Kazi zipo ila ajira hakuna

Ukweli mchungu,Mimi nimekuelewa Mkulu
Wabongo wamezoea siasa (maneno matamu ya kinafiki). Mimi hadi nimefungua grocery na nikawa nauza mwenyewe - watu wananicheka lakini kuna kitu nilikuwa napata; badala ya kutoka kwenye mishe zangu nikajichanganya kwenye baa za watu nilikuwa naenda kwenye grocery yangu - nachoma mishkaki na inaisha kabisa.
Yaani nikiangalia kazi zilizopo mtaani ni nyingi sana ila watu / vijana hawataki kabisa.
 
Ukweli mchungu,Mimi nimekuelewa Mkulu
10000000000% CORRECT SIR!!!.... Kijana mwenzang usipochukia haya utajuata.... Mana hata mm ni Bachelor degree cjaajiriwa na sina iman na kaujiriwa kabsaaa..... Japo ni ukwel mwanzo mgum xanaa hasa ukizingatia umetoka chuo na huna backup nzur ya financial capital..... Inabidi kutumia akili nying xana kuwa mbunifu ku rise capital,,......


Kwa upande mwngine mazingira wezeshi toka serekalini ni muhimu sanaa ili kuendeleza juhudi za kijana,........
 
Habari za leo waungwana!
Leo nakushirikisha katika hili .... hapa Tanzania tuna wasomi wetu wengi ambao wanachotaka ni AJIRA TU. Serikali nayo inadhani itaweza kutatua tatizo la ajira kwa a one-sided view. Kwamba mtu asiye na ajira dawa yake kumpa ajira. Si kweli kwamba hiyo ndo dawa pekee. In fact tuendako hiyo ni wrong solution. Mfano mdogo ajira za madereva kwa dunia ya leo zinaondoka moja moja.
Fikiria: Siku jiji hili la Dar es Salaam kwa mfano hili likiwa na Mwendokasi kila Kona ya jiji na huko mbali na city centre kote kuanzia Bunju (au Bagamoyo) hadi Mbagala na hadi huko Chalinze.
Halafu treni za umeme ziko
Halafu self driving cars
Halafu drones za kudeliver mizigo kwa wateja (yani uko zako nyumbani labda Bunju unaagiza chakula KFC Posta unalipia kwa M-PESA kinaletwa na drone ndani ya robo saa tu hadi mlangoni kwako)
Hapo mtu aliyesomea udereva ataendesha nini?
Licha ya hayo mambo kukawia yatafika. Lakini hata kabla hayajafika ajira ngapi zipo na nani atapata nani akose.
Wasomi wetu ni lazima waanze kuwaza tofauti na wasomi wa mwaka 1970. Lazima kuwaza option ya kusurvive nje ya mfumo wa ajira.
Tatizo wengi wanachotaka ni MSHAHARA tu. Ndo maana wakikutana na wewe utasikia: "BRO NIUNGANISHE BASI HATA KWA RAFIKI ZAKO NIPATE KAZI". Ndo lugha yao. NIUNGANISHE. Yaani utadhani wewe umekuwa fundi welding... Ukimpa idea nyingine HATAKI.
Ndo maana watu wasio na shule ndeefu ndo wanakuwa matajiri. Si bure. Katika matajiri wote 2000+ kwenye Forbes wenye MBA unaweza kuta hata 10 hawafiki. Na hao wenye hiyo MBA siyo kuwa ndo imewafanya wa excel in bness.
Lazima kuwaza kwa mapana. Wasomi hawataki kuumiza kichwa wanataka ready made things. Hii si njema kwa afya ya uchumi wa taifa letu.
Ukitazama #DiamondPlutnumz na karanga unashangaa kwa nini msomi akikuona unaanzisha biashara yako anataka umpe tu AJIRA hataki umfundishe afanye. Makanisani nako wasomi wanaombewa tu wapate AJIRA. Basi. Kweli? Ina maana hakuna MAONO mengine kwa wasomi wetu isipokuwa ajira?
Elimu ya juu kwa vijana wengi imepeleka creativity yao na uthubutu wao CHINI!
So sad!
Sikiliza kijana msomi:
Ni muhimu kuyatazama maisha yako kwa mapana na kwa upya kabisa pasipo kuyahusisha na elimu yako ya darasani kabisa.
Mungu awabariki sana.

Jifunze Kuthubutu tusiwe na kikomo cha kufikiri.
Fikiri hata mara 1000 usiochoke unapoanguka ndo inakuongezea uwezo wa kutatua Changamoto zinazokukakabili.
KUMBUKA AJIRA HAZIPO LAKINI KAZI ZIPO

UNAWEZA WAKATI NI SASA.
neno la kweli sana hili,natamani kuwaambia watu wengi kwamba ajira hamna ila kazi zipo...
 
Matajiri ni wachache sana duniani,ukilinganisha na idadi ya watu waliopo;hii inamaanisha mtu kuwa tajiri au kujiajiri ni kipaji na sio kila mtu anacho,kwa hiyo wanaoshauri watu wajiajiri wajiulize je yeye amejiajiri/ameajiriwa.
 
Matajiri ni wachache sana duniani,ukilinganisha na idadi ya watu waliopo;hii inamaanisha mtu kuwa tajiri au kujiajiri ni kipaji na sio kila mtu anacho,kwa hiyo wanaoshauri watu wajiajiri wajiulize je yeye amejiajiri/ameajiriwa.
Hii ni point ya maana sana.
 
Kufikiri ndio kukoje? au unapofikiri unakuwaje? nahisi labda hata mimi sijui kufikiri, ingawa mleta uzi anasema tufikirie hata mara 1000, je kufikiri mara moja kukoje?
 
Hili jibu sahihi kwa mleta Mada, Wapishe vijana uje ufikirie mtaani mara 1000000, tuone hizo fikra zako.
Jaribu kunielewa - mimi ndiye mleta mada; sina ajira - najishughulisha na mambo yangu kila siku. Na sijawahi kuajiriwa labda kufanya kazi za mkataba mfupi tu.
Kikubwa nashukuru kuna vijana niliwashauri na sasa wamekubali ushauri wangu niko nao tunaendelea kufanya kazi. Waliikuwepo tu mitaani wanazunguka na bahasha lakini kwa sasa wapo wanapiga kazi kama kawaida.
Anayesema haiwezekani yuko sahihi - na pia anayesema inawezekana yuko sahihi.
Unavyofikiri ndivyo ulivyo!
 
Naomba niwajibu wote kwa pamoja mnaofikiri kwamba mimi nimeajiriwa ...
Nikiwa mdogo (chini ya miaka 14) nilikuwa na uwezo wa kutengeneza vikapu - entukuru na kupeleka minadani. Haikutosha, nikawa nafuga kuku wa kienyeji, nauza mayai na kuku pia. Shughuli hiyo niliendelea nayo hadi nilipomaliza elimu ya msingi na kulazimika kwenda sekondari - bweni.

Wakati nikiwa sekondari, likizo zangu zote nilirudi kijijini kuendelea na mchakato huo huo. Hivyo kwenye kukua kwangu nilizoea mzingira ya kujitafutia pesa za kwangu binafsi kwa ajili ya matumizi yangu. Wazazi waliwajibika kulipa karo (japo ilikuwa kidogo) pamoja na matumizi mengine ya lazima pindi niwapo shuleni.

Baada ya kumaliza kidato cha nne, nilijiunga moja kwa moja DarTech (kwa sasa inaitwa DIT); nikiwa hapo nilikuwa nachukua bidhaa toka mipakani Tunduma na Mtukura na kuwauzia wamachinga kwa bei ya jumla; wao wanaingiza mtaani na kupata faida. Baadaye nikapata mchongo wa kwamba chuma chakavu kina soko nchini Kenya - mnunuzi mzuri alikuwa anaitwa Mkole (sijui kama bado yupo). Niliporudi nyumani nilinunua mzani kwa ajili ya kupima chuma - hivyo vijana wa pale mtaani walikusanya masufuria mabovu, nyaya n.k na kuleta kupima; nilimwajiri kijana ambaye kazi yake ilikuwa ni kupima na kutunza kumbukumbu. Akifikisha mzigo unaozidi kilo 100 nilisafiri toka Dar kurudi home ili nisafirishe mzigo kupeleka Kenya. Huko nilirudi na bidhaa za urembo ambazo niliendelea kuwauzia wamachinga.

Baada ya kumaliza chuo; sikuwa na wazo la kuajiriwa kwa kuwa tayari nilishakuwa mzoefu wa kutosa hela kwenye biashara na kupata faida. Kwa kuwa nilikuwa huru, nilifanikiwa kupata watu wenye mali ambazo zina spidi ndogo (hazitoki sana) hivyo walinipatia ili niwe na mlango wa biashara hapa Tanzania. NIliendelea na shughuli hizo na baadaye niliona kuwa shughuli za matumizi ya computer zinalipa; hivyo nilijiandikisha kufanya mitihani kwa kuwa ujuzi wa kutumia computer nilikuwa nao tayari (Nilisoma computer DarTech kama somo la ziada ambalo tulikuwa hatufanyi mtihani - miaka ya 90 hiyo).

Hadi sasa ninapoandika hivi; huwa nafanya kazi za muda; nalipwa kilicho changu naendelea na shughuli zangu. Ajira inafunga ufahamu; sio kwamba nawadanganya - hii ndiyo kweli yangu. Kwa sasa ni muelimishaji wa vikundi vya wajasiriamali; nafuga, nafanya kazi na NGO ambayo mimi ni mwanzilishi - MAISHA YANAENDA.

Ukipata ajira fanya ila usikae tu nyumbani eti unasubiri ajira wakati benk una pesa kama laki 500,000/= inaendelea kupungua kila iitwayo leo.
Mkuu nina laki tano kweli iko benki sina wazo la biashara...hakika Unaweza ukanipa maujuzi ya kujiongeza
 
Mkuu nina laki tano kweli iko benki sina wazo la biashara...hakika Unaweza ukanipa maujuzi ya kujiongeza
Kuna kipindi nilifundisha kuhusu mpango wa vikundi vya hisa.
Ebu nikupe mfano mdogo ...
Watu 10, kila mmoja ana hela yake ametunza eti iongezeke ndo afanye shughuli fulani. Lakini watu kumi hawa ukiwaunganisha kimawazo ni rahisi wote kupata mitaji yao ndani ya muda mfupi.. hapa natoa mfano wa kile ninachokifanya.
Anza hisa kwa watu 10 Kila mmoja atoe kianzio Tshs. 100,000/= Mtakuwa na jumla ya Tshs. 1,000,000/=
Alafu mjipangie kuwa thamani ya Hisa moja iwe Tshs. 5,000/= Hivyo kwa watu 10; kila mmoja akinunua Hisa 3 mtapata jumla ya Tshs (3 x 5,000/= x watu 10) = 150,000/= - inaweza ikazidi hapo.
Jumla mtakuwa na Tshs. 1,150,000/=. Hiyo hela tangaza kuikopesha kwa riba ya asilimia 10 kwa mwezi.
Baada ya miezi sita tu nakuhakikishia mtakuwa na pesa ndefu sana ambapo kila mmoja ataendesha shughuli zake kwa uhakika zaidi.
Back to your laki tano .... fuga kuku au sungura au bata. Soko liko njenje.
 
Kuna kipindi nilifundisha kuhusu mpango wa vikundi vya hisa.
Ebu nikupe mfano mdogo ...
Watu 10, kila mmoja ana hela yake ametunza eti iongezeke ndo afanye shughuli fulani. Lakini watu kumi hawa ukiwaunganisha kimawazo ni rahisi wote kupata mitaji yao ndani ya muda mfupi.. hapa natoa mfano wa kile ninachokifanya.
Anza hisa kwa watu 10 Kila mmoja atoe kianzio Tshs. 100,000/= Mtakuwa na jumla ya Tshs. 1,000,000/=
Alafu mjipangie kuwa thamani ya Hisa moja iwe Tshs. 5,000/= Hivyo kwa watu 10; kila mmoja akinunua Hisa 3 mtapata jumla ya Tshs (3 x 5,000/= x watu 10) = 150,000/= - inaweza ikazidi hapo.
Jumla mtakuwa na Tshs. 1,150,000/=. Hiyo hela tangaza kuikopesha kwa riba ya asilimia 10 kwa mwezi.
Baada ya miezi sita tu nakuhakikishia mtakuwa na pesa ndefu sana ambapo kila mmoja ataendesha shughuli zake kwa uhakika zaidi.
Back to your laki tano .... fuga kuku au sungura au bata. Soko liko njenje.
Mkuu nyumba za kupanga unafugia wapi kuku au sungura...? Bado natega sikio kukusikiliza
 
Jifunze kuhusu Hisa ...
Mkuu nyumba za kupanga unafugia wapi kuku au sungura...? Bado natega sikio kukusikiliza
Hebu soma hiyo hapo kwanza ... kwa nini umeangalia karibu sana kwenye kufuga tu. Maelezo yangu ya awali yana maana zaidi ya kufuga.

NGUVU YA UMOJA
Siku moja kundi la watu 500 walikua wamehudhuria Semina. Mara msemaji mkuu wa semina hiyo akaanza kumpa kila mtu puto (balloon), na kuwaambia kila mmoja aandike jina lake juu la puto alilopewa.

Kisha maputo yote yakakusanywa na kuwekwa kwenye chumba kimoja.Kisha watu wote wakaambiwa waingie kwenye chumba hicho na kila mmoja atafute puto lenye jina lake ndani ya dakika 5. Kila mmoja akaanza kuhangaika huku na kule akitafuta puto lake bila mafanikio, na chumba chote kikawa na fujo tupu.Baada ya dakika 5 kwisha, hakuna hata mmoja aliyekua amefanikiwa kupata puto lake.

Ndipo msemaji akawaambia basi kila mmoja achukue puto lolote tu na ampe mtu ambaye jina lake limeandikwa kwenye puto hilo. Ndani ya dakika chache kila mmoja akawa ameshapata puto lake.Ndipo msemaji mkuu akasema:
Hii inatokea kwenye maisha yetu kila siku. Kila mtu anahangaika kutafuta furaha yake huku na kule, bila kujua ilipo. Furaha yako ipo kwenye furaha za watu wengine. Wape furaha watu wanaokuzunguka;nawe utapata Furaha yako.Usipende kujitenga… Maisha ni watu…. Bila watu hakuna furaha….hakuna Maisha!

Kuna kitu kinaitwa Cage ... tengeneza cage then mwombe huyo mwenye nyumba sehemu ndogo tu just ft 3 x 4 weka cage yako fugia humo.
 
Endelea kudanganyana - mi natumia laptop yangu na modem.
Mkuu, wewe ni Mtu smart sana, Comment kama hizi huna haja ya Kuzijibu kabisa, Unsoma unapita tu; Jibu vitu vyenye Hoja nzito, hiyo inatosha, Usitake kumfurahisha Kila mtu; Wenye uhitaji tumekuelewa Mkuu;
 
Back
Top Bottom