Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,781
- 898
KATIBU MKUU WA UVCCM TAIFA NDUGU KENANI LABANI KIHONGOSI ATENGA MUDA WA KUSIKILIZA NA KUPOKEA MAONI NA USHAURI.
KESHO JUMATATU 16.08.2021 SAA 3 ASUBUHI KATIBU MKUU WA UVCCM TAIFA NDUGU KENANI LABANI KIHONGOSI ATAKUWEPO OFISI NDOGO ZA UVCCM UPANGA DAR ES SALAAM VIJANA WOTE MNAKARIBISHWA SANA.
Kesho Jumatatu 16.8.2021 kuanzia saa 3 Asubuhi nitakuwepo ofisi za UVCCM UPANGA Jijini Dar es Salaam kusikiliza pia kupokea maoni na ushauri, napenda kuwakaribisha Vijana wote tuzungumze pamoja. Karibuni sana katika Ofisi yenu Tuzungumze na kupokea mawazo.
.
.
.
Hongera sana Katibu Mkuu (KM) UVCCM Taifa Ndugu KENANI LABAN KIHONGOSI kwa hatua hii kubwa ya kuleta mabadiriko, hakika umeendelea kuihubiri sera yako ya #MtumishiWaWote kwa vitendo.
Binafsi kwangu nimeifurahia hatua hii ambayo naamini litakua na faida nyingi sana.
Kitendo cha sisi vijana kupata nafasi ya kushauri na kutoa maoni kuhusiana na Jumuiya itakua na faida kubwa sana, Miongoni Mwa faida ni;
1 - Unairudisha dhana ya Jumuiya Yetu ni ya kila Kijana si ya watu wachache kama ilivyokuwa ikionekana zamani.
2 - Lakini unaendelea kuishi dhana ya #MtumishiWaWote.
3 - Naamini hatua hii itasaidia sana kuboresha idara ya Hamasa na Chipukizi.
4 - Nashauri zoezi hili litakua liwe Endelevu, walau lifanyike kila baada ya miezi 6 ili kuwa na maboresho ya mara kwa mara.
5 - Lakini zoezi hili linaweza kuigwa na viongozi wetu wa chini
#MtumishiWaWote🙏