Phillemon Mikael
Platinum Member
- Nov 5, 2006
- 10,529
- 8,614
mazishi
waombolezaji kinamama msibani
Wakuu wa wilaya za Kilimanjaro wakiwa msibani
baadhi ya waombolezaji
SOURCE: Michuzi Blog
waombolezaji kinamama msibani
Wakuu wa wilaya za Kilimanjaro wakiwa msibani
baadhi ya waombolezaji
Habari na picha na
Dixon Busagaga,
Same
RAIS Jakaya Kikwete jana ameongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa mnikulu marehemu Rajabu Kianda aliyefariki dunia Februari 7 mwaka huu kwa ugonjwa wa shinikizo la damu.
Dixon Busagaga,
Same
RAIS Jakaya Kikwete jana ameongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa mnikulu marehemu Rajabu Kianda aliyefariki dunia Februari 7 mwaka huu kwa ugonjwa wa shinikizo la damu.
Akizungumza baada ya mazishi yaliyofanyika kijiji cha Kangokoro kata ya Kihuria wilayani Same,Rais Kikwete aliitaka familia ya marehemu kuwa wavumilivu na moyo wa subira hasa katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao.
Naye katibu mkuu wa Ikulu Bw Michael Mwanda akisoma wasifu wa wa marehemu Kianda alimtaja marehemu kuwa alikuwa ni mchapa kazi hodari na kwamba ni mfano wa kuigwa..
Kwa upande wake baba mdogo wa marehemu ,Bw Said Nyika akitoa neno la familia ameishukuru serikali kwa msaada iliyotoa wakati wa matibabu ya ndugu yao hadi mauti yalipomfika.
Mazishi hayo pia yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali wakiwemo wakuu wa wilaya,wabunge, viongozi wa vyama vya siasa, taasisi mbali mbali za serikali na zisizo za serikali.
Marehemu Kianda aliyefariki dunia Februari 7 katika hospitali ya Muhimbili ,amezikwa katika makaburi ya familia yaliyopo eneo la Mashine kata ya Kihurio na ameacha mjane na watoto sita.
SOURCE: Michuzi Blog