Kazi ya Kikwete ni kuhudhuria kila msiba?

Phillemon Mikael

Platinum Member
Nov 5, 2006
10,529
8,614
mazishi

waombolezaji+1.JPG

waombolezaji kinamama msibani
wakuu+wa+wilaya+za+Kilimanjaro.JPG

Wakuu wa wilaya za Kilimanjaro wakiwa msibani
wakuu+wa+wilaya+za+mkoa+wa+Kilimanjaro.JPG


baadhi ya waombolezaji​

Habari na picha na
Dixon Busagaga,
Same
RAIS Jakaya Kikwete jana ameongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa mnikulu marehemu Rajabu Kianda aliyefariki dunia Februari 7 mwaka huu kwa ugonjwa wa shinikizo la damu.

Akizungumza baada ya mazishi yaliyofanyika kijiji cha Kangokoro kata ya Kihuria wilayani Same,Rais Kikwete aliitaka familia ya marehemu kuwa wavumilivu na moyo wa subira hasa katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.

Naye katibu mkuu wa Ikulu Bw Michael Mwanda akisoma wasifu wa wa marehemu Kianda alimtaja marehemu kuwa alikuwa ni mchapa kazi hodari na kwamba ni mfano wa kuigwa..

Kwa upande wake baba mdogo wa marehemu ,Bw Said Nyika akitoa neno la familia ameishukuru serikali kwa msaada iliyotoa wakati wa matibabu ya ndugu yao hadi mauti yalipomfika.

Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo wakuu wa wilaya,wabunge, viongozi wa vyama vya siasa, taasisi mbali mbali za serikali na zisizo za serikali.

Marehemu Kianda aliyefariki dunia Februari 7 katika hospitali ya Muhimbili ,amezikwa katika makaburi ya familia yaliyopo eneo la Mashine kata ya Kihurio na ameacha mjane na watoto sita.


SOURCE: Michuzi Blog
 
yes me nadhani ni moja ya jukumu kubwa la rais....sio misiba tu kuwajulia hali wagonjwa pia katika hospitali mbalimbali
 
pamoja na madhaifu aliyoyasema Semenya, kweli Kikwete ni Bigwa wa kuudhulia misiba, anajitahidi, sijui ni sifa ama ni ujiko.
 
Rais lazima awe karibu na watu ni sehemu ya majukumu yake, kama kuhudhuria kwa raisi msibani wewe kumekukweza, waliofiwa, jamaa na marafiki wanafarajika
 
Rais lazima awe karibu na watu ni sehemu ya majukumu yake, kama kuhudhuria kwa raisi msibani wewe kumekukweza, waliofiwa, jamaa na marafiki wanafarajika
Sio kila msiba ndugu! mingine kama kweli ameguswa, basi awatume viongozi wake wasaidizi kama vile DC, RC n.k wamwakilishe. Anatuletea adha kubwa sana ya foleni hasa wakazi wa Dar.

Wajua tena msafara wa raisi ukipita, magari mengine yote husibiri kwa masaa zaidi mawili kwenye foleni. Madhara yake hata kiuchumi ni makubwa pia!
 
Rais lazima awe karibu na watu ni sehemu ya majukumu yake, kama kuhudhuria kwa raisi msibani wewe kumekukweza, waliofiwa, jamaa na marafiki wanafarajika


rais hakuwa na sababu ya kwenda kuzika same kwa huyu afisa usalama aliyefariki..kwani kitendo cha rais na mkewe kufika pale mikocheni nyumbani siku ya kuaga mwili wa marehemu...na kwakuwa inajulikana rais ni mtu mwenye mamlaka na kazi nyingi....kile kitendo pekee kilitosha kuonesha upendo wake kwa maafisa wake wanaomlinda na kumsaidia kazi......lakini bado tena amesafiri na kutumia siku nyingine nzima kwenda kuzika same......urais ni cheo kikuu sana ....ingetosha kumtuma mkuu wa mkoa au waziri wa utawala bora ..amuwakilishe kama kweli aliona ...inafaa.....

the president wants to win peoples emmotions at all time....that may not be possibe!!
 
pamoja na madhaifu aliyoyasema Semenya, kweli Kikwete ni Bigwa wa kuudhulia misiba, anajitahidi, sijui ni sifa ama ni ujiko.

Watu bwana!!! Kweli uongozi kazi, hivi Rais kuhudhuria msiba ni kutaka sifa? Kwakweli unachekesha. Rais ni kama mtanzania mwingine yeyote ambaye anaguswa na kifo cha mtu ambaye ama alikuwa anafahamiana naye kwa karibu au ni ndugu au rafiki wa karibu bila kujali nafasi yake serikalini. Kama ambavyo wewe huwa unaomba Ruhusa ili kwenda kwenye msiba na yeye ana nafasi ya kufanya hivyo. Mbona tupo hivyo watanzania?? Tunaacha kuangalia mambo ya msingi tunaanza kujadili mambo ambayo ni too personal!! Wewe unafahamu Kikwete na huyo bwana wanamahusiano gani? Tuache ushabiki unaopitiliza kiasi. hata kama ni kumchukia lakini siyo kihivyo.
 
yaani huyu anaona aibu tu kwenda ngomani lakini ingekuwa amri yake aaaah ..ngomanai kama kawaaa
 
Kuna rafiki yangu ni bingwa wa hesabu na siku moja nilikuwa nae ktk porojo zake akaanza kukokotoa mambo yanavyofanyika pale ikulu na Mh wetu, akasema tufanye pale ikulu kuna masomo 5 na kama yeye angekuwa mwalimu angetowa marks hizi, sijui mimi na wewe tungetowa zipi?
1. Kuhudhuria misiba na mazishi - 86%
2.Safari za Nje -89%
3. Safari za Ndani- 61%
4.Kukaa ofisini- 15%
5. Msimamo katika vita ya ufisadi- 05%
 
Watu bwana!!! Kweli uongozi kazi, hivi Rais kuhudhuria msiba ni kutaka sifa? Kwakweli unachekesha. Rais ni kama mtanzania mwingine yeyote ambaye anaguswa na kifo cha mtu ambaye ama alikuwa anafahamiana naye kwa karibu au ni ndugu au rafiki wa karibu bila kujali nafasi yake serikalini. Kama ambavyo wewe huwa unaomba Ruhusa ili kwenda kwenye msiba na yeye ana nafasi ya kufanya hivyo. Mbona tupo hivyo watanzania?? Tunaacha kuangalia mambo ya msingi tunaanza kujadili mambo ambayo ni too personal!! Wewe unafahamu Kikwete na huyo bwana wanamahusiano gani? Tuache ushabiki unaopitiliza kiasi. hata kama ni kumchukia lakini siyo kihivyo.

hakuwa na sababu ya msingi kusafiri kwenda same kuhudhuria msiba ambao angeweza kumtuma mwakilishi na yeye akatulia ofisini kufanya kazi.ndo shida ya kula miguu ya kuku wakati wa utoto madhara yake ndo hayo sasa yanaonekana ukubwani..
 
Kuna rafiki yangu ni bingwa wa hesabu na siku moja nilikuwa nae ktk porojo zake akaanza kukokotoa mambo yanavyofanyika pale ikulu na Mh wetu, akasema tufanye pale ikulu kuna masomo 5 na kama yeye angekuwa mwalimu angetowa marks hizi, sijui mimi na wewe tungetowa zipi?
1. Kuhudhuria misiba na mazishi - 86%
2.Safari za Nje -89%
3. Safari za Ndani- 61%
4.Kukaa ofisini- 15%
5. Msimamo katika vita ya ufisadi- 05%

kukaa ofisini ni 1.2%
safari za nje 98.7
kuhudhuria mazishi ni 100%
 
hakuwa na sababu ya msingi kusafiri kwenda same kuhudhuria msiba ambao angeweza kumtuma mwakilishi na yeye akatulia ofisini kufanya kazi.ndo shida ya kula miguu ya kuku wakati wa utoto madhara yake ndo hayo sasa yanaonekana ukubwani..

juzi alitumia masaa mawili kwenda kuaga marehemu mikocheni ....jana siku nzima hajafanya kazi...kisa anazika....,ukishakuwa rais kuna vitu unapoteza...kimoja ni kuwa hata muda wa rais ni mali yetu!..asiufisadi muda wetu tuliompa! alaaa!
 
Kuhudhuria misiba hakudetermine ubora au ubaya wa kiongozi,hiyo ni culture ya kawaida kabisa,hata kama angeudhuria kila msiba wa wilaya ya Ilala sisi tunachojali anaifanyia nini Tanzania.Sometimes muwe mnapunguza kauli za kubeza.
 
Back
Top Bottom