Kazi zipo ila ajira hakuna

Mkuu, wewe ni Mtu smart sana, Comment kama hizi huna haja ya Kuzijibu kabisa, Unsoma unapita tu; Jibu vitu vyenye Hoja nzito, hiyo inatosha, Usitake kumfurahisha Kila mtu; Wenye uhitaji tumekuelewa Mkuu;
Ahsante kwa kunielewa mkuu; inatubidi tubadirike kifikra vinginevyo malalamiko yatakuwa kibao.
 
Habari za leo waungwana!
Leo nakushirikisha katika hili .... hapa Tanzania tuna wasomi wetu wengi ambao wanachotaka ni AJIRA TU. Serikali nayo inadhani itaweza kutatua tatizo la ajira kwa a one-sided view. Kwamba mtu asiye na ajira dawa yake kumpa ajira. Si kweli kwamba hiyo ndo dawa pekee. In fact tuendako hiyo ni wrong solution. Mfano mdogo ajira za madereva kwa dunia ya leo zinaondoka moja moja.
Fikiria: Siku jiji hili la Dar es Salaam kwa mfano hili likiwa na Mwendokasi kila Kona ya jiji na huko mbali na city centre kote kuanzia Bunju (au Bagamoyo) hadi Mbagala na hadi huko Chalinze.
Halafu treni za umeme ziko
Halafu self driving cars
Halafu drones za kudeliver mizigo kwa wateja (yani uko zako nyumbani labda Bunju unaagiza chakula KFC Posta unalipia kwa M-PESA kinaletwa na drone ndani ya robo saa tu hadi mlangoni kwako)
Hapo mtu aliyesomea udereva ataendesha nini?
Licha ya hayo mambo kukawia yatafika. Lakini hata kabla hayajafika ajira ngapi zipo na nani atapata nani akose.
Wasomi wetu ni lazima waanze kuwaza tofauti na wasomi wa mwaka 1970. Lazima kuwaza option ya kusurvive nje ya mfumo wa ajira.
Tatizo wengi wanachotaka ni MSHAHARA tu. Ndo maana wakikutana na wewe utasikia: "BRO NIUNGANISHE BASI HATA KWA RAFIKI ZAKO NIPATE KAZI". Ndo lugha yao. NIUNGANISHE. Yaani utadhani wewe umekuwa fundi welding... Ukimpa idea nyingine HATAKI.
Ndo maana watu wasio na shule ndeefu ndo wanakuwa matajiri. Si bure. Katika matajiri wote 2000+ kwenye Forbes wenye MBA unaweza kuta hata 10 hawafiki. Na hao wenye hiyo MBA siyo kuwa ndo imewafanya wa excel in bness.
Lazima kuwaza kwa mapana. Wasomi hawataki kuumiza kichwa wanataka ready made things. Hii si njema kwa afya ya uchumi wa taifa letu.
Ukitazama #DiamondPlutnumz na karanga unashangaa kwa nini msomi akikuona unaanzisha biashara yako anataka umpe tu AJIRA hataki umfundishe afanye. Makanisani nako wasomi wanaombewa tu wapate AJIRA. Basi. Kweli? Ina maana hakuna MAONO mengine kwa wasomi wetu isipokuwa ajira?
Elimu ya juu kwa vijana wengi imepeleka creativity yao na uthubutu wao CHINI!
So sad!
Sikiliza kijana msomi:
Ni muhimu kuyatazama maisha yako kwa mapana na kwa upya kabisa pasipo kuyahusisha na elimu yako ya darasani kabisa.
Mungu awabariki sana.

Jifunze Kuthubutu tusiwe na kikomo cha kufikiri.
Fikiri hata mara 1000 usiochoke unapoanguka ndo inakuongezea uwezo wa kutatua Changamoto zinazokukakabili.
KUMBUKA AJIRA HAZIPO LAKINI KAZI ZIPO

UNAWEZA WAKATI NI SASA.
Fact,
Ila kwa hapa jamii forum Mkuu sidhani Kama sisi vijana wa humu tutakuelewa,
Maana tuna common excuse ya kutokua na mtaji,
Lakini inasikitisha Sana unakuta ni mwaka wa pili sasa tokea msomi ahitimu shahada yake, na ajira hajapata na bado haoni umuhimu wa kuwaza alternative ya kutatua tatizo la ajira,
 
Fact,
Ila kwa hapa jamii forum Mkuu sidhani Kama sisi vijana wa humu tutakuelewa,
Maana tuna common excuse ya kutokua na mtaji,
Lakini inasikitisha Sana unakuta ni mwaka wa pili sasa tokea msomi ahitimu shahada yake, na ajira hajapata na bado haoni umuhimu wa kuwaza alternative ya kutatua tatizo la ajira,
Kuna msingi mmoja wa kubadirisha fikra unasema hivi "Mfundishe mtu kitu fulani mara 16; baada ya hapo kuna mabadiriko yatatokea kwenye fikra zake"
Mabadiriko hayo ni maswali atakayokuwa ajijiuliza, moja ni la kwa nini jambo hili limefundishwa sana lakini mimi haliniingii? Akipata jibu la sali hili tayari ameanza kubadirika kwenye fikra.
 
Siku ya kwanza kuona hii post nilikuona kama ni Mwana siasa hivi mkuu ila this time naona ni kweli baada ya kufanyia kazi kwa upande flani uko sahihi muhimu tu mtu binafsi kuchanganua akili nini afanye na kipi ni sahihi kwa upande wake.
 
1. Unajiajiri kwanza ili upate mtaji ....

2. Mtaji namba moja ni hiyo elimu uliyo nayo; elimu hiyo unaibadili inakuwa maarifa ... maarifa hayo unayatoa kwa wengine .. hapa kuna tatizo kidogo jinsi ya kuyatoa.
Wengi wanahitaji ku-deliver walicho nacho kichwani kwa njia iliyozoeleka .. kufundisha madarasani. Ukiandika vitabu je?
Umejibu vizuri, kuongezea, kuyatoa hayo maarifa sasa inawezekana kwa kuwa consultant au freelancer kwenye mtandao kama www.ajiras.com
Mtu uhitaji mtaji wa hela, ni ujuzi wako. Unaregister na kupost kazi unayoweza kumfanyia mtu.
 
Umewaza mbali hakika lakini nikuulize swali dogo sana ivi unawezaje kujiajiri bila mtaji au ndo ile twende saccos tukakope tulime matikiti.


Swali la pili wewe umejiajiri basi tupatie walau mbinu mkuu sababu naamini mali inapatikana darasani


Assume nimemaliza bachelor ya ualimu wa sanaa.
Cheki www.ajiras.com angalia unaweza kutoa huduma gani kwa watu, huduma ambayo watalipia.
Kwa kutumia elimu yako hiyo, unaweza fanya hivyo. Kujiunga ni bure na watu wa ajiras wanakufanyia marketing wenyewe.
 
naona unatafuta Ban kwa nguvu
Ban ya nini tena? Kuna tatizo kwenye hiyo post?
Watu mnaongelea kujiajiri, na hiyo site niya freelancing kuhusu kujiajiri tena ya bongo. Una uza na kununua huduma.
Kama kupatana tofauti ni kuwa huuzi vitu, unauza ujuzi wako.
 
Ban ya nini tena? Kuna tatizo kwenye hiyo post?
Watu mnaongelea kujiajiri, na hiyo site niya freelancing kuhusu kujiajiri tena ya bongo. Una uza na kununua huduma.
Kama kupatana tofauti ni kuwa huuzi vitu, unauza ujuzi wako.
sawa , ila unatafuta ugomvi wa lazima na Mods
 
Umesema neno ambalo wengi hawapendi kulisikia japo lina ukweli.
Jamani vijana msione dawa chungu tunataka mpone
 
Siku ya kwanza kuona hii post nilikuona kama ni Mwana siasa hivi mkuu ila this time naona ni kweli baada ya kufanyia kazi kwa upande flani uko sahihi muhimu tu mtu binafsi kuchanganua akili nini afanye na kipi ni sahihi kwa upande wake.
Ahsante kwa kunielewa ...
Sijawahi kuwa mwanasiasa na sitegemei kuwa mwanasiasa. Napenda sana kufuatilia mambo mengi na kujaribu kufanya kwa vitendo.
 
Jifunze kuhusu Hisa ...

Hebu soma hiyo hapo kwanza ... kwa nini umeangalia karibu sana kwenye kufuga tu. Maelezo yangu ya awali yana maana zaidi ya kufuga.

NGUVU YA UMOJA
Siku moja kundi la watu 500 walikua wamehudhuria Semina. Mara msemaji mkuu wa semina hiyo akaanza kumpa kila mtu puto (balloon), na kuwaambia kila mmoja aandike jina lake juu la puto alilopewa.

Kisha maputo yote yakakusanywa na kuwekwa kwenye chumba kimoja.Kisha watu wote wakaambiwa waingie kwenye chumba hicho na kila mmoja atafute puto lenye jina lake ndani ya dakika 5. Kila mmoja akaanza kuhangaika huku na kule akitafuta puto lake bila mafanikio, na chumba chote kikawa na fujo tupu.Baada ya dakika 5 kwisha, hakuna hata mmoja aliyekua amefanikiwa kupata puto lake.

Ndipo msemaji akawaambia basi kila mmoja achukue puto lolote tu na ampe mtu ambaye jina lake limeandikwa kwenye puto hilo. Ndani ya dakika chache kila mmoja akawa ameshapata puto lake.Ndipo msemaji mkuu akasema:
Hii inatokea kwenye maisha yetu kila siku. Kila mtu anahangaika kutafuta furaha yake huku na kule, bila kujua ilipo. Furaha yako ipo kwenye furaha za watu wengine. Wape furaha watu wanaokuzunguka;nawe utapata Furaha yako.Usipende kujitenga… Maisha ni watu…. Bila watu hakuna furaha….hakuna Maisha!

Kuna kitu kinaitwa Cage ... tengeneza cage then mwombe huyo mwenye nyumba sehemu ndogo tu just ft 3 x 4 weka cage yako fugia humo.
Unaandika hadithi tu
 
Ni kweli, kazi zipo kibao. Nchi hii ina changamoto chungu nzima, nchi hii bado changa haina maendeleo. Inahitajika kufanya kazi kubwa sana kutatua changamoto na kufanya nchi yetu iendelee kama nchi zingine zilizoendelea.

Sema, kikwazo kikubwa kwa sasa ni 'mentality' ya kikoloni kuwa maisha ya msomi ama maisha ya kipato ni kuwa na ajira ya kupata mshahara mwisho wa mwezi.

Siku hii mentality ikifa akilini na moyoni mwa mtu ndipo atakaposhangaa ni namna gani alivyo na uwezo mkubwa wa kujipatia kipato kikubwa nje ya ajira.

Kazi zipo nyingi sana, sema tu sio za lelema unapaswa kujituma si kawaida tofauti na watu waliopo kwenye ajira. Na hapa ndipo penye shida sana watu hawataki kujituma sana, wanataka kujituma kidogo tu kama wafanyavyo wenye ajira.

Mimi nasisitiza tujitume sana maisha yatakuwa mazuri mara kumi zaidi ya walio kwenye ajira. Hii nchi ina kazi nyingi mno ila ajira ni chache sana kama sio hakuna kabisa.

Hata hivyo ieleweke tu wazi kuwa kadri muda unavyosonga mbele ndivyo hali inavyozidi kuwa complicated wala tusitarajie eti mambo yatakuwa ahueni kidogo.

Hali ya maisha ya sasa ina provide kile kitu kinaitwa 'SURVIVAL FOR THE FITTEST'. Hata waliopo kwenye ajira wanalalamika kipato kidogo, hawana future nzuri na walio nje ya ajira wanalalamika maisha magumu. Hii contradiction ndio haswa inatengeneza mazingira 'survival for the fittest, and the weak will perish'. Let's be fit.

Kwa maneno mengine ni kusema kwamba, kwa nyakati hizi the strongest and luckiest people are going to shine above the weak people, yaani hizi ndio nyakati bora kabisa za watu strong and lucky. Prove yourself how strong and lucky you are, or else how weak you are!

Kwa hisani ya Tutor B
 
Hizi story wakati unazitoa gawa na mil.5 kwa kila kijana nadhani itasaidia kutekeleza hilo wazo kwa vitendo. Laiti kama mazingira ya biashara yangekuwa rafiki vijana wengi wangekuwa na msukumo wa kujiajiri. Unakopa mtaji kwa ndugu ufanye kitu unakutana na changamoto lukuki mtaji unakata unaishia kuwa maskini tu. Maana biashara nyingi huwez fanikiwa ukiwa unaianza tu. Na trust me ukitaka ufanye biashara kwa ubunifu wa hali ya juu inataka huge investment in branding kuliko hata bidhaa zenyewe utazozalisha. Wateja ndio msingi wa mafanikio kwenye biashara, branding ni gharama sana!
 
Back
Top Bottom