Kazi ya kuelezea mazuri ya awamu ya tano inahitaji weledi na sio kuongozwa na kiburi.

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,489
13,608
Katika hotuba mojawapo ya Mwalimu Nyerere, anasikika akiongelea idadi ya wataalam aliokuwa nao wakati nchi ikianza safari ya kuwa huru mwaka 1961.

Desemba mwaka huu imetimia miaka 55 tangu safari hiyo ianze. Ukizitazama picha za mitaa ya Dar, Arusha na Mwanza ambazo zilipigwa siku za mwanzoni za Tanganyika huru halafu ukazilinganisha na hizi za sasa, tofauti ni kubwa sana.

Mengi mema na mabaya yamefanyika ndani ya uongozi wa awamu zote tano tangu uhuru. Mpaka tumefikia hii awamu ya tano, kujifunza na kukosea kumekuwa ndio utaratibu wa maisha binafsi na yale ya kiuongozi.

Wakati mwaka wa kwanza wa awamu ya tano ukiwa umemalizika, yapo mema yenye kustahili kupewa nafasi kubwa na muhimu na mabaya pia.

Lakini hii ni Tanzania ambayo walioelimika na wanaoendelea kuelimika ni wengi sana. Uwezo wa watu kuhoji na kujenga hoja, ni mkubwa sana.

Hivyo kazi ya kuelezea kwa ufasaha malengo ya mipango ya serikali ya muda mfupi na mrefu, isifanyike kwa kuongozwa na kile kiburi cha madaraka. Bali ifanyike kwa weledi mkubwa kwani anayeelezewa mipango hiyo, anapoweza kushawishika katika kuikubali ndipo baraka zake zinapoweza kufanikisha malengo ya serikali.

Ikiwa wakati wa uhuru madaktari hawakuzidi watano, leo hii tunao wengi sana, unapojenga hoja kama mtu wa serikali basi ujue upana wa hadhira inayoupokea ujumbe wako kwa wakati mmoja.

Unapoelezea mipango ya wizara kwa mfano wa sheria, ujue kwamba kuna wanasheria wengi tu wanaoandaliwa vyuoni na wengine wapo kazini, basi na ujenge hoja huku ukitambua mrejesho utakaoupata kutoka kwa wadau wengi wa sekta ya sheria.

Afrika imekuwa na tatizo la wenye kutakiwa kuelezea wakifanyacho kwa niaba ya wananchi, kushindwa kuwashawishi watu wengi juu ya kile wakifanyacho.

Mwaka 2017 na uwe ni mwaka ambao mipango na mikakati ya kiserikali itakawasilishwa kwa wananchi, katika namna ambazo zitaendana na wingi wa watu wenye weledi katika sekta fulani.

Kazi isiishie katika kuwasilisha ripoti fulani bali muwasilishaji atambue umuhimu wa weledi katika uwasilishaji wake ili apunguze manung'uniko ya walengwa na wasio walengwa wa kile alichokiwasilisha.

Mungu atuongoze wana Jamii Forum ili tuumalize mwaka 2016 kwa amani na tuuanze mwaka 2017 kwa matarajio chanya katika maisha yetu.

Mungu atubariki sote.
 
Kumbuka kutimiza wajibu wako kwanza. Wakati unasubiri imshinde, unaweza wewe kutumbuliwa na ofisi yako.
Kwa sisi tumezoea tukishidwa,tunakubali makosa yako mnasonga mbele,lakini wanasiasa wetu hawakubaligi hadi nchi iingie gizani,hata upinzani mwangalie mbowe kama atakuli akifanya makosa,huwezi ukawa wewe dreva, kondakta ,mpiga debe, fundi ukafanikiwa na basi lako,namsikia anasema sekta ya utalii itakuwa kwa kununua ndege,sijui lini wadau walishirikishwa kuona kama ni kweli,serikali haina watalii watalii ni wa makampuni,kama wenyewe wanasema tuondoe VAT halafu wewe unasema tusitoe tununue ndege time will tell.
 
Naomba kuuliza swali nje ya mada'....
Kwani kesho mkemia atahutubia taifa hili?
Mkuu, sina uhakika, tulizoea BWM na JMK kuwasikia wakitupa mrejesho wa yote yaliyofanyika mwaka mzima.

Jamaa yupo na ndugu zake kijijini, sina hakika kama anapendelea utaratibu huo.
 
Kwa sisi tumezoea tukishidwa,tunakubali makosa yako mnasonga mbele,lakini wanasiasa wetu hawakubaligi hadi nchi iingie gizani,hata upinzani mwangalie mbowe kama atakuli akifanya makosa,huwezi ukawa wewe dreva, kondakta ,mpiga debe, fundi ukafanikiwa na basi lako,namsikia anasema sekta ya utalii itakuwa kwa kununua ndege,sijui lini wadau walishirikishwa kuona kama ni kweli,serikali haina watalii watalii ni wa makampuni,kama wenyewe wanasema tuondoe VAT halafu wewe unasema tusitoe tununue ndege time will tell.
Sidhani kama dereva ni yeye konda ni yeye na mpiga debe ni yeye. Ni maneno ya mtaani ambayo hakuna anayeweza kuyathibitisha.
Kununua ndege ni jambo jema, mkuu watalii walikuwa wanakwenda na ndege mpaka Kenya halafu wanakuja Tanzania, walikuwa wanaacha fedha Kenya kwanza halafu makombo yanakuja kwetu.
Nadhani umeona picha ya kadi ya krismasi ya Rais wa Kenya, inaonyesha mlima Kilimanjaro kwa nyuma yake. Maana yake ni kwamba jirani zetu wameshasoma mchezo na kutambua tumeshaamka kwenye akili za kibiashara.
Haya magumu ya sasa ni ya muda tu, yanatengenezwa mazingira ya sisi watanzania kuweza kufaidika na fursa tulizonazo humu nchini.
 
Sidhani kama dereva ni yeye konda ni yeye na mpiga debe ni yeye. Ni maneno ya mtaani ambayo hakuna anayeweza kuyathibitisha.
Kununua ndege ni jambo jema, mkuu watalii walikuwa wanakwenda na ndege mpaka Kenya halafu wanakuja Tanzania, walikuwa wanaacha fedha Kenya kwanza halafu makombo yanakuja kwetu.
Nadhani umeona picha ya kadi ya krismasi ya Rais wa Kenya, inaonyesha mlima Kilimanjaro kwa nyuma yake. Maana yake ni kwamba jirani zetu wameshasoma mchezo na kutambua tumeshaamka kwenye akili za kibiashara.
Haya magumu ya sasa ni ya muda tu, yanatengenezwa mazingira ya sisi watanzania kuweza kufaidika na fursa tulizonazo humu nchini.
Kilimanjaro airport kuna ndege nyingi zinashuka bila kupitia nairobi,kuna kipindi abiria hamna hadi safari wanapunguza,ishu siyo ndege,serikali haijltangazi mbuha zake kama kenya,wadau wapo na hawasikilizwi.
 
Katika hotuba mojawapo ya Mwalimu Nyerere, anasikika akiongelea idadi ya wataalam aliokuwa nao wakati nchi ikianza safari ya kuwa huru mwaka 1961.

Desemba mwaka huu imetimia miaka 55 tangu safari hiyo ianze. Ukizitazama picha za mitaa ya Dar, Arusha na Mwanza ambazo zilipigwa siku za mwanzoni za Tanganyika huru halafu ukazilinganisha na hizi za sasa, tofauti ni kubwa sana.

Mengi mema na mabaya yamefanyika ndani ya uongozi wa awamu zote tano tangu uhuru. Mpaka tumefikia hii awamu ya tano, kujifunza na kukosea kumekuwa ndio utaratibu wa maisha binafsi na yale ya kiuongozi.

Wakati mwaka wa kwanza wa awamu ya tano ukiwa umemalizika, yapo mema yenye kustahili kupewa nafasi kubwa na muhimu na mabaya pia.

Lakini hii ni Tanzania ambayo walioelimika na wanaoendelea kuelimika ni wengi sana. Uwezo wa watu kuhoji na kujenga hoja, ni mkubwa sana.

Hivyo kazi ya kuelezea kwa ufasaha malengo ya mipango ya serikali ya muda mfupi na mrefu, isifanyike kwa kuongozwa na kile kiburi cha madaraka. Bali ifanyike kwa weledi mkubwa kwani anayeelezewa mipango hiyo, anapoweza kushawishika katika kuikubali ndipo baraka zake zinapoweza kufanikisha malengo ya serikali.

Ikiwa wakati wa uhuru madaktari hawakuzidi watano, leo hii tunao wengi sana, unapojenga hoja kama mtu wa serikali basi ujue upana wa hadhira inayoupokea ujumbe wako kwa wakati mmoja.

Unapoelezea mipango ya wizara kwa mfano wa sheria, ujue kwamba kuna wanasheria wengi tu wanaoandaliwa vyuoni na wengine wapo kazini, basi na ujenge hoja huku ukitambua mrejesho utakaoupata kutoka kwa wadau wengi wa sekta ya sheria.

Afrika imekuwa na tatizo la wenye kutakiwa kuelezea wakifanyacho kwa niaba ya wananchi, kushindwa kuwashawishi watu wengi juu ya kile wakifanyacho.

Mwaka 2017 na uwe ni mwaka ambao mipango na mikakati ya kiserikali itakawasilishwa kwa wananchi, katika namna ambazo zitaendana na wingi wa watu wenye weledi katika sekta fulani.

Kazi isiishie katika kuwasilisha ripoti fulani bali muwasilishaji atambue umuhimu wa weledi katika uwasilishaji wake ili apunguze manung'uniko ya walengwa na wasio walengwa wa kile alichokiwasilisha.

Mungu atuongoze wana Jamii Forum ili tuumalize mwaka 2016 kwa amani na tuuanze mwaka 2017 kwa matarajio chanya katika maisha yetu.

Mungu atubariki sote.
Nasikia hadi leo hii bado hujapewa hata uenyekiti wa nyumba kumi
 
Katika hotuba mojawapo ya Mwalimu Nyerere, anasikika akiongelea idadi ya wataalam aliokuwa nao wakati nchi ikianza safari ya kuwa huru mwaka 1961.

Desemba mwaka huu imetimia miaka 55 tangu safari hiyo ianze. Ukizitazama picha za mitaa ya Dar, Arusha na Mwanza ambazo zilipigwa siku za mwanzoni za Tanganyika huru halafu ukazilinganisha na hizi za sasa, tofauti ni kubwa sana.

Mengi mema na mabaya yamefanyika ndani ya uongozi wa awamu zote tano tangu uhuru. Mpaka tumefikia hii awamu ya tano, kujifunza na kukosea kumekuwa ndio utaratibu wa maisha binafsi na yale ya kiuongozi.

Wakati mwaka wa kwanza wa awamu ya tano ukiwa umemalizika, yapo mema yenye kustahili kupewa nafasi kubwa na muhimu na mabaya pia.

Lakini hii ni Tanzania ambayo walioelimika na wanaoendelea kuelimika ni wengi sana. Uwezo wa watu kuhoji na kujenga hoja, ni mkubwa sana.

Hivyo kazi ya kuelezea kwa ufasaha malengo ya mipango ya serikali ya muda mfupi na mrefu, isifanyike kwa kuongozwa na kile kiburi cha madaraka. Bali ifanyike kwa weledi mkubwa kwani anayeelezewa mipango hiyo, anapoweza kushawishika katika kuikubali ndipo baraka zake zinapoweza kufanikisha malengo ya serikali.

Ikiwa wakati wa uhuru madaktari hawakuzidi watano, leo hii tunao wengi sana, unapojenga hoja kama mtu wa serikali basi ujue upana wa hadhira inayoupokea ujumbe wako kwa wakati mmoja.

Unapoelezea mipango ya wizara kwa mfano wa sheria, ujue kwamba kuna wanasheria wengi tu wanaoandaliwa vyuoni na wengine wapo kazini, basi na ujenge hoja huku ukitambua mrejesho utakaoupata kutoka kwa wadau wengi wa sekta ya sheria.

Afrika imekuwa na tatizo la wenye kutakiwa kuelezea wakifanyacho kwa niaba ya wananchi, kushindwa kuwashawishi watu wengi juu ya kile wakifanyacho.

Mwaka 2017 na uwe ni mwaka ambao mipango na mikakati ya kiserikali itakawasilishwa kwa wananchi, katika namna ambazo zitaendana na wingi wa watu wenye weledi katika sekta fulani.

Kazi isiishie katika kuwasilisha ripoti fulani bali muwasilishaji atambue umuhimu wa weledi katika uwasilishaji wake ili apunguze manung'uniko ya walengwa na wasio walengwa wa kile alichokiwasilisha.

Mungu atuongoze wana Jamii Forum ili tuumalize mwaka 2016 kwa amani na tuuanze mwaka 2017 kwa matarajio chanya katika maisha yetu.

Mungu atubariki sote.
Nasikia hadi leo hii bado hujapewa hata uenyekiti wa nyumba kumi
 
Kilimanjaro airport kuna ndege nyingi zinashuka bila kupitia nairobi,kuna kipindi abiria hamna hadi safari wanapunguza,ishu siyo ndege,serikali haijltangazi mbuha zake kama kenya,wadau wapo na hawasikilizwi.
Hilo ni suala muhimu kufanyiwa kazi, kwani ikiwa mipango ni kuwa na ndege sita mpya. Ni lazima matangazo ya mbuga yapewe kipaumbele.

Lakini kuna tangazo la klabu ya sunderland ambalo inasemekana watu walitengeneza mazingira ya upigaji. Kabla ya mechi za premier league wachezaji wa timu hiyo huvaa fulana zinazowakaribisha watalii nchini mwetu.

Kuna fursa kwenye utalii ni suala la wizara kujipanga kwa dhati.
 
Hilo ni suala muhimu kufanyiwa kazi, kwani ikiwa mipango ni kuwa na ndege sita mpya. Ni lazima matangazo ya mbuga yapewe kipaumbele.

Lakini kuna tangazo la klabu ya sunderland ambalo inasemekana watu walitengeneza mazingira ya upigaji. Kabla ya mechi za premier league wachezaji wa timu hiyo huvaa fulana zinazowakaribisha watalii nchini mwetu.

Kuna fursa kwenye utalii ni suala la wizara kujipanga kwa dhati.
Tatizo lililoko hii nchi ni wadau hawashirikishwi wanaonekana hawafai,mifano ni hii ya utalii,na kuna kilimo haiwezekani tunasema hii nchi asilimia 60 mpaka 70 wanategemea kilimo halafu shule za msingi hamna somo la kilimo,hao asilimia 60 hadi 70 wanarudi kwenye kilimo na hawana ujuzi,sasa hivi kuna ruzuku ya mbegu serikali inalipa 30 % 70% mkulima kwa baadhi za wilaya,lakini ukienda mbegu zenye ruzuku ni ghali kuliko zisizo na ruzuku,sisi waafrika kamatumelogwa.
 
Sidhani kama dereva ni yeye konda ni yeye na mpiga debe ni yeye. Ni maneno ya mtaani ambayo hakuna anayeweza kuyathibitisha.
Kununua ndege ni jambo jema, mkuu watalii walikuwa wanakwenda na ndege mpaka Kenya halafu wanakuja Tanzania, walikuwa wanaacha fedha Kenya kwanza halafu makombo yanakuja kwetu.
Nadhani umeona picha ya kadi ya krismasi ya Rais wa Kenya, inaonyesha mlima Kilimanjaro kwa nyuma yake. Maana yake ni kwamba jirani zetu wameshasoma mchezo na kutambua tumeshaamka kwenye akili za kibiashara.
Haya magumu ya sasa ni ya muda tu, yanatengenezwa mazingira ya sisi watanzania kuweza kufaidika na fursa tulizonazo humu nchini.
HAPO KWENYE NYEKUNDU INAONYESHA HATA HAMUJUI JIOGRAFIA VIZURI. RUDI KWENYE PICHA UNAYOISEMA ANGALIA KAMA MLIMA UNA VILELE VIWILI AU KIMOJA, NDIPO USEME NI KILIMANJARO
 
Pole sana rafiki yangu kwa kazi isiyo na malipo kwani ilipo anzia kujipendekeza naona jamaa kakuchunia
Mkuu kwa sababu wewe unajipendekeza unafikiri kila mtu ni aina yako. Wengine humu tunapenda kujenga hoja na kusoma jinsi ambavyo watu wanajenga hoja.

Bwana mdogo Mmawia ungenifahamu usingeandika mawazo ya kipunguani kama haya unayoyaandika mara kwa mara.
 
HAPO KWENYE NYEKUNDU INAONYESHA HATA HAMUJUI JIOGRAFIA VIZURI. RUDI KWENYE PICHA UNAYOISEMA ANGALIA KAMA MLIMA UNA VILELE VIWILI AU KIMOJA, NDIPO USEME NI KILIMANJARO
Issenye unaanzisha mada nyingine juu ya mada inayoendelea. Logic ya picha ile ya Kenyatta umeielewa au unaongea vitu ambavyo huvifahamu?.
 
Kumbuka kutimiza wajibu wako kwanza. Wakati unasubiri imshinde, unaweza wewe kutumbuliwa na ofisi yako.

..sasa unapojibu wachangiaji wenzako namna hii huoni kwamba unaonyesha KIBURI?

..nimeona kuna mahali umeandika kwamba mchangiaji mwenzako ana mawazo ya kipunguani.

..je huo ni uungwana?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom