Ukiangalia katiba yao sasa hivi , haitofautiani sana na za nchi za Magharibi, na uwajibikaji uko wazi. Hivyo mihimili yote ya dola hujitegemea na ukiharibu unawajibika mwenyewe kisheria na si kama hapa kwetu tunapobembelezana eti tujiangalie na kuvua magamba.
Sasa hivi unaendelea mchakato wa kumpata Chief Justice, na interview zinafanyika live na kila Mkenya na dunia kwa ujumla anaangalia. Hivyo atakayepatikana ni yule anayejua kweli atawatendea nini waKenya, na si kama boya letu Werema.
Kwa kweli tukiendelea na mizaha hii hapa kwetu Tanzania, tujiandae kupokwa ile sifa aliyotuachia Mwalimu Nyerere ambapo watu wa Tanzania waliheshimika duniani kote.
Ni jambo la busara sana kwa Kikwete kuacha ubinafsi na kuwatendea haki watanzania kwa kuwapa katiba wanayoitaka ili nasi tuweze kuwajibishana ili tujenge taifa letu.Huu ndio utakuwa urithi mkubwa ambao JK anaweza kutuachia Watanzania na akabaki na sifa hadi kaburini. Mwinyi alituanziashia soko huria, Mkapa akaja na kujenga uchumi, JK anatakiwa atupe katiba tunayoitaka. Anatakiwa asafishe mafisadi, na ufisadi ndani ya serikali yake na chama chake ili ajenge heshima mbele ya jamii. Akifanya hayo , atakuwa ametuweka mahali pazuri kupambana na Wakenya hatimaye tusije mezwa kama vidagaa na nchi hiyo yenye wajanja wengi. AKifanya hivyo, JK nitamsamehe kwa rafu zote alizofanya kwenye uchaguzi Mkuu 2010.
Mungu tupe hekima katika hili
Kwa kadri mambo yanavyoenda Kenya , Afrika Mashariki ijiandae kuwa koloni la Kenya. Hawa watu wako serious kwa kila kitu na si mizaha inayoendelea hapa kwetu. Ukiangalia katiba yao sasa hivi , haitofautiani sana na za nchi za Magharibi, na uwajibikaji uko wazi. Hivyo mihimili yote ya dola hujitegemea na ukiharibu unawajibika mwenyewe kisheria na si kama hapa kwetu tunapobembelezana eti tujiangalie na kuvua magamba.
Sasa hivi unaendelea mchakato wa kumpata Chief Justice, na interview zinafanyika live na kila Mkenya na dunia kwa ujumla anaangalia. Hivyo atakayepatikana ni yule anayejua kweli atawatendea nini waKenya, na si kama boya letu Werema.
Kwa kweli tukiendelea na mizaha hii hapa kwetu Tanzania, tujiandae kupokwa ile sifa aliyotuachia Mwalimu Nyerere ambapo watu wa Tanzania waliheshimika duniani kote.
Ni jambo la busara sana kwa Kikwete kuacha ubinafsi na kuwatendea haki watanzania kwa kuwapa katiba wanayoitaka ili nasi tuweze kuwajibishana ili tujenge taifa letu.Huu ndio utakuwa urithi mkubwa ambao JK anaweza kutuachia Watanzania na akabaki na sifa hadi kaburini. Mwinyi alituanziashia soko huria, Mkapa akaja na kujenga uchumi, JK anatakiwa atupe katiba tunayoitaka. Anatakiwa asafishe mafisadi, na ufisadi ndani ya serikali yake na chama chake ili ajenge heshima mbele ya jamii. Akifanya hayo , atakuwa ametuweka mahali pazuri kupambana na Wakenya hatimaye tusije mezwa kama vidagaa na nchi hiyo yenye wajanja wengi. AKifanya hivyo, JK nitamsamehe kwa rafu zote alizofanya kwenye uchaguzi Mkuu 2010.
Mungu tupe hekima katika hili