Kazi za Kiongozi Mkuu wa ACT-Tanzania

Mimi nadhani ni wakati wetu sisi wananchi kujifunza badala ya kuendelea kulaumu maana Kilichotokea ACT ni uamsho juu ya madaraka na kutenganisha Uongozi wa Chama kama chombo kinachosimamia wanachama na uongozi wa nchi unaowakilisha watu wote bila kujali matabaka yao.

ACT kuwa na cheo cha Kiongozi ndio mpango mzima japo tumeona Zitto kapewa majukumu makubwa zaidi na hii inatokana na mazoea yetu sisi wote maana JK ni Kiongozi na Mwenyekiti wa CCM, Mbowe ni Mwenyekiti na kiongozi wa Chadema, Lipumba ni Mwenyekit na Kiongozi wa CUF, vivyo hivyo vyama vyote vya siasa nchi kila kiongozi amechukua majukumu mengi na makubwa kuendesha chama na kutangaza itikadi na sera za chama kwa wananchi, matokeo yake kumekuwa na vurugu kubwa juu ya nani sauti ya chama.

nakumbuka wakati fulani nilikutana na Marafiki wa Slaa nikataka kushauri mabadiliko ktk uongozi kuwepo na viongozi wa chama na viongozi wa Kitaifa nikaona watu wenyewe hatuelewani nikameza maneno yangu maana niliuliza tu kwa nini muwe wafuasi marafiki wa Slaa lakini sio wafuasi wa Chadema? wakajibu wao wanakubaliana na vision ya Dr.Slaa tu...Jibu zuri kabisa lakini hawakuelewa undani wake.

Hivyo iwe mwanzo mzuri kwetu na vyama kujitambua kwamba hakuna sababu ya kujirundikia madaraka maana inakupa majukumu mengi mtu mmoja kupita kiasi. Hili ndilo tatizo letu na tujifunze na nina hakka ACT watarekebisha majukumu baina ya Kiongozi na Mwenyekiti kulingana na muundo huu lakini ukweli ni kwamba hivi ndivyo inavyotakiwa. Na vyama vinginevyo wafuatie maana hii ndio demokrasia.

Kwahiyo inamaana kuwa hayo madaraka aliyonayo supreme leader zzk sio mengi na makubwa?! au unadhan hicho kilichoandikwa kwenye katiba ni madaraka madogo?!

Watanzania bana unaandika kitu na kukisahau hapo hapo!
 
Kwahiyo inamaana kuwa hayo madaraka aliyomayo supreme leader sio mengi na makubwa?! Watanzania bana unaandika kitu na kukisahau hapo hapo!
Hapana sijasema hivyo, niilichosema viongozi wote wa vyama ni supreme leaders iwe hata hao Wenyeviti maana tumeshindwa kutenganisha madaraka ya ndani ya vyama na madaraka ya vyama kwa wananchi wote. Chadema nako hakuna unafuu wowote, Kiongozi alitakiwa kuwa Dr.Slaa na Mwenyekiti awe Mbowe watenganishe mamlaka yao badala ya Dr.Slaa kuwa Katibu wa chama halafu mgombea Urais, Mbowe Mwenyekiti na Kiongozi mkuu.. Na sitegemei utanielewa kwa sababu tumezoea kutawaliwa na sii kuongozwa.
 
Mimi nadhani ni wakati wetu sisi wananchi kujifunza badala ya kuendelea kulaumu maana Kilichotokea ACT ni uamsho juu ya madaraka na kutenganisha Uongozi wa Chama kama chombo kinachosimamia wanachama na uongozi wa nchi unaowakilisha watu wote bila kujali matabaka yao.

ACT kuwa na cheo cha Kiongozi ndio mpango mzima japo tumeona Zitto kapewa majukumu makubwa zaidi na hii inatokana na mazoea yetu sisi wote maana JK ni Kiongozi na Mwenyekiti wa CCM, Mbowe ni Mwenyekiti na kiongozi wa Chadema, Lipumba ni Mwenyekit na Kiongozi wa CUF, vivyo hivyo vyama vyote vya siasa nchi kila kiongozi amechukua majukumu mengi na makubwa kuendesha chama na kutangaza itikadi na sera za chama kwa wananchi, matokeo yake kumekuwa na vurugu kubwa juu ya nani sauti ya chama.

nakumbuka wakati fulani nilikutana na Marafiki wa Slaa nikataka kushauri mabadiliko ktk uongozi kuwepo na viongozi wa chama na viongozi wa Kitaifa nikaona watu wenyewe hatuelewani nikameza maneno yangu maana niliuliza tu kwa nini muwe wafuasi marafiki wa Slaa lakini sio wafuasi wa Chadema? wakajibu wao wanakubaliana na vision ya Dr.Slaa tu...Jibu zuri kabisa lakini hawakuelewa undani wake.

Hivyo iwe mwanzo mzuri kwetu na vyama kujitambua kwamba hakuna sababu ya kujirundikia madaraka maana inakupa majukumu mengi mtu mmoja kupita kiasi. Hili ndilo tatizo letu na tujifunze na nina hakka ACT watarekebisha majukumu baina ya Kiongozi na Mwenyekiti kulingana na muundo huu lakini ukweli ni kwamba hivi ndivyo inavyotakiwa. Na vyama vinginevyo wafuatie maana hii ndio demokrasia.

Mimi nitakuelewa kama utaya align majukumu ya kiongozi mkuu wa act na ya mwenyekiti wa act ili nifanye balancing na vyama vingine kuona kama mwenyekiti analo jukumu lolote la uenyekiti au ni figure head tu chamani.

Kuhusu kiongozi wa chama na kiongozi wa taifa hapo umeniacha kidogo, kwakuwa nijuavyo mimi kiongozi wa kitaifa anatokana na kiongozi wa chama huu ndio mfumo uliopo Tanzania, kwahiyo ukisema tuwatofautishe hawa kidogo nahitaji elimu yako hapa mkuu.
 
Kwa mujibu wa Katiba ya ACT ZZK atakuwa na madaraka yafuatato

"Kazi za Kiongozi Mkuu wa ACT-Tanzania

i) Atakuwa kiongozi mkuu wa chama kwenye mikutano mikuu ya chama Taifa, mkutano mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu.

ii) Atakuwa mkuu wa siasa, mshauri na mwelekezaji kwa viongozi wote na maafisa wa ACT-Tanzania

iii) Kuteua wajumbe watano wa Kamati Kuu kwa mujibu wa Katiba hii

iv) Atakuwa ndiye mtoa tamko rasmi kuhusu masuala ya sera na mtazamo wa chama

v) Atakuwa mtoa habari mahususi kwenye mkutano mkuu, Halmashauri Kuu na Kamati Kuu kuhusu hali ya kisiasa nchini na masuala mengine ya kitaifa na kimataifa.

vi) Atasimamia, kufunza na kutoa maelekezo kuhusu shughuli zote za ACT-Tanzania

vii) Iwapo kiongozi wa ACT-Tanzania hayupo kwa sababu yoyote ile basi Mwenyekiti wa chama Taifa atakuwa Kaimu kiongozi mkuu wa Chama.

viii) Iwapo kiti cha kiongozi mkuu wa Chama kitakuwa wazi kwa sababu ya kujiuzulu, kuondoka katika Chama, kuvuliwa uongozi au uanachama, maradhi yenye kuondoa uwezo wa kufanya kazi au kifo, utaratibu ulioelezwa katika

(vi) ya ibara ndogo hii utatumika kwa sharti kwamba Mkutano Mkuu Maalumu wa Taifa utaitishwa katika muda usiozidi miezi sita tangu kuwa wazi kwa kiti hicho kwa ajili ya kuchagua Kiongozi Mkuu wa Chama mwingine.

ix) Ataweza kuondolewa kwenye madaraka baada ya mapendekezo ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa azimio la Mkutano Mkuu wa Taifa
litakaloungwa mkono na theluthi mbili ya kura za wajumbe halali waliohudhuria na kupiga kura.

x) Atakuwa ni nuru na taswira ya ACT-Tanzania"

Si waseme tu kuwa yeye ndiye mwenyekiti na huyo wanayedai kuwa mwenyekiti ni makamu kwani shida ni nini
 
Si waseme tu kuwa yeye ndiye mwenyekiti na huyo wanayedai kuwa mwenyekiti ni makamu kwani shida ni nini

Mkuu Ayatollah zitto anaogopa kuambiwa ni mroho madaraka that's why kajipa cheo hicho. Yeye ndio act na act ndo yeye.
 
Siku chache zilizopita mwanasiasa kijana mwenye kupenda madaraka alitudhihilishia dhiri pasipo na shaka baada ya kuwa kiongozi mkuu wa ACT chama alichokianzisha kwa hisani ya CCM.Akiwa CDM alikuwa anaunyemelea uanyekiti wa chama sasa alivyoondoka CDM na kwenda kwenye genge lake ameenda mbali kwa kuanzisha cheo cha kiongozi mkuu wa chama kwa kuibadili katiba ya awali pamoja na rangi ya bendera.Cheo cha mwenyekiti kinakuwa hakina meno madaraka yote yapo kwa kiongozi mkuu yaani ameanzisha ufalme/usultani hadi kwenye vyama vya siasa.Je,hiyo ni sawa?
 
Huyu jamaa atawaua kwa presha.

Ni suala la muda, ZZK atafutika kwenye siasa za Tanzania. Huyu ni mbinafsi mpenda madaraka. Anaweza kufuatwa na vipofu na opportunists ambao wanafikiri wanaweza kupata ubunge kupitia ZZK!
 
Chama cha Ayatollah. Jamaa analoga balaa.Yaani kajimilikisha Chama Kikatiba halafu wapambe wake wanakata viuno vya maneno huku JF balaa
 
Kila baada ya topic moja inayofuata lazima inamuhusu ZZK.Jamaa nyota yake iko juu, kuna watu wanamapenzi na Zitto mpaka naogopa.
 
Sijawahi kuona chama cha siasa kuwa na mtu aliye na madaraka ya kumzidi mwenyekiti. Yaani ni kituko tupu. Hongera mfalme zitto
 
zittoact.jpg


MOJAWAPO ya matukio ya kisiasa yaliyotawala vyombo vya habari, mazungumzo ya kawaida na mitandao ya kijamii mwezi Machi mwaka huu ni kuzinduliwa rasmi kwa Chama cha ACT-Wazalendo. Uzinduzi wa chama hiki ulifanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam Machi 29, 2015.

Mambo mawili muhimu yametawala mjadala kuhusu kuzinduliwa kwa chama hiki. Jambo la kwanza ni kuhusu itikadi ya chama, ambayo ni ujamaa wa kidemokrasia. Baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa wamehoji uhalali na uhalisia wa chama hiki katika kuhuisha na kutekeleza siasa ya ujamaa katika mazingira ya dunia ya leo ambapo siasa za ubwanyenye zimetawala.

Jambo la pili ni muundo wa uongozi unaotumiwa na chama hiki. Tofauti na utaratibu uliozoeleka katika miundo ya uongozi ya vyama hapa nchini, ACT-Wazalendo kimekuja na muundo wenye Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama.

Katika makala ya leo ninajadili na kufafanua kuhusu dhana na msingi wa muundo wa uongozi wa ACT-Wazelendo. Nikipata fursa huko mbele nitajitahidi kufafanua dhana na msingi wa itikadi ya Demokrasia ya ujamaa kama inavyotumiwa na ACT-Wazalendo hasa katika mazingira ya Tanzania ya leo.

Jambo moja jema katika mjadala unaoendelea kuhusu ACT-Wazalendo ni kwamba angalau tumeanza kujadili kuhusu itikadi na mifumo ya uendeshaji wa vyama vya siasa, badala ya kila siku kujadili matukio ya kisiasa yanayotokea.

Mfumo wa uongozi wa ACT-Wazalendo unajumuisha Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti wa Chama. Kimsingi huu ndio mfumo wa uongozi unaotumiwa na vyama vya siasa katika nchi nyingi zilizomo katika Jumuiya ya Madola.

Kwa mfano, nchini Uingereza mfumo wa uongozi wa chama cha Conservatives unajumuisha Kiongozi wa Chama na Wenyeviti wawili. Kiongozi wa Chama cha Conservatives ni Waziri Mkuu wa sasa David Cameron wakati Grant Shapps na Lord Feldman ni wenyeviti wa chama hicho. Kiongozi wa Chama cha Liberal Democrats ni Nick Clegg wakati mwenyekiti wa chama (wanamuita Rais) ni Sal Brinton.

Mifano pia ipo mingi katika Bara la Afrika. Kwa mfano, Raila Odinga ni Kiongozi wa ODM nchini Kenya wakati Mwenyekiti wa Chama hicho ni Henry Kosgey. Nchini Afrika Kusini, Kiongozi wa Chama tawala cha ANC ni Jacob Zuma wakati Mwenyekiti wa chama hicho ni mwana mama Baleka Mbete, ambaye pia ni Spika wa Bunge la Afrika Kusini.

Sababu ya msingi ya kuwa na mfumo wa uongozi wa chama tofauti na mwenyekiti ni kuepuka kutengeneza chama dola. Moja ya matatizo yanayoikumba demokrasia barani Afrika ni ukweli kwamba mfumo wa uongozi wa vyama vya siasa ni wa kidola.

Hapa kwetu, kwa mfano, CCM ni chama dola kwa maana kwamba kimejipenyeza serikalini kutokana na muundo wake ambapo mwenyekiti wake ndiyo huyohuyo anakuwa kiongozi wa serikali. Huyu akimaliza kuendesha vikao vya Baraza la Mawaziri anahamia kuendesha vikao vya chama. Ni kwa sababu hii chama kinakuwa hakina uwezo wala mamlaka ya kuhoji utendaji wa serikali yake.

Matokeo ya muundo huo ndio yanayomfanya sasa Katibu Mkuu wa CCM kufanya kazi ya vyama vya upinzani ya kulalamika na kuikemea serikali yake barabarani kwa sababu anajua kwamba hawezi kuwa na nafasi hiyo ndani ya vikao vya chama kwa sababu huko serikali ndiyo inayoendesha chama.

Mfumo wa chama dola wa CCM hauna tofauti na vyama vingine. Ndiyo kusema vyama hivi navyo vitalazimika kuwa vyama dola mara vitakapoingia madarakani. Mfumo wa chama dola ni hatari kwa demokrasia kwa sababu hulazimisha watumishi wa umma kufanya kazi ya chama tawala badala ya kutumikia serikali kwa mujibu wa taaluma zao.

Kwa hiyo, msingi wa kuwa na mfumo wa uongozi wa chama sambamba na uenyekiti ni kuondoa udola katika chama cha siasa. Mfumo huu unatoa nafasi kwa chama kuweza kuhoji na kusimamia utendaji wa serikali yake bila chenyewe kujigeuza kuwa serikali. Hiki ndicho kilichofanyika Afrika Kusini ambapo baada ya kuona Rais Thabo Mbeki ameshindwa kusimamia sera za ANC katika serikali chama kiliamua kumuweka pembeni na hatimaye kumchagua Jacob Zuma kuwa Kiongozi wa Chama na baadaye Rais wa Afrika Kusini. Jambo hili lisingewezekana katika mfumo wa chama dola.

Kwa hiyo msingi wa ACT-Wazalendo kuwa na mfumo wa Kiongozi wa Chama sambamba na Mwenyekiti ni kugawanya majukumu ya kuendesha mfumo wa chama na kueneza itikadi na sera za chama kwa umma. Kwa mujibu wa Katiba ya ACT-Wazalendo, jukumu la msingi la Kiongozi wa Chama nje ya serikali ni kueneza itikadi, falsafa, misingi na sera za chama kwa umma. Ndiyo kusema kazi kubwa ya Kiongozi wa Chama itakuwa ni kuongoza jahazi la kuzunguka nchini katika kusaka kuungwa mkono na wananchi.

Jukumu la msingi la Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo ni kusimamia uendeshaji wa chama na taasisi zake. Yeye ndiye atakuwa mwenyekiti wa vikao vyote vya maamuzi ndani ya chama ikiwemo Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu.

Siku ACT-Wazalendo ikichaguliwa na kuunda serikali jukumu la Kiongozi wa Chama litakuwa ni kusimamia uendeshaji wa serikali na kuhakikisha kwamba serikali inatekeleza sera za chama kikamilifu na atatoa taarifa ya utekelezaji wa sera katika vikao vya chama vitakavyoendeshwa na Mwenyekiti wa chama.

Mgawanyo wa majukumu ya Kiongozi Mkuu na Mwenyekiti wa Chama yanajitokeza pia katika mamlaka za uteuzi. Kwa mfano, Kiongozi Mkuu wa Chama ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa wenyeviti wa kamati za kisera na washauri wa chama. Mwenyekiti kwa upande wake ana mamlaka ya kupendekeza uteuzi wa watendaji wa chama kama vile manaibu katibu wakuu.

Kwa hiyo, pamoja na kwamba kimuundo Kiongozi wa Chama ndiye mwenye mamlaka zaidi ya kiuongozi ndani ya ACT-Wazalendo, mgawanyo wa nafasi mbili za Kiongozi wa Chama na Mwenyekiti ni wa kimajukumu zaidi kuliko kimamlaka.

Tunaamini kwamba kwa kuwa na mfumo wa uongozi huu ni hatua muhimu ya kujenga chama cha siasa kisicho chama dola. Aidha mfumo huu utahakikisha kwamba Mwenyekiti wa chama anakuwa na nafasi ya kutosha ya kujenga na kusisimamia uendeshaji wa mifumo ya chama.

CHANZO: Raia mwema
 
Back
Top Bottom