Kaze anaihujumu Yanga, mtimueni haraka sana kwa mustakabali wa klabu

Wabongo kwa ujuaji kama Nabi aliomba siku 100 ili falsafa yake ifanye kazi kwenye timu tunawezaje kumulaumu Kaze kusimama mechi tatu? unataka kuniambia hizi mechi tatu tumecheza Nabi hahusiki kwa lolote?
wewe sio shabiki wa yanga
 
Simaanishi kwamba anafanya fitna, la hasha ila uwezo wake mdogo kimbinu na ufundishaji ni zaidi ya hujuma. Nilianza kuwa na mashaka na uwezo wa Kaze kwenye mechi ya Yanga vs Gwambina msimu uliopita akiwa kocha mkuu pale alipo wapumzisha wachezaji muhimu eti kwa sababu anaogopa wataumizwa waikose mechi ya Simba matokeo yake akaishia kutoa draw na Gwambina na kupunguza pengo la point dhidi ya Simba.

Mechi iliyo fuatia ndio nika zidi kuwa na mashaka zaidi, ilikuwa ni Simba vs Yanga ya goli moja moja Yanga wakifunga kupitia Sarpong na Simba wakisawazisha kupitia Onyango dakika za majeruhi. Mechi hiyo Yanga walitawala kipindi cha kwanza na Simba tayari walikuwa wameisha elekea kibla. Kwa mshangao wa wengi Yanga wamerudi kipindi cha pili eti wamepaki basi, SHAABASH. Ulisikia wapi hiyo? Ulisikia wapi kwenye mechi ya derby katikati ya ligi timu inapaki basi kuanzia dakika ya 46 ya kipindi cha pili? Matokeo yake Simba wakasawazisha goli kizembe kabisa katika mechi ambayo Yanga walipaswa kushinda.

Akiwa kama kocha msaidizi alifanya madudu ya karne huko Zenji. How comes unamtoa Mshery ambae amecheza dakika 90 na ameshazoea mechi damu imechemka kisha unamuingiza shati akae golini ? uzembe wa Kaze unaigharimu sana Yanga.

Mechi dhidi ya Namungo Yanga walishinda kwa juhudi binafsi za wachezaji.

Mechi dhidi ya Simba Yanga walipaswa kushinda mechi hiyo without a doubt ila Kaze ndio ame ihujumu timu. How comes unamtoa Moloko ambae alimzuia Shabalala asipande unamuingiza Nkane ambae wachezaji wa Simba hawamuogopi wanakiona kitoto tu ambacho hakina madhara? Matokeo yake Yanga wakazidiwa sana baada ya sub ya Moloko na walikoswa goli la dakika za mwisho achilia mbali shuti la faulo ya Boko ambalo lilipaa juu.

Haya sasa huko Kigoma ndio kichefuchefu, hivi Yanga mnashindwa vipi kuwafunga Ruvu Shooting na Rose Muhando juu? Yanga mlikuwa mnaizidi Simba kwa tofauti ya point 12 hata Simba wakishinda viporo vyao lakini kwa uzembe wa Kaze point zimerudi zile zile 10. Msipo angalia hata mwaka huu ubingwa mtaukosa kwa sababu Simba bado wanautaka ubingwa kwa udi na uvumba and they mean business. Ninyi Yanga endeleeni kufanya ajizi huku mkijua wazi kuwa ajizi nyumba ya njaa.

Kwa ubora wa kikosi cha Yanga, hata ukimpa Zuchu hawezi kutoa draw na Ruvu Shooting.

# I have never heard a Young Africans fan says he is down with Kaze.

# Kaze must go.

# And if u wanna be down with Kaze, then......
Unaqeza kutuonesha cheti chako cha ukocha?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom