Kazi nzito na nyepesi aliyonayo Tundu Lissu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,587
215,179
KAZI NZITO NA NYEPESI ALIYONAYO ANTIPHAS;

Huyu Jamaa anaweza kuwa na mzigo mzito sana ama mwepesi kuwafuta WATANZANIA machozi, na kuijenga TANZANIA mpya baada ya kuwaongoza kupata uhuru kwa Awamu ya pili.

Awamu hii ya pili ikiwa ni uhuru kutoka kwa kikundi cha watu waafrika wenzetu (The so called Elite) wanaojiaminisha na kujihakikishia wanabaki madarakani milele iwe hata kwa goli la mkono japo wamechokwa na wameshindwa kazi ya kuleta matunda ya Uhuru kwa kila mtanzania.

ugumu unakuja vipi..

ugumu unakuja pale ambapo kila mtanzania ambaye anataka mabadiliko ameelekeza masikio na matumaini yake kwa huyu bwana (Masiah/Mkombozi). Wote wakiamini kuwa atakuwa MTATUZI wa matatizo yao , iwe kisheria katika haki na uhuru wa kujieleza, kiuchumi na hata kielimu, Elimu ambayo haina mashiko ,imepitwa na wakati.

Urahisi uko wapi..

Matumaini na matarajio haya MAKUBWA yaweza kuonekana ni mambo yanayompa MZIGO MZITO mtu mmoja, lakini kiukweli inaweza kuwa rahisi kwake kwani ana sifa sifutazo;

1.Ni mtu anayeifahamu vyema historia sio tu ya Tanzania bali hata huko kwingineko duniani.

2.Anayajua vyema matukio na mambo mengi mbalimbali YALIYOPITA kwa kina na kwa mifano hai kitu kinachomjengea wezo mkubwa wa kutabiri YAJAYO.

3. Anayafahamu vyema matatizo ya Taifa hili kama vile sababu za kutonufaishwa na mali asili na rasilimali zetu, mikataba ya kilaghai, kero za muungano ambazo zimekuwa zikifunikwa na suluhu zake, sababu za kufeli kwa sera mbalimbali kama sera za kupambana na wahujumu uchumi kipindi cha Sokoine.

Anayafahamu maatizo hivyo hatapata taabu aanzie wapi. Kufahamu chanzo cha tatizo ni mwanzo mzuri wa kulitatua.

Hii ni tofauti kabisa na wengine ambao wamekuwa wakionesha nia ya kutaka kutuongoza kutatua matatizo ili hali mpaka leo hii wanauliza hawajui ni kwanini sisi ni masikini, hawajui fedha zinaibwaje ingawa wamehudumu ndani ya serikali hii kwa miongo kadhaa tena ndani ya baraza la maamuzi. Unaomba vipi kazi usiyoifahamu kwa undani? Sidhani kama huu ni wakati wa kujaribu wakati Taifa linahitaji matibabu liko mahututi?

4. Anauchukia na ana hofu ya UTAWALA wa MABAVU usiofuata sharia kwani anajua madhara yake, amekuwa akisisitiza utawala wa sharia, uhuru wa maoni, malumbano ya hoja . Amekuwa akitoa na kulaani kwa mifano mingi ya tawala zisizojali utu na njia bora za kutatua matatizo ya jamii kama akina Stalin, Hitler pamoja na oparesheni za akina Edward sokoine japo zlikuwa na nia njema.

5. Sio mnafiki, ni msemakweli na anao ujasiri wa kumkosoa, kumpinga ama kumsahihisha mtu waziwazi na bado akawa anamhusudu.

Amekuwa akikosoa waziwazi baadhi ya viongozi wanaosifika na kukumbukwa Mfano Mwalimu Nyerere ,Sokoine, Kikwete n.k. Hii ni ishara ya kiongozi mwenye uthubutu na muwazi pale unapokosea bila kubaki na chuki moyoni.

6. Ni mbobezi wa sharia na mtetezi wa haki , usawa kwa makundi yote iwe waliokuwa na vyama ama wasiokuwa navyo.
Ni wazi kuwa taifa baada ya uhuru linahitaji kuwa na mazingira yanayomfanya mwananchi ajione huru na mwenye haki juu ya rasilimali za nchi yake tofauti na iliyozoeleka sasa ambapo huwezi kuwa hata kiongozi wa ofisi ya umma pasipojuwa mshabiki wa chama kilichopo madarakani.

Taifa ni pana, lisiishie tu kwenye uchadema na uccm. wapo wasiopenda kujiunga na vyama

7. Amekuwa ni kiunganishi cha makundi mbalimbali licha ya tofauti za kiimani, kitamaduni, kiitikadi hata mbinu. Mfano amekuwa mtetezi wa wazanzibari wakiwemo masheikh wa uhamsho , amekuwa akiwaheshimu pia walioko chama tofauti nay eye akiwaita kwa majina kaka yangu, dada yangu ama ndugu yangu. Hiyo ni ishara ya kuwa ni kama kielelzo na kiunganishi cha UDUGU uliokwisha kuanza kupotezwa na chuki.

8. Sio kigeugeu, misimamo yake dhidi ya haki na usawa haibadiliki tangu akiwa shule hata alipoianza kazi yake rasmi miaka kibao iliyopita licha ya kubatizwa majina mbalimbali kama vile MCHOCHEZI.tangu miaka ya 90 anafahamika kama mtetezi wa wanyonge akiwaigania mamia ya wanakijiji dhidi ya wawekezaji waonevu walikaribishwa na viongozi walafi waliokuwa madarakani.

9. kutokana na kuwa shupavu katika kuusimamia ukweli , hivyo ni mtu ambaye hafungwi na nidhamu ya unafiki wa kumuonea haya usoni yeyote iwe ni mtu mkubwa kiasi gani. Hana deni la kulipa fadhila hivyo ni rahisi kwake kushuhulika na masuala yote ya ufisadi bila kubagua chambo na kuwaacha wakubwa.

MWISHO:

Pamoja na sifa hizi na nyingine nyingi alizonazo, tunamwombea na tunamsihi awe na MSAMAHA ,kwa yeyote anaeyesoma alama za nyakati anakubaliana nami kuwa huu ni wakati wa kujenga upya Taifa .

Na Taifa haliwezi kujengwa kwa kuendeleza gurudumu la VISASI bali kwa waliojiona wana haki sana kujishusha na kutubu walipokosea na wale walioonewa kusamehe kisha kuketi meza moja kujenga upya na kutibu majeraha ya TAIFA TANZANIA na AFRIKA kwa ujumla

1568201872933.jpeg
 
Naunga mkono hoja, huyu TL atatuungasha na kuturudisha katika umoja na uzalendo tofauti na huyu wa sasa anaetugawa na kutueneza chuki ndani ya mioyo yetu. Jambo la kupendelea chama chake kifanye mikutano na kunyima wenzake ni chuki kubwa anayosambaza magu upande wa pili na ndiyo maana hata ndege ikishikwa watu wanashngilia .

Magu hatufai 2020.
 
Wengine wanasema ni ngumu sana kuivurusha CCM madarakani kwa sanduku la kura bila kujali itasimamisha mawe au watu ili yapigiwe kura....

Lakini ukweli mchungu kwa wenzetu hawa wanaosimama ktk imani hii ni kuwa, KILA KITU KINA NYAKATI NA MAJIRA yake bila kujali ni kitamu ama kichungu; kinapendeza au kuchukiza kiasi gani....

MAJIRA na NYAKATI zikifika huondoka na hufa na watu hushangaa na kujiuliza limewezekanaje hili....!!???

Nani alikuwa anajua kuwa Robert Mugabe angekufa juzi?

Nani alijua kuwa huyu anayeabudiwa na baadhi yetu kama "BABA WA TAIFA" hayati Mwl Julius K. Nyerere angekufa na kuoza ardhini?

Hivi kwa waliokuwepo enzi zile za KANU ya Kenya chini ya mtu aliyetukuzwa kwelikweli na baadhi ya Wakenya hata kupachikwa kitangulizi cha "MTUKUFU" kabla ya jina lake, Rais Daniel Arap Moi.....

Nani alijua hata kuweza kutabiri tu kuwa, kufumba na kufumbua angetoweka yeye, chama chake na watu wake wa kikundi cha sifa kama mvuke wa moto?

Nakubaliana na wewe kabisa, kuwa, ni wakati wa Watanganyika wote kufikiri juu ya hatima ya uongozi wa Taifa letu nje ya Chama Cha Mapinduzi ( CCM) na wafuasi wake.....

Kwangu mimi haijalishi itakuwa CHADEMA na Tundu Lissu, Mbowe, Sumaye ama Nyalandu ama yeyote ndani humor; Ama ACT - Wazalendo na Zito Kabwe ama Bernard Membe ama mwingine yeyote ndani mwao humo.....lakini isiwe CCM na chapa yake, baasi inatosha sana.....

For sure, John Pombe Magufuli na CCM yake iwe mwisho 2020. Miaka 66 toka enzi ikiitwa TANU mwaka 1954 hadi ilipojibadilisha na kuitwa CCM mwaka 1977 inatosha....

Wamefanya waliyoweza kufanya, wameshindwa waliyoshindwa......

Kwa ufupi sana ni kuwa, mbwa huyu ni mzee sana. Hawezi kutuletea mawindo tena ili tuendelee kula kitoweo.....

Ana umri wa zaidi ya umri wa kustaafu binadamu kazini wa miaka 60, inatosha na wote tuseme inatoshaaaaa...!!
 
Dn
KAZI NZITO NA NYEPESI ALIYONAYO ANTIPHAS;

Huyu Jamaa anaweza kuwa na mzigo mzito sana ama mwepesi kuwafuta WATANZANIA machozi, na kuijenga TANZANIA mpya baada ya kuwaongoza kupata uhuru kwa Awamu ya pili.

Awamu hii ya pili ikiwa ni uhuru kutoka kwa kikundi cha watu waafrika wenzetu (The so called Elite) wanaojiaminisha na kujihakikishia wanabaki madarakani milele iwe hata kwa goli la mkono japo wamechokwa na wameshindwa kazi ya kuleta matunda ya Uhuru kwa kila mtanzania.

ugumu unakuja vipi..

ugumu unakuja pale ambapo kila mtanzania ambaye anataka mabadiliko ameelekeza masikio na matumaini yake kwa huyu bwana (Masiah/Mkombozi). Wote wakiamini kuwa atakuwa MTATUZI wa matatizo yao , iwe kisheria katika haki na uhuru wa kujieleza, kiuchumi na hata kielimu, Elimu ambayo haina mashiko ,imepitwa na wakati.

Urahisi uko wapi..

Matumaini na matarajio haya MAKUBWA yaweza kuonekana ni mambo yanayompa MZIGO MZITO mtu mmoja, lakini kiukweli inaweza kuwa rahisi kwake kwani ana sifa sifutazo;

1.Ni mtu anayeifahamu vyema historia sio tu ya Tanzania bali hata huko kwingineko duniani.

2.Anayajua vyema matukio na mambo mengi mbalimbali YALIYOPITA kwa kina na kwa mifano hai kitu kinachomjengea wezo mkubwa wa kutabiri YAJAYO.

3. Anayafahamu vyema matatizo ya Taifa hili kama vile sababu za kutonufaishwa na mali asili na rasilimali zetu, mikataba ya kilaghai, kero za muungano ambazo zimekuwa zikifunikwa na suluhu zake, sababu za kufeli kwa sera mbalimbali kama sera za kupambana na wahujumu uchumi kipindi cha Sokoine.

Anayafahamu maatizo hivyo hatapata taabu aanzie wapi. Kufahamu chanzo cha tatizo ni mwanzo mzuri wa kulitatua.

Hii ni tofauti kabisa na wengine ambao wamekuwa wakionesha nia ya kutaka kutuongoza kutatua matatizo ili hali mpaka leo hii wanauliza hawajui ni kwanini sisi ni masikini, hawajui fedha zinaibwaje ingawa wamehudumu ndani ya serikali hii kwa miongo kadhaa tena ndani ya baraza la maamuzi. Unaomba vipi kazi usiyoifahamu kwa undani? Sidhani kama huu ni wakati wa kujaribu wakati Taifa linahitaji matibabu liko mahututi?

4. Anauchukia na ana hofu ya UTAWALA wa MABAVU usiofuata sharia kwani anajua madhara yake, amekuwa akisisitiza utawala wa sharia, uhuru wa maoni, malumbano ya hoja . Amekuwa akitoa na kulaani kwa mifano mingi ya tawala zisizojali utu na njia bora za kutatua matatizo ya jamii kama akina Stalin, Hitler pamoja na oparesheni za akina Edward sokoine japo zlikuwa na nia njema.

5. Sio mnafiki, ni msemakweli na anao ujasiri wa kumkosoa, kumpinga ama kumsahihisha mtu waziwazi na bado akawa anamhusudu.

Amekuwa akikosoa waziwazi baadhi ya viongozi wanaosifika na kukumbukwa Mfano Mwalimu Nyerere ,Sokoine, Kikwete n.k. Hii ni ishara ya kiongozi mwenye uthubutu na muwazi pale unapokosea bila kubaki na chuki moyoni.

6. Ni mbobezi wa sharia na mtetezi wa haki , usawa kwa makundi yote iwe waliokuwa na vyama ama wasiokuwa navyo.
Ni wazi kuwa taifa baada ya uhuru linahitaji kuwa na mazingira yanayomfanya mwananchi ajione huru na mwenye haki juu ya rasilimali za nchi yake tofauti na iliyozoeleka sasa ambapo huwezi kuwa hata kiongozi wa ofisi ya umma pasipojuwa mshabiki wa chama kilichopo madarakani.

Taifa ni pana, lisiishie tu kwenye uchadema na uccm. wapo wasiopenda kujiunga na vyama

7. Amekuwa ni kiunganishi cha makundi mbalimbali licha ya tofauti za kiimani, kitamaduni, kiitikadi hata mbinu. Mfano amekuwa mtetezi wa wazanzibari wakiwemo masheikh wa uhamsho , amekuwa akiwaheshimu pia walioko chama tofauti nay eye akiwaita kwa majina kaka yangu, dada yangu ama ndugu yangu. Hiyo ni ishara ya kuwa ni kama kielelzo na kiunganishi cha UDUGU uliokwisha kuanza kupotezwa na chuki.

8. Sio kigeugeu, misimamo yake dhidi ya haki na usawa haibadiliki tangu akiwa shule hata alipoianza kazi yake rasmi miaka kibao iliyopita licha ya kubatizwa majina mbalimbali kama vile MCHOCHEZI.tangu miaka ya 90 anafahamika kama mtetezi wa wanyonge akiwaigania mamia ya wanakijiji dhidi ya wawekezaji waonevu walikaribishwa na viongozi walafi waliokuwa madarakani.

9. kutokana na kuwa shupavu katika kuusimamia ukweli , hivyo ni mtu ambaye hafungwi na nidhamu ya unafiki wa kumuonea haya usoni yeyote iwe ni mtu mkubwa kiasi gani. Hana deni la kulipa fadhila hivyo ni rahisi kwake kushuhulika na masuala yote ya ufisadi bila kubagua chambo na kuwaacha wakubwa.

MWISHO:

Pamoja na sifa hizi na nyingine nyingi alizonazo, tunamwombea na tunamsihi awe na MSAMAHA ,kwa yeyote anaeyesoma alama za nyakati anakubaliana nami kuwa huu ni wakati wa kujenga upya Taifa .

Na Taifa haliwezi kujengwa kwa kuendeleza gurudumu la VISASI bali kwa waliojiona wana haki sana kujishusha na kutubu walipokosea na wale walioonewa kusamehe kisha kuketi meza moja kujenga upya na kutibu majeraha ya TAIFA TANZANIA na AFRIKA kwa ujumla

View attachment 1204439
Ccm wamesahau dunia tunapita
 
KAZI NZITO NA NYEPESI ALIYONAYO ANTIPHAS;

Huyu Jamaa anaweza kuwa na mzigo mzito sana ama mwepesi kuwafuta WATANZANIA machozi, na kuijenga TANZANIA mpya baada ya kuwaongoza kupata uhuru kwa Awamu ya pili.

Awamu hii ya pili ikiwa ni uhuru kutoka kwa kikundi cha watu waafrika wenzetu (The so called Elite) wanaojiaminisha na kujihakikishia wanabaki madarakani milele iwe hata kwa goli la mkono japo wamechokwa na wameshindwa kazi ya kuleta matunda ya Uhuru kwa kila mtanzania.

ugumu unakuja vipi..

ugumu unakuja pale ambapo kila mtanzania ambaye anataka mabadiliko ameelekeza masikio na matumaini yake kwa huyu bwana (Masiah/Mkombozi). Wote wakiamini kuwa atakuwa MTATUZI wa matatizo yao , iwe kisheria katika haki na uhuru wa kujieleza, kiuchumi na hata kielimu, Elimu ambayo haina mashiko ,imepitwa na wakati.

Urahisi uko wapi..

Matumaini na matarajio haya MAKUBWA yaweza kuonekana ni mambo yanayompa MZIGO MZITO mtu mmoja, lakini kiukweli inaweza kuwa rahisi kwake kwani ana sifa sifutazo;

1.Ni mtu anayeifahamu vyema historia sio tu ya Tanzania bali hata huko kwingineko duniani.

2.Anayajua vyema matukio na mambo mengi mbalimbali YALIYOPITA kwa kina na kwa mifano hai kitu kinachomjengea wezo mkubwa wa kutabiri YAJAYO.

3. Anayafahamu vyema matatizo ya Taifa hili kama vile sababu za kutonufaishwa na mali asili na rasilimali zetu, mikataba ya kilaghai, kero za muungano ambazo zimekuwa zikifunikwa na suluhu zake, sababu za kufeli kwa sera mbalimbali kama sera za kupambana na wahujumu uchumi kipindi cha Sokoine.

Anayafahamu maatizo hivyo hatapata taabu aanzie wapi. Kufahamu chanzo cha tatizo ni mwanzo mzuri wa kulitatua.

Hii ni tofauti kabisa na wengine ambao wamekuwa wakionesha nia ya kutaka kutuongoza kutatua matatizo ili hali mpaka leo hii wanauliza hawajui ni kwanini sisi ni masikini, hawajui fedha zinaibwaje ingawa wamehudumu ndani ya serikali hii kwa miongo kadhaa tena ndani ya baraza la maamuzi. Unaomba vipi kazi usiyoifahamu kwa undani? Sidhani kama huu ni wakati wa kujaribu wakati Taifa linahitaji matibabu liko mahututi?

4. Anauchukia na ana hofu ya UTAWALA wa MABAVU usiofuata sharia kwani anajua madhara yake, amekuwa akisisitiza utawala wa sharia, uhuru wa maoni, malumbano ya hoja . Amekuwa akitoa na kulaani kwa mifano mingi ya tawala zisizojali utu na njia bora za kutatua matatizo ya jamii kama akina Stalin, Hitler pamoja na oparesheni za akina Edward sokoine japo zlikuwa na nia njema.

5. Sio mnafiki, ni msemakweli na anao ujasiri wa kumkosoa, kumpinga ama kumsahihisha mtu waziwazi na bado akawa anamhusudu.

Amekuwa akikosoa waziwazi baadhi ya viongozi wanaosifika na kukumbukwa Mfano Mwalimu Nyerere ,Sokoine, Kikwete n.k. Hii ni ishara ya kiongozi mwenye uthubutu na muwazi pale unapokosea bila kubaki na chuki moyoni.

6. Ni mbobezi wa sharia na mtetezi wa haki , usawa kwa makundi yote iwe waliokuwa na vyama ama wasiokuwa navyo.
Ni wazi kuwa taifa baada ya uhuru linahitaji kuwa na mazingira yanayomfanya mwananchi ajione huru na mwenye haki juu ya rasilimali za nchi yake tofauti na iliyozoeleka sasa ambapo huwezi kuwa hata kiongozi wa ofisi ya umma pasipojuwa mshabiki wa chama kilichopo madarakani.

Taifa ni pana, lisiishie tu kwenye uchadema na uccm. wapo wasiopenda kujiunga na vyama

7. Amekuwa ni kiunganishi cha makundi mbalimbali licha ya tofauti za kiimani, kitamaduni, kiitikadi hata mbinu. Mfano amekuwa mtetezi wa wazanzibari wakiwemo masheikh wa uhamsho , amekuwa akiwaheshimu pia walioko chama tofauti nay eye akiwaita kwa majina kaka yangu, dada yangu ama ndugu yangu. Hiyo ni ishara ya kuwa ni kama kielelzo na kiunganishi cha UDUGU uliokwisha kuanza kupotezwa na chuki.

8. Sio kigeugeu, misimamo yake dhidi ya haki na usawa haibadiliki tangu akiwa shule hata alipoianza kazi yake rasmi miaka kibao iliyopita licha ya kubatizwa majina mbalimbali kama vile MCHOCHEZI.tangu miaka ya 90 anafahamika kama mtetezi wa wanyonge akiwaigania mamia ya wanakijiji dhidi ya wawekezaji waonevu walikaribishwa na viongozi walafi waliokuwa madarakani.

9. kutokana na kuwa shupavu katika kuusimamia ukweli , hivyo ni mtu ambaye hafungwi na nidhamu ya unafiki wa kumuonea haya usoni yeyote iwe ni mtu mkubwa kiasi gani. Hana deni la kulipa fadhila hivyo ni rahisi kwake kushuhulika na masuala yote ya ufisadi bila kubagua chambo na kuwaacha wakubwa.

MWISHO:

Pamoja na sifa hizi na nyingine nyingi alizonazo, tunamwombea na tunamsihi awe na MSAMAHA ,kwa yeyote anaeyesoma alama za nyakati anakubaliana nami kuwa huu ni wakati wa kujenga upya Taifa .

Na Taifa haliwezi kujengwa kwa kuendeleza gurudumu la VISASI bali kwa waliojiona wana haki sana kujishusha na kutubu walipokosea na wale walioonewa kusamehe kisha kuketi meza moja kujenga upya na kutibu majeraha ya TAIFA TANZANIA na AFRIKA kwa ujumla

View attachment 1204439
Mbona mnatumia nguvu kubwa katika kumsifia na kumwabudu?Hadi mnakufuru eti masiha
 
5) Sio mnafiki, ni msemakweli na anao ujasiri wa kumkosoa, kumpinga ama kumsahihisha mtu waziwazi na bado akawa anamhusudu.

Hii namba 5 kidogo sio sawa alimponda lowasa kama fisadi kisha akamshafisha...
Huu ni unafiki
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom