Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,188
- 39,952
Wikiendi iliyopita nilipata mualiko kutoka kwa mpenzi wangu wa zamani; nami nikafunga safari na kueleka mkoani. Baada ya kufika, nikatafuta 'lodge' iliyonipendeza, nikalipia chumba kwa ajili ya mapumziko. Kwa sababu nilikuwa bado sijala, nikaweka oda ya chakula, kitimoto rosti, ndizi, matunda, na bia mbili. Baada ya kuweka oda, nikaenda kuoga ili kupunguza uchovu. Nilipotoka bafuni, ndipo wakaniletea vyakula nilivyoagiza na kuanza kula taratibu. kutokana na uchangamfu wangu, hapo 'lodge' wakawa wamenizoea kwa muda mfupi.
Baada ya kama dakika 20, mwenyeji wangu ndipo akanipigia simu, 'nimeshafika nielekeze chumba ulichofikia' ; nikamwambia ingia hapo mapokezi na wakulete chumba namba 207, baada ya kama dakika chache hivi akawa amefika; ile kumuona tu, na namna alivyovaa nguo za kimitego, ukichangia na chura aliyonayo pamoja na uzuri; nilijiona leo nafaidi utamu wote wa dunia.
Baada ya kusalimiana huku tukiwa tumeshikana, ghafla tukajikuta tupo ulimwengu mwingine; kelele zilivyokuwa zinatoka humo ndani, hadi watu wa nje, mapokezi walikuwa wanasikia; mbaya zaidi anakuwa anataja jina langu ambalo ndio nimeliandikisha pale mapokezi; mchaka mchaka umeendelea kwa muda mrefu huku akipiga makelele tu,najaribu kumzuia kwa kumziba mdomo wapi, anaendelea tu kupiga kelele; nikajisema kimoyo moyo nikisikiliza kelele zake hapa pamoja na kuogopa watu wanaosikia kelele, mzee atalala na sitafaidi kilichonileta.
Nikamuacha aendelee kupiga kelele, ingawa kwenye koldo kuna miguu ilikuwa inatembea tembea lakini mi sikuogopa; baada ya zoezi kuisha, wote mwili ni jasho kama vile tumemwagiwa maji, ingawa AC ilikuwepo. Tukatazamana na kucheka tu.
Baada ya muda akasema aende nyumbani mara moja, halafu baada ya lisaa 1 atarudi, nikamkubalia; Alipoondoka tu, nikasema ngoja nitoke nje niangalie kidogo mazingira; ile kutoka tu, kila mmoja ananiangalia; nikawa najiuliza tatizo ni nini...nikajua inawezekana zile kelele wamezifanya kama 'agenda'. Nikajikausha tu, kama hakuna kilichotokea nikasogelea kaunta na kuendeleza kupiga bia.
Wakuu, mlishakutana na hali hii? Na ulijisikiaje?
Baada ya kama dakika 20, mwenyeji wangu ndipo akanipigia simu, 'nimeshafika nielekeze chumba ulichofikia' ; nikamwambia ingia hapo mapokezi na wakulete chumba namba 207, baada ya kama dakika chache hivi akawa amefika; ile kumuona tu, na namna alivyovaa nguo za kimitego, ukichangia na chura aliyonayo pamoja na uzuri; nilijiona leo nafaidi utamu wote wa dunia.
Baada ya kusalimiana huku tukiwa tumeshikana, ghafla tukajikuta tupo ulimwengu mwingine; kelele zilivyokuwa zinatoka humo ndani, hadi watu wa nje, mapokezi walikuwa wanasikia; mbaya zaidi anakuwa anataja jina langu ambalo ndio nimeliandikisha pale mapokezi; mchaka mchaka umeendelea kwa muda mrefu huku akipiga makelele tu,najaribu kumzuia kwa kumziba mdomo wapi, anaendelea tu kupiga kelele; nikajisema kimoyo moyo nikisikiliza kelele zake hapa pamoja na kuogopa watu wanaosikia kelele, mzee atalala na sitafaidi kilichonileta.
Nikamuacha aendelee kupiga kelele, ingawa kwenye koldo kuna miguu ilikuwa inatembea tembea lakini mi sikuogopa; baada ya zoezi kuisha, wote mwili ni jasho kama vile tumemwagiwa maji, ingawa AC ilikuwepo. Tukatazamana na kucheka tu.
Baada ya muda akasema aende nyumbani mara moja, halafu baada ya lisaa 1 atarudi, nikamkubalia; Alipoondoka tu, nikasema ngoja nitoke nje niangalie kidogo mazingira; ile kutoka tu, kila mmoja ananiangalia; nikawa najiuliza tatizo ni nini...nikajua inawezekana zile kelele wamezifanya kama 'agenda'. Nikajikausha tu, kama hakuna kilichotokea nikasogelea kaunta na kuendeleza kupiga bia.
Wakuu, mlishakutana na hali hii? Na ulijisikiaje?