Kazi inapoendelea kila Rais anapohutubia Makamu na Waziri Mkuu nao wapo. Imekaaje hii?

Inawezekena ktk baadhi ya matukio kuna issues ambazo waziri mkuu anahusika sana ktk kuzitolea ufafanuzi kwa nafasi yake,
Haina maana kwamba presdent anaweza kutoa ufafanuzi kwa mambo yote kwa wakati mmoja, hivyo anahitaji pengine kuandamana na top officials japo si ktk matukio yote.
Suala la usalama nadhani wao wanajua zaidi wanajipangaje kuliko hata sisi ambao hata mgambo hatujapita.
 
Kwanini unawataja waziri mkuu na makamu wa rais bila kusema chochote cha kumkosoa moja kwa moja aliyewaalika?

Siku hizi CDM mnajifanya kumpigia debe rais aliyeko madarakani baada ya kugundua ni sehemu salama ya kujifichia (siku shamba la miwa likichomwa moto ndio mwisho wa wanyama nyemelezi wakianza kutimua mbio bila mafanikio, mko kwenye mtego wa panya vizuri sana

Umesoma CDM wapi katika bandiko langu?

Sisomi umataga kwenye bandiko lako:

Kabla sijautumia nikuulize kwanza wewe ni mataga?
 
Inawezekena ktk baadhi ya matukio kuna issues ambazo waziri mkuu anahusika sana ktk kuzitolea ufafanuzi kwa nafasi yake,
Haina maana kwamba presdent anaweza kutoa ufafanuzi kwa mambo yote kwa wakati mmoja, hivyo anahitaji pengine kuandamana na top officials japo si ktk matukio yote.
Suala la usalama nadhani wao wanajua zaidi wanajipangaje kuliko hata sisi ambao hata mgambo hatujapita.

Hotuba ni one way communication. Nani anafafanua nini kwenye hotuba ya mheshimiwa Rais?

Acha tuone nani atafafanua nini.
 
Mataga ni nini? Unaamanisha kutaga mayai, halafu iweje? Ebo!!

Mbona mapovu hivyo kama ya Omo jombi? Wengine hawatagi mayai. Wenyewe wapo watakwambia wanataga nini?

Kumbuka sijakuita mataga ila nimekuuliza kama wewe ni mmoja wao hapo nikiwa nakukumbusha accordingly kuwa ni fyongo mno kuleta u CDM pasipo husika na hata bila kuuliza!

Why do you take things so, for granted? CDM hata kusiko husika?

Wajameni!

Mwimbaji mmoja aliimba, anasema - huo ni ushamba!
 
Hotuba ni one way communication. Nani anafafanua nini kwenye hotuba ya mheshimiwa Rais?

Acha tuone nani anafafanua nini.
Ndo kitu nachojaribu kusema hapa, kwamba president anahotuba yake, pm nae ananafasi yake na atazungumza vitu tofauti kabisa ambavyo navyo ni muhimu kwa taifa, japo nimesema si Mara zote.
 
Ndo kitu nachojaribu kusema hapa, kwamba president anahotuba yake, pm nae ananafasi yake na atazungumza vitu tofauti kabisa ambavyo navyo ni muhimu kwa taifa, japo nimesema si Mara zote.

Wacha tumsikilize mama sasa.

Zama mpya hizi itapendeza zaidi siku zingine mama atokee peke yake.

Mama anatosha sana.
 
Huyo ni wale walioamini kuwa Mbowe angekuwa waziri mkuu nchi hii. Sasa mambo yamegeuka jamaa anakuja na uzi usioeleweka hapa jamvini

Tuliza mananihii wewe - DC mpendwa. Tunamsikiliza mama, tusipitwe mambo.

Ametoka kivingine - kila mtu na barakoa.

Tunasubiria ana nini kuhusu nyungu, bupeji, covidol na zile juice za mwendazake tokea Madagascar.
 
Mabibi na mabwana awamu hii ina maajabu yake. Imekuwa kila Mama Samia anapokuwa anahutubia hapa nchini, basi waheshimiwa: Mpango, Majaliwa na vigogo wa juu nao never miss.

Haiyumkiniki vigogo hawa walipenda pia kuwapo Kampala na Nairobi.

Hiiiiii bagosha!

Wajameni, hizi gharama za kuwasafirisha hawa vigogo wote tokea walipokuwa kwenda kwenye hizi hafla zinakuwa je? Kwani nao wakikaa kwenye runinga au radio kama kina sisi haitoshi?

Wajameni si mmpe mama nafasi afanye vitu vyake?

Hii kufuatana fuatana hii si inaweza kuwa na athari nyingi tu zikiwamo za kiusalama, kuoneana aibu kwenye kutumbuana mubashara nk?

Wamekuwa kama kumbi kumbi. Bibi mbele bwana nyuma!

Au nasema urongo ndugu zangu?
Wasukuma orodhesheni madukuduku yenu yote mama ayafanyie kazi, maana nyinyi ni yatima kwa hakika
 
hakuna kitu kizur kama kuonesha strong front zmbele za watu hasea wawekezaji.....hiyo ni kuonesha team work na umoja
 
Mabibi na mabwana awamu hii ina maajabu yake. Imekuwa kila Mama Samia anapokuwa anahutubia hapa nchini, basi waheshimiwa: Mpango, Majaliwa na vigogo wa juu nao never miss.

Haiyumkiniki vigogo hawa walipenda pia kuwapo Kampala na Nairobi.

Hiiiiii bagosha!

Wajameni, hizi gharama za kuwasafirisha hawa vigogo wote tokea walipokuwa kwenda kwenye hizi hafla zinakuwa je? Kwani nao wakikaa kwenye runinga au radio kama kina sisi haitoshi?

Wajameni si mmpe mama nafasi afanye vitu vyake?

Hii kufuatana fuatana hii si inaweza kuwa na athari nyingi tu zikiwamo za kiusalama, kuoneana aibu kwenye kutumbuana mubashara nk?

Wamekuwa kama kumbi kumbi. Bibi mbele bwana nyuma!

Au nasema urongo ndugu zangu?
Tulia wewe hii nchi ilichezewa sana, acha kazi iendelee
 
Uyo ni msukule wa marehemu magufuli, mbowe Hana mazuzu Kama uyo, mwenzenu uyo

Heri umemwambia. Tatizo la misukule kutokujua kuwa yenyewe ni misukule kweri kweri, hiyo tu ni shughuli pevu. Misukule ya leo eti hata ina uthubutu wa kumilikishana wenye nayo.

Hiiiiii bagosha!
 
Back
Top Bottom