Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Waheshimiwa nisaidie kitendawili hiki:
Tangazo la kazi limetolewa. Sifa za nafasi hiyo ninazo. Barua ya maombi na CV nimeandaa na kuomba kazi hiyo. Sasa wameniita kwenda kwenye interview pamoja na wengine walioomba na kuwa-short listed. Mimi sitaki kwenda kwenye interview hiyo kwa sababu nahisi kuna njama za kuniuliza maswali "mabaya" ili nikose kazi hiyo, lakini kazi naitaka sana. Je niipateje kazi hiyo bila kwenda interview. Je CV yangu itatosha kuwashawishi waajiri wanipe kazi hiyo na kuwaacha waliofika kwenye interview hiyo?
Hii ina tofauti gani na CCM? Udiwani, Ubunge na Urais wanautaka. maombi wamepeleka. CV zao (Ilani) wamepeleka. Waajiri ni Watanzania. Wamewaalika waombaji kwenye interview (Midahalo), lakini CCM hawataki kwenda, lakini wanasisitiza kuwa kazi wanaitaka. Je kazi wapewe?
Tangazo la kazi limetolewa. Sifa za nafasi hiyo ninazo. Barua ya maombi na CV nimeandaa na kuomba kazi hiyo. Sasa wameniita kwenda kwenye interview pamoja na wengine walioomba na kuwa-short listed. Mimi sitaki kwenda kwenye interview hiyo kwa sababu nahisi kuna njama za kuniuliza maswali "mabaya" ili nikose kazi hiyo, lakini kazi naitaka sana. Je niipateje kazi hiyo bila kwenda interview. Je CV yangu itatosha kuwashawishi waajiri wanipe kazi hiyo na kuwaacha waliofika kwenye interview hiyo?
Hii ina tofauti gani na CCM? Udiwani, Ubunge na Urais wanautaka. maombi wamepeleka. CV zao (Ilani) wamepeleka. Waajiri ni Watanzania. Wamewaalika waombaji kwenye interview (Midahalo), lakini CCM hawataki kwenda, lakini wanasisitiza kuwa kazi wanaitaka. Je kazi wapewe?