Kauli za "walitaka kunihonga" mara ooh " wananiomba niwateue" mbona hazikuwepo awamu zilizopita?

Zero Hours

JF-Expert Member
Apr 1, 2011
12,944
18,652
Hizi kauli za mara ooh " walitaka kunuhonga" mara " wananiomba niwateue" mimi kibinafsi zinanikera sana kwa sababu kwanza zimekaa kinafiki na pili zimekaa kimipasho kama sio taarabu.

Kwa mfano mimi kibinafsi huwa namchukia mwanamke anayekuja kwangu nakuanza kujitamba kwamba mara ooh flani anataka kunihonga gari mara hoo flani anataka nimchague yeye. Mara nyingi wanawake wa aina hii huwa ni waongo na wanapenda majivuno.

Sasa tukija kwenye upande wa siasa unakuta kiongozi anakuja kujitamba eti nilitaka kuhongwa. Huwa najiuliza, inamaana Takukuru hajui inafanya nini. Na hata hao Takukuru wapo tu wanakodoa macho hawawezi hata mchukua maelezo na kufanya kazi yao?

Kusema ukweli hii misemo haikuwepo awamu iliyopita. Mi nachoona hapa, Maigizo yanazidi kiwango cha bongo movie.

Unakuja kujitamba, "Ooh...wapo wengi wananiomba omba". Wewe Kwani umekuwa Yesu?

Mbona Nyie mnakujaga kutuomba sisi kura ila hatujitambi????

Tena ndye yulee aliye kuwa anatuombaomba kura mpaka anapiga pushup.

Alfu nilichogundua, kumbe vyeo mnaombana...Duh!!! Na mimi naombaa.... asee.
 
84b16e73241c1518be291f714ceb85a7.jpg


Kidume cha vyama vyote vya siasa
 
Sijawahi kuona msukuma mpenda sifa kama huyu wa chattle ni shida eti hapa mjini. kila siku anataka aonekane kwenye fenti page, kila siku ni lundo la uteuzi then anaanza kuapishwa mmoja mmoja ili aendelee kuuza sura. Mara tena malori ya uchafu sijui kwa kuwa yeye ni dereva wa lori aarhg ama kweli msema kweli ni mpenzi wa dedi wa Gairo
 
Sijawahi kuona msukuma mpenda sifa kama huyu wa chattle ni shida eti hapa mjini. kila siku anataka aonekane kwenye fenti page, kila siku ni lundo la uteuzi then anaanza kuapishwa mmoja mmoja ili aendelee kuuza sura. Mara tena malori ya uchafu sijui kwa kuwa yeye ni dereva wa lori aarhg ama kweli msema kweli ni mpenzi wa dedi wa Gairo
Huyo Dedi Gairo inaoneka naye aliomba au aliombwa..
 
Back
Top Bottom