Kauli za Rais Magufuli na Mwita Waitara ni kauli za hatari sana kwa Tanzania ijayo

gemmanuel265

JF-Expert Member
Feb 16, 2016
8,485
18,045
Baada ya Tundu Lissu kuipinga ile ripoti ya pili ya madini maarufu ripoti ya makinikia ya Prof Osoro na kuiita uchafu wa kitaaluma, Rais wa Tanzania mh John Magufuli alinukuliwa na vyombo vya habari akitamka maneno ambayo aliona kuna mtu anakwamisha juhudi zake za kupambania rasilimali za nchi

Mh Rais Magufuli alitamka maneno haya "hatuwezi kuwa vitani halafu askari aliye mbele ageuke na kuanza kushambulia wenzake, huyo hatumwachi salama, hawezi kitugeuka tukamwacha" haya ni maneno ya hatari sana kwa Tanzania ijayo yenye umoja wa kitaifa.

Kuna clip inasambaa kwenye mitandao ya kijamii inayoaminika ni ya Naibu Waziri wa Tamisemi Mwita Waitara naona naye karejea maneno yenye kufanana sana na ya Rais Magufuli

Waitara anasema tuko kwenye vita ya kiuchumi anapotokea mtu anataka kutukwamisha lazima tumuwahi

Anasema kuna mtu anazurura huko nje kukwamisha juhudi za rais Magufuli, hivyo dawa yake ni kumtanguliza

Anasema tumepanda kwenye mtumbwi ambapo mmoja ameanza kuutoboa ili tuzama, anasema mtu huyo dawa yake ni kumtanguliza ndani maji

Hizi kauli za hawa viongozi ni kauli za hatari sana japo watu wanaweza kuona ni kauli zisizo na athari zozote kitaifa kwa wakati huu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizi ni kauli chochezi. Zinapotolewa na viongozi huwa ni kauli hatari sana.
 
hizo nikauli za kishujaa zilizojaa uthubutu wa hali ya juu na uzalendo wa nchi uliotukuka but the question is; zinatumikaje na kwa nani hv wanaemkusudia ni adui kweli wa taifa( na si waserikal)
 
The law is too strong for the weak and too weak for the strong - Henry Kissinger
 
Vita vya uchumi ni vigumu labda kuliko vita ya kupigania uhuru wa nchi kujitawala.

Katika vita hii maadui wengine sio visible,pia kuna collateral damage kibao ili kufanikisha ushindi.

Lakini kibaya zaidi washiriki wake wanaweza kuwa watu watiifu lakini wasiwe na mbinu za madeni.
 
Hizi kauli za hawa viongozi ni kauli za hatari sana japo watu wanaweza kuona ni kauli zisizo na athari zozote kitaifa kwa wakati huu

Hata wewe kama unalipwa na wazungu wambie wakupe uraia wa nchi zao, hunafaida ya kuwa mtanzania, ikiwa unawatete Mabwana zenu waibe maliasili zetu kwa kivuli cha demokrasia
 
Hata wewe kama unalipwa na wazungu wambie wakupe uraia wa nchi zao, hunafaida ya kuwa mtanzania, ikiwa unawatete Mabwana zenu waibe maliasili zetu kwa kivuli cha demokrasia

Hakuna mzungu anaweza kuja kuiba rasilimali hapa nchini, ni lazima akae mezani tena na viongozi walioko madarakani wakubaliane jinsi ya kuchimba na maslahi ya taifa. Hapo Lissu anawezaje kuwahakikishia hao wazungu kuiba rasilimali zetu?
 
Wanapanga kuua Watanzania kwa misingi ya dhana zao fake za Vita ya kiuchumi. Rasilimali wawagawie bure Wazungu wao, halafu wajifanye mbuni kuanza mauaji ya watu wasio na hatia. Hivi Watanzania wakichachamaa leo dhidi ya viongozi wa CCM na serikali yake Nani miongoni mwao atabaki salama!!?
Waambieni kuna kesho, akina Waitara wasiitazame Leo kwa ulevi wao!!!
 
Kuwa kiongozi wa kisiasa ni kukubali kutumia ushawishi wa kisiasa kupata ufuasi na uungwaji mkono kwa maono yako. Haya mambo hayahitaji mabavu hata kidogo. Isitoshe kuna tofauti kati ya kupinga na kukosoa. Ukiona viongozi wanaoitwa ni wa kisiasa wanatumia nguvu nyingi na mabavu kwa kwa mambo ya kisiasa kabisa ujue kuna kosa limefanyika; hao hawakustahili kabisa kuwa viongozi wa kisiasa kwa sababu hawajui hata maana ya uongozi wa kisiasa! That is the bottomline.
 
Back
Top Bottom