O-man
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 323
- 65
Kuna bar na guest (mwenyewe ameipa jina la hoteli) jirani yangu inatunyima amani kwa kelele za juke box. Ni kuanzia asubuhi mpaka usiku wa saa 6 au zaidi. Tumezungumza na mmiliki lakini wapi. Ilifikia hatua baadhi ya majirani wanaoishi gorofani kutupia vipande vya matofali juu ya paa la hiyo hoteli ili kufikisha ujumbe wa hizo kelele, bado zinaendelea. Mjumbe, M/kiti wa serikali za mitaa na mtendaji wanazo taarifa. Hapa tumekwama. Msaada wenu unahitajika kutuondolea kadhia hii.