KadaMpinzani
JF-Expert Member
- Jan 31, 2007
- 3,715
- 86
Kelele za upinzani hazinisumbui -JK
2007-10-21 10:16:10
Na Juma Thomas, Roma
Rais Jakaya Kikwete, amesema kelele zinazopigwa na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu utendaji wa serikali yake hazimsumbui.
Amesema viongozi hao wana uhuru wa kusema ili mradi tu hawachochei vurugu nchini.
``Hali ya siasa ni shwari nchini Tanzania, kelele nyingi zinazopigwa na viongozi wa vyama vya siasa ndio kufanikiwa kwenyewe kisiasa. Hii hainisumbui,`` alisema.
Rais Kikwete aliyasema hayo jana wakati akiongea na Watanzania wanaoishi nchini Italia.
Kuhusu uraia wa nchi mbili na raia wa nje kupiga kura, Rais Kikwete alisema mambo hayo bado yanashughulikiwa.
Alisema Viongozi wa vyama vya upinzani wamekuwa wakituhumu baadhi ya watendaji serikalini kuwa ni wabadhirifu wa mali za umma.
Hivi karibuni viongozi hao walitoa orodha ndefu ya maofisa wa serikali ambao walidai kuwa ni mafisadi.
Hata hivyo, Rais Kikwete alisema kuwa katika siasa za vyama vingi shutuma kama hizo, pamoja na kwamba hazina ukweli wowote, haziwezi kuepukika.
``Hiki ndicho tunachokitegemea kwenye siasa za vyama vingi,`` alisema Rais Kikwete.
Kuhusu usalama wa raia na mali zao, Rais Kikwete alisema kuwa wimbi la ujambazi ambalo lilitikisa serikali mwanzoni mwa utawala wake sasa limedhibitiwa.
``Hatuwezi kusema tutaufuta kabisa ujambazi lakini nachoweza kusema ni kwamba hivi sasa tatizo limepungua kwa kiasi kikubwa baada ya kushirikisha majeshi yetu yote katika mapambano dhidi ya ujambazi,`` alisema.
Kuhusu chakula , alisema kuwa nchi imepata mavuno ya kutosha mwaka huu, na kwamba tatizo sasa ni soko kwa ajili ya mazao ya wakulima.
Nchi ilikumbwa na uhaba wa chakula mwaka jana baada ya kukumbwa na kiangazi cha muda mrefu hali iliyoilazimu kuomba chakula cha msaada kutoka nchi wahisani.
Kuhusu elimu rais aliwaeleza Watanzania hao, ambao wengi wao ni mapadri wa Kanisa Katoliki, kuwa serikali imejitahidi kuhakikisha kuwa kila mtoto wa umri wa kwenda shule anapata nafasi hiyo. Alisema kuwa hivi sasa asilimia 97 ya watoto wenye umri wa kuanza shule ya wameingia shule ya msingi.
Kuhusu shule za sekondari, Rais Kikwete alisema kuwa hivi sasa kila kata ina shule ya sekondari ili kuwezesha watoto wanaomaliza elimu ya msingi waweze kujiunga.
Hata hivyo, alisema kuwa changamoto kubwa ni walimu pamoja na maabara. ``Tunataka wanasayansi kwa hiyo suala la kuwa na maabara katika shule hizi ni la muhimu sana,`` alisema.
Alisema ili kuhakikisha kuwa shule hizo zinakuwa na walimu wa kutosha serikali iliamua kubadilisha chuo cha ualimu Changombe pamoja na Mkwawa kuwa vyuo vikuu ili kupata walimu wa sekondari wengi.
Rais alisema kuwa sambamba na hilo serikali pia imevitaka vyuo vikuu binafsi kuanzisha vitivyo vya elimu ili kupata walimu wengi.
Kuhusu gonjwa la ukimwi, rais alisema kuwa serikali imeendelea kuwaelimisha wananchi namna na kupambana na tatizo hilo. Alisema ili kupambana vizuri na tatizo la ukimwi ni bora kila mwananchi akajua afya yake.
Mwezi Julai mwaka huu Rais Kikwete alifungua kampeni maalumu ya kupima kwa hiari virusi vya ukimwi, na tayari watu 700,000 wamekwisha jitokeza kupima.
Kuhusu madini rais alisema kuwa sheria zinafanyiwa marekebisho ili raslimamli ya madini iweze kuwanufaisha Watanzania zaidi.
Alisema hivi sasa serikali inajenga uwezo wa kusimamia vyema madini ili kuhakikisha kuwa wawekezaji pamoja na wananchi wote wananufaika na rasmali hiyo.
Aliwataka Watanzania hao kukumbuka nyumbani pamoja na kuwekeza walikotoka. Aliwataka pia kutafuta misaada ya maendeleo ili kuendeleza nchi yao.
Akisoma risala, Mwenyekiti wa Watanzania wanaoishi Italia, Padri Gaudensi Mushi, alisema kuwa wanaridhishwa na juhudi za rais Kikwete za kuendeleza uchumi pamoja na huduma nyingine za jamii, ikiwemo elimu.
Aliiomba serikali iangalie uwezekano wa kurekebisha sheria ili kuruhusu uraia wa nchi mbili, ikiwa ni pamoja na kuwaruhusu Watanzania walioko nje ya nchi kupiga kura.
Akijibu hoja hizo, Rais Kikwete alisema suala la uraia wa nchi zaidi ya moja linashughulikiwa na Tume ya Kurekebisha Sheria, na kwamba Tume ikimaliza kazi yake itaishauri serikali.
Hata hivyo, Rais alisema kuwa suala hilo halitaki haraka na kuwaomba Watanzania hao kuwa wavumilivu.
Leo Rais Kikwete atahutubia mkutano wa amani ulioandaliwa na Jumuia ya Mtakatifu Egidio utakaofanyika katika jiji la Napels.
SOURCE: Nipashe
2007-10-21 10:16:10
Na Juma Thomas, Roma
Rais Jakaya Kikwete, amesema kelele zinazopigwa na viongozi wa vyama vya siasa kuhusu utendaji wa serikali yake hazimsumbui.
Amesema viongozi hao wana uhuru wa kusema ili mradi tu hawachochei vurugu nchini.
``Hali ya siasa ni shwari nchini Tanzania, kelele nyingi zinazopigwa na viongozi wa vyama vya siasa ndio kufanikiwa kwenyewe kisiasa. Hii hainisumbui,`` alisema.
Rais Kikwete aliyasema hayo jana wakati akiongea na Watanzania wanaoishi nchini Italia.
Kuhusu uraia wa nchi mbili na raia wa nje kupiga kura, Rais Kikwete alisema mambo hayo bado yanashughulikiwa.
Alisema Viongozi wa vyama vya upinzani wamekuwa wakituhumu baadhi ya watendaji serikalini kuwa ni wabadhirifu wa mali za umma.
Hivi karibuni viongozi hao walitoa orodha ndefu ya maofisa wa serikali ambao walidai kuwa ni mafisadi.
Hata hivyo, Rais Kikwete alisema kuwa katika siasa za vyama vingi shutuma kama hizo, pamoja na kwamba hazina ukweli wowote, haziwezi kuepukika.
``Hiki ndicho tunachokitegemea kwenye siasa za vyama vingi,`` alisema Rais Kikwete.
Kuhusu usalama wa raia na mali zao, Rais Kikwete alisema kuwa wimbi la ujambazi ambalo lilitikisa serikali mwanzoni mwa utawala wake sasa limedhibitiwa.
``Hatuwezi kusema tutaufuta kabisa ujambazi lakini nachoweza kusema ni kwamba hivi sasa tatizo limepungua kwa kiasi kikubwa baada ya kushirikisha majeshi yetu yote katika mapambano dhidi ya ujambazi,`` alisema.
Kuhusu chakula , alisema kuwa nchi imepata mavuno ya kutosha mwaka huu, na kwamba tatizo sasa ni soko kwa ajili ya mazao ya wakulima.
Nchi ilikumbwa na uhaba wa chakula mwaka jana baada ya kukumbwa na kiangazi cha muda mrefu hali iliyoilazimu kuomba chakula cha msaada kutoka nchi wahisani.
Kuhusu elimu rais aliwaeleza Watanzania hao, ambao wengi wao ni mapadri wa Kanisa Katoliki, kuwa serikali imejitahidi kuhakikisha kuwa kila mtoto wa umri wa kwenda shule anapata nafasi hiyo. Alisema kuwa hivi sasa asilimia 97 ya watoto wenye umri wa kuanza shule ya wameingia shule ya msingi.
Kuhusu shule za sekondari, Rais Kikwete alisema kuwa hivi sasa kila kata ina shule ya sekondari ili kuwezesha watoto wanaomaliza elimu ya msingi waweze kujiunga.
Hata hivyo, alisema kuwa changamoto kubwa ni walimu pamoja na maabara. ``Tunataka wanasayansi kwa hiyo suala la kuwa na maabara katika shule hizi ni la muhimu sana,`` alisema.
Alisema ili kuhakikisha kuwa shule hizo zinakuwa na walimu wa kutosha serikali iliamua kubadilisha chuo cha ualimu Changombe pamoja na Mkwawa kuwa vyuo vikuu ili kupata walimu wa sekondari wengi.
Rais alisema kuwa sambamba na hilo serikali pia imevitaka vyuo vikuu binafsi kuanzisha vitivyo vya elimu ili kupata walimu wengi.
Kuhusu gonjwa la ukimwi, rais alisema kuwa serikali imeendelea kuwaelimisha wananchi namna na kupambana na tatizo hilo. Alisema ili kupambana vizuri na tatizo la ukimwi ni bora kila mwananchi akajua afya yake.
Mwezi Julai mwaka huu Rais Kikwete alifungua kampeni maalumu ya kupima kwa hiari virusi vya ukimwi, na tayari watu 700,000 wamekwisha jitokeza kupima.
Kuhusu madini rais alisema kuwa sheria zinafanyiwa marekebisho ili raslimamli ya madini iweze kuwanufaisha Watanzania zaidi.
Alisema hivi sasa serikali inajenga uwezo wa kusimamia vyema madini ili kuhakikisha kuwa wawekezaji pamoja na wananchi wote wananufaika na rasmali hiyo.
Aliwataka Watanzania hao kukumbuka nyumbani pamoja na kuwekeza walikotoka. Aliwataka pia kutafuta misaada ya maendeleo ili kuendeleza nchi yao.
Akisoma risala, Mwenyekiti wa Watanzania wanaoishi Italia, Padri Gaudensi Mushi, alisema kuwa wanaridhishwa na juhudi za rais Kikwete za kuendeleza uchumi pamoja na huduma nyingine za jamii, ikiwemo elimu.
Aliiomba serikali iangalie uwezekano wa kurekebisha sheria ili kuruhusu uraia wa nchi mbili, ikiwa ni pamoja na kuwaruhusu Watanzania walioko nje ya nchi kupiga kura.
Akijibu hoja hizo, Rais Kikwete alisema suala la uraia wa nchi zaidi ya moja linashughulikiwa na Tume ya Kurekebisha Sheria, na kwamba Tume ikimaliza kazi yake itaishauri serikali.
Hata hivyo, Rais alisema kuwa suala hilo halitaki haraka na kuwaomba Watanzania hao kuwa wavumilivu.
Leo Rais Kikwete atahutubia mkutano wa amani ulioandaliwa na Jumuia ya Mtakatifu Egidio utakaofanyika katika jiji la Napels.
SOURCE: Nipashe