Kenya Aibu Tupu!

K-Boko

JF-Expert Member
Aug 3, 2013
697
218
Timu kadhaa zilizoshiriki Senior Challenge Cup huko Kenya, ikiwemo Zanzibar Heroes, zimekwama kwa siku kadhaa zikisota nchini humo hata baada ya kutolewa mashindanoni. Kutokana na sintofahamu hiyo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar leo imeingilia kati na kuwarudisha mashujaa wake kwa ndege ya kukodi baada ya kuchoshwa na danadana za wenyeji kupitia Shirikisho lao la soka-FKF. Kwa kuzongwa na hasira, viongozi wa Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) wamesita kutoa kauli leo kwa kuhofia kukurupuka na kauli inayoweza kuvuruga uhusiano wa nchi!

Source: Radio One Stereo (7:30 p.m. Sports Programme)
 
Kwanini nishangae FKF kushindwa kuzigharamia timu shiriki usafir wa kurudi makwao wakati viwanjani hakukua na watazamaji na hata hawo tulokua tunawaona hawakuwa wakilipa viingilio,wameta hasara mno..Musonye na wenzake ni aibu kweli..:)
 
Wakati umefika wa kubadilisha mifumo ya mashindano ya CECAFA ili yalete msisimko na hivyo kwenda kibiashara zaidi. Enzi za Gossage hakukuwa na wadhamini wala mechi hazikuonyeshwa fawahisha (live), zilitangaziwa tu redioni. Lakini zilivuta hisia za Afrika ya Mashariki nzima. Hata mashindano yalipobadilshwa kuwa Challenge msisimko uliendelea, kiasi cha kuwa na Junior Challenge ambayo nayo ilibamba si haba. Tangu Shirikisho la Mpira la Afrika ya Mashariki kuwa CECAFA kwa nchi washiriki kuongezeka, msisimko uko kwenye mteremko. Tujiulize kulikoni, nahisi bado mashindano haya na ya vilabu yanabaki kuwa ni muhimu kwa ukanda huu.
 
Back
Top Bottom