Uchaguzi 2020 Kauli za mgombea wa CHADEMA zinashangaza sana

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Uchaguzi wa mwaka huu umekuwa wa ajabu sana. Maana ukilinganisha na chaguzi zilizopita mwaka huu ni vituko na mambo ya ajabu sana.

Okiondoa uchaguzi wa mwaka 2015 miaka ya nyuma wapinzani walikuwa na hoja. Na mikutano yao ilikuwa na hamasa. Nakumbuka mwaka 2010 alikuwa akisimama Dk Slaa unaona uwanja mzima unasisimka. Maana mbali na kuibua madudu ya ufisadi lakini alikuwa anatoa nondo za maana juu ya namna gani atalifanyia taifa letu kama angelishinda.

Mwaka huu ni dalili kuwa CHADEMA hawakuwa na utayari wa kuja kupambana na Ccm ili kuchukua dola.

Mgombea wa CHADEMA anatoa hoja za ajabu sana kiasi kwamba anatia aibu. Mfano anadiliki kusema eti sababu Tanzania ni nchi ya kitropiki basi mradi wa JNHP hauna tija na kuwa hautakuwa na ufanisi,sababu tu mvua sio nyingi. Hivi hii inaingia akilini! Yaani anasema kuwa bora tungeendelea kujenga uzalishaji umeme wa gas pale Kinyerezi. Hivi hajui Kinyerezi phase 1& 2 ni kama MW 200 tu. Ujenzi wake umechukua muda mrefu.

Lakini JNHPP inajengwa kwa miaka mitatu na itapokamilika mwakani ni Mw 2100 zitazalishwa kwa mkupuo. Na hoja anazotoa kuwa umeme wa gas una gharama kidogo kuliko wa maji ni ukakasi na zinamuondolea sifa za kuwa kiongozi.

Mimi binafsi nilitarajia ampongeze JPM kwa kujenga mradi kama ule kwa pesa za ndani kuliko kuleta habari kama hizi ambazo zinashangza sana. Ila mimi siwezi kushangaa maana huu mradi hata mabeberu walikuwa wanaupinga na mgombea wa Chadema anajinasibu kuwa yupo karibu na Mabeberu

Je, kwa hoja kama hizi zisizo na kichwa wala miguu CHADEMA mlistahili kuwa na mgombea kama huyu? Kwanini msingeziua tu na kutafuta madiwani na wabunge kama hamna mgombea!
 
Sasa wewe unabishana naye wakati alikueleza kuwa alikuwa kwenye utafiti kuhusu hayo mambo kwa miaka mitatu tena huko Duniani? Yule mwenzako anasema hataki kwenda Ulaya maana Ulaya anaijenga Tanzania ndiyo siyo wa ajabu?
 
Fedha za Ndani maana yake fedha za kodi zetu kujengewa ni haki yetu sasa kwanini aue na watu apoteze na watu wawalawiti Mashekhe wazulumu wafanyakazi na Wafanyabiashara na wakulima wa korosho
Ahaaa. Ameua wapi? Acheni uhuni. Masheikh kawafanyia hayo maovu lini?
 
Hili hata mimi nilishangaa, ni kweli Lissu anatoa haya kwenye ilani ya CDM au ni maoni yake binafsi, maana kila mtaalam anajua umeme wa maji una gharama nafuu zaidi ya umeme wa jua na gesi, sasa mgombea urais, Lissu kuja kusema JNHPP ( Stigler’s gorge) ni ghali zaidi ya umeme wa jua, unatambua tu uropokaji umechukua nafasi yake na CDM hawakujiandaa au hawakumuandaa Lissu kuja kugombea kama anaropoka asiyoyajua.
 
Mnadanganywa ukiona mkandarasi ametoka nje ya Tanzania ujue ni pesa za mkopo au msaada wa mabeberu. JPM hawezi uza korosho akapeleka pesa Misri.
Pesa zinapatikana kwa kodi zinazoliopwa. Sio mpaka uuze korosho.
 
Hili hata mimi nilishangaa, ni kweli Lissu anatoa haya kwenye ilani ya CDM au ni maoni yake binafsi, maana kila mtaalam anajua umeme wa maji una gharama nafuu zaidi ya umeme wa jua na gesi, sasa mgombea urais, Lissu kuja kusema JNHPP ( Stigler’s gorge) ni ghali zaidi ya umeme wa jua, unatambua tu uropokaji umechukua nafasi yake na CDM hawakujiandaa au hawakumuandaa Lissu kuja kugombea kama anaropoka asiyoyajua.
Mwaka huu wanavuna aibu ya mwaka.
 
Sasa wewe unabishana naye wakati alikueleza kuwa alikuwa kwenye utafiti kuhusu hayo mambo kwa miaka mitatu tena huko Duniani? Yule mwenzako anasema hataki kwenda Ulaya maana Ulaya anaijenga Tanzania ndiyo siyo wa ajabu?

Kwa hiyo wataalum wa Lissu wamemuambia umeme wa jua ( solar) , upepo na umeme wa gesi ni gharama ndogo zaidi ya umeme wa maji, na CDM pia wamekubali na kuweka kwenye ilani yao bila kufikiri, kama mambo basics hivi hamjui mnaropoka uongo, mnachojua ni nini sasa?
 
Sasa wewe unabishana naye wakati alikueleza kuwa alikuwa kwenye utafiti kuhusu hayo mambo kwa miaka mitatu tena huko Duniani? Yule mwenzako anasema hataki kwenda Ulaya maana Ulaya anaijenga Tanzania ndiyo siyo wa ajabu?
Utafiti gani unaonyesha umeme wa gas ni cheap kuliko Hep? Utafiti gani unaonyesha Stiegler's gorge maji yatakosekana sababu ni tropical area. Maana hata Wajerumani walioanga kuzalisha umeme miaka hiyooo. Sasa mgombea wenu anadanganya watu!
 
Kwa hiyo wataalum wa Lissu wamemuambia umeme wa jua ( solar) , upepo na umeme wa gesi ni gharama ndogo zaidi ya umeme wa maji, na CDM pia wamekubali na kuweka kwenye ilani yao bila kufikiri, kama mambo basics hivi hamjui mnaropoka uongo, mnachojua ni nini sasa?
India wanatengeneza umeme wa jua wa megawati 10000 kwa trilioni 8, tanzania tunatengeneza umeme wa maji (stieglers gorge) megawati 1200 kwa trillion 6. sasa hebu tueleze kuwa ni umeme upi wenye gharama hapo?
 
India wanatengeneza umeme wa jua wa megawati 10000 kwa trilioni 8, tanzania tunatengeneza umeme wa maji (stieglers gorge) megawati 1200 kwa trillion 6. sasa hebu tueleze kuwa ni umeme upi wenye gharama hapo?
Weka ushahidi unachosema.
 
Back
Top Bottom