dronedrake
JF-Expert Member
- Dec 25, 2013
- 23,171
- 54,646
00. Kua Mataga wa buku 7
Pia volt 50 ac hazitoshi kuua mtuHiyo namba 6 umeweka chumvi.
Hamna fundi anapandishwa kwenye line zenye. Msongo mkubwa wa umeme zikiwa energised.
Si kweli....wapo wanaofanya kazi live line kwenye transmission lines....hata tz wapo!Hiyo namba 6 umeweka chumvi.
Hamna fundi anapandishwa kwenye line zenye. Msongo mkubwa wa umeme zikiwa energised.
Pamoja na wachoraji tattooMkuu umesahau Hawa wanaowasafisha dada zetu kucha hasa za miguuni.
Mkuu tuheshimishe na sisi.10. Kuendesha Malori
Kazi hii ni hatari kwasababu kuu mbili, kwanza ni umbali ambao madereva hawa hulazimika kuendesha gari na la pili ni aina za barabara wanazokutana nazo, nyingi zikiwa ni za hatari sana ikiwemo miteremko na milima mikali.
Kwa hapa nchini Tanzania, maeneo kama Kitonga na Sekenke kwa miaka ya nyuma yalikuwa yakichukua roho za madereva wengi kutokana na mazingira yalivyokuwa hatarishi.
Takwimu zilizokusanywa 2014 zinasema zaidi ya madereva wa malori 700 duniani walipoteza maisha mwaka huo.
09. Askari Magereza
Unaweza kushangaa lakini ukweli ndio huo, hii ni kazi ambayo usipokuwa makini kwa 100% unaweza kupoteza maisha kwa haraka sana.
Asilimia kubwa ya wafungwa ni watu hatari, baadhi yao wamehukumiwa kifungo cha maisha hivyo hawana cha kupoteza, wanaweza kukudhuru bila kuhofia chochote.
Gereza kama la Gldani lililopo Georgia linatumika kuhifadhi wafungwa waliohukumiwa kwa makosa makubwa na ya hatari. Katika gereza hili askari wa zamu hawezi kuwa mmoja. Matukio ya kupigana na ubakaji ni kitu cha kawaida na askari hulazimika kuwa waangalifu wakati wa kushughulika na mambo hayo.
08. Wafanyakazi Kwenye Mitambo ya Nyuklia
Mwaka 2011 kulitokea tukio la nyuklia kuvuja na kusababisha kiasi kikubwa cha mionzi kusambaa. Ili kuzuia isilete madhara ilikuwa ni lazima wataalamu wasogee eneo hilo na kuziba kurudisha katika hali ya kawaida.
Hatari ya kusogea eneo hilo ilikuwa kubwa sana kwavile mionzi hiyo ilikuwa na sumu kali kwa mwili wa binadamu ambapo watu wengine waliaswa kukaa umbali wa kilomita nyingi kutoka eneo la tukio.
Lakini wafanyakazi walilazimika kuendelea kuwepo jirani ili kufunga hali iliyopelekea wengi wapoteze maisha. Hii ni kazi ya hatari hasa.
07. Uchimbaji Mafuta
Wafanyakazi katika machimbo ya mafuta hulazimika kufanya kazi kwa masaa hadi 16 kwa siku. Wakati wakiendelea na kazi wanapaswa kuwa makini mno na mashine zinazozunguka ambapo kosa moja tu linaweza kupelekea ajali mbaya.
Kwavile uchimbaji huu hufanyika baharini, wafanyakazi hawa wanapaswa pia kuwa makini na mawimbi ya bahari huku mafuta yenyewe yakiwa ni hatari namba moja.
Mwaka 2010 wafanyakazi 11 walipoteza maisha katika machimbo ya mafuta nchini Mexico baada ya kutokea kwa mlipuko mkubwa.
06. Mafundi Wanaojenga 'Line' za Umeme
Umeme wa Volti 50 tu unatosha kuondoa uhai wa binadamu, gridi ya umeme huweza kubeba hadi Volti 800,000 unadhani unaweza kuua watu wangapi?.
Fikiria fundi anapanda juu a nguzo kubwa umbali wa takribani mita 50 na kulazimika kuwa makini na vitu viwili;
1. Asianguke chini
2. Asikosee kugusa umeme
Kosa lolote kati ya hayo yanaweza kuuondoa uhai wako ndani ya sekunde chache tu.
05. Mwandishi wa Habari za Kivita
Mwandishi wa habari hulazimika kuingia katikati ya uwanja wa vita ili apate picha na taarifa za matukio zenye ubora zaidi.
Anachoweza kufanya ili kujitetea ni kuwaa kivazi chenye logo ya 'PRESS' kifuani na mgongoni akitumaini hilo tu litamsaidia asipigwe risasi, hii ni kazi inayohitaji moyo wa ujasiri.
04. Wachimbaji Makaa ya Mawe
Mfanyakazi katika migodi ya makaa ya mawe hulazimika kufanya kazi kwa wastani wa masaa 12 kila siku na katika mazingira hatarishi ambayo nafasi ni finyu na unaweza kupata shida ya kupumua kutokana na vumbi la makaa hayo.
Kupumua katika vumbi hili ni hatari sana lakini endapo mfanyakazi atazimia basi tambua kuwa yupo chini ya ardhi kwa umbali wa zaidi ya mita 100. Kama ana bahati basi atakufa muda huo huo, lakini kama hana bahati basi anaweza kunasa huko ardhini na akafa taratibu kutokana na njaa.
03. Upasuaji wa Mbao
Unaweza kudhani msumeno wa umeme ndio kitu pekee cha hatari katika kazi hii, unajidanganya kwavile watu wengi hupoteza maisha kwa kutojua tu ni upande upi mti utaangukia baada ya kuukata.
Ukiangukiwa na mti mkubwa kama huo hapo pichani kunakuwa hakuna namna ya kukuokoa na huo unakuwa mwisho wa maisha yako.
02. Wanaanga
Siku utakayoamua kuwa Mwanaanga basi tambua tayari una asilimia saba za kupoteza maisha ukiwa katika kazi zako.
Kosa moja tu wakati wa kurusha roketi linaweza kusababisha kwenda uelekeo usio sahihi na kupotea, roketi kulipuka, hewa safi ya Oxygen ambayo husafiri nayo kwa matumizi ya huko angani huweza kuvuja au mtu akapotelea angani moja kwa moja.
01. Uvuvi
Kazi hii imeshika namba moja katika orodha ya kazi 10 za hatari zaidi duniani. Utamu wa samaki kwenye migahawa unatufanya wengi tusahau hata mchakato wa upatikanaji wake.
Hii ni kazi ngumu na ya hatari sana wala si masihara. Mfanyakazi hulazimika kufanya kazi kwa masaa hadi 24 kila siku akipambana kumwaga maji nje ya boti, kunyanyua vitu vizito na kuwa makini na mawimbi ambayo yanaweza kumuondoa mtu yeyote kwenye boti.
Ukimuuliza mkongwe yeyote wa kazi hii kama aliwahi kunusurika na kifo majini basi atakuambia 'NDIO'.View attachment 1766905
Mkuu just relax kazi zote zina changamoto zake! lakini kuna zingine zina changamoto zaidi baadhi nimejaribu kuzielezea na zingine wadau wanajazia. Kuna kazi mtu anaweza kufanya na mwingine asiweze kwa sababu kazi hiyo ni pasua kichwa.Source ?
Umekaa ndo ukafikiria hicho
me naomba nikuulize swali zipi ni kazi salamaa?